Baada ya kupata video hizi toka YouTube na kuziweka hapa, sikuwa na matarajio kuwa zitawafurahisha watu. La hasha. Na tovuti hii haiweki habari za kufurahisha tu, bali kufikirisha. Lengo langu kuu ndilo hilo. Kuweka kinachonikamata akili na kunisababisha mtu awze au kufikiri "ni sababu gani hasa iliyomsababisha mtu kusema hivi? au kutenda vile nk nk," si kuchekesha tu au kukejeli wengine kwa starehe zetu.

Mtu usiingie katika mapambano halafu, kama mbuni ujitahidi kuficha kichwa pekee ndani ya shimo, kisha mwenyewe ujione upo salama il hali kiwiliwili chote kipo nje.

Vile vile, tusisahau kuwa mtu uingiapo vitani, adui yako humchagulii silaha atakayokupiga nayo.

Hivyo video hizi nimeziweka makusudi kwa wasiofahamu wazione, na kwa wale wanaozifahamu, basi "warudishe mapigo" kuielimisha jamii ikiwa kinachotamkwa ni upotofu. Yawezekana ukawa mwenye akili na mwepesi kung'amua "mpunga" na "chuya", lakini usisahau wengine huhitaji "kupeta" au "kuchekecha" ama "kutafuna" kwanza kabla ya kujua ipi kweli "pumba" na ipi ndiyo "chuya", ndivyo tunavyotofautiana kiakili.

Tusijisahaulishe kuwa tunawalalamikia wananchi ati wanawachagua viongozi wasiofaa na papo hapo hatuwaelimishi. Ikiwa mawazo yao ndiyo kama yaliyomo kwenye video hizi au ni wepesi kuamini ujumbe uliopo kwenye video hizi, bila kutizama video na kuyafahamu, tutaanza vipi kumwelimisha huyu mwananchi? Tutamhubiria? Mbona wanahubiriwa sana tu Makanisanina Misikitini lakini maovu yanaenelea? Mi nadhani ili kutoa elimu maridhawa, inampasa mwelimishaji ajue awazacho mtu ndiposa ajue namna ya kuchukuliana na kumwelimisha yule wanayetofautiana mtizamo. Hapo ndipo malumbano ya hoja yanapokuwa sawia. Haya mnayoyaona kwenye video ni muhtasari na uwakilishi wa mawazo yaliyotanda katika jamii.

Tusiwe waoga wa kufahamu habari tusizozipenda. Tusipende kukaa kwenye "comfort zote" na kutaka habari za kutufurahisha tu. Kufanya hivyo ni kupoteza fursa ya kumsoma mpinzani wako anavyokuharibia.

Changamoto
Ikiwa kweli wapo wanaokerwa na video hizi, ni hatua gani wanachukua nao "kuwafukunyua" wapinzani wao? Nachelea kusema, mbinu ya "zuia isionekane" na "jidai hatufahamu", hiyo ni mbinu iliyofeli.

Hizi ni siasa za tit-for-tat. Stepping into the ring, means you are ready for a fight. If you have the potential to attack and destroy me, so do I. Dare to show me what you've got and I'll show you what I've got.
credit: hanskara
 


Comments

28/09/2010 12:54am

Ipo siku Dr. Slaa atawaumbua watu hadi kuyakimbia madaraka ambayo wanayatafuta kwa udi na uvumba.

Tusisahau Newton's third law of motion: In every action there is equal and opposite reaction.

Reply
kiva
28/09/2010 1:05am

mie hata kama ningekuwa simuungi mkono silaa bado sioni kigezo cha kukimbia mke au kukimbia upadri ni ishu mke kitu gani bwana hata mwinyi alikuwa nao matala lakini hao wake hatuna haja nao sie twataka kiongozi na sio mke wala mume wa mtu , kazi ya uraisi si kushindana kukaa na mke au kumuacha kwanza sie mke wake wa kazi gani na sisi ,hakika hapa CCM ina hoja dhaifu sana na hakika kwa staili hii chama kinapotea njia na hakina maisha marefu na upadri kwani upadri wake unatusaidia nini na sidhani kama ni kipimo sahihi

Reply
Makoba
28/09/2010 3:43am

Mtanzania yeyote Mzalendo wa kweli, mwenye akili timamu, asome habari hii. Yeyote yule asiye na mtindio wa ubongo, wala mtumwa wa hila chafu, anaalikwa kusoma. Hata wale wenye udumavu wa kiakili, na utando wa buibui na tongotongo za ufisadi za CCM, karibuni msome. Jielimishe , hakuna kulipia, ni bure! Soma kwa makini, kisha awashirikishe ndugu, jamaa na marafiki zake popote pale walipo..

Dr Slaa yes we can! Huyu ni mtanzania wa pili baada ya Nyerere kuchukia ufisadi kwa vitendo. Ni mtanzania wa pili kuchukia umaskini wa watanzania kwa vitendo. Ni Dr. Slaa aliyesimama na kutaja majina ya wala rushwa na mafisadi. Akataka wale wanaopinga wampeleke mahakamani. Hakuna aliyethubutu kujitokeza kumpeleka mahakamani.

Ni Dr. Slaa aliyesimama bungeni kuomba posho za wabunge kupungzwa kuzielekeza zaidi kwa watanzania maskini. Ni Dr Slaa aliyesimama bila woga kunyosha vidole kwa matumizi mabaya ya ofisi za umma. Ni Dr Slaa amekuwa mtanzania baada ya Nyerere kutoa hoja za nguvu zinazomlenga kumkomboa mtanzania maskini. Maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi? Ajira milioni moja ziko wapi? Hebu mwenye mbavu za kujibu swali hili ajibu bila unafiki!

Ni Dr Slaa anayeweza kudhibiti matumizi mabaya ya ofisi za umma. Ni Dr Slaa anayeweza kuwapa elimu ya bure watoto wetu pale mlimani. Achana na longolongo za CCM kuwatoza ushuru watoto. Waulizeni majukwaani wao Nyerere aliwatoza ada? Kama si kutaka watanzania waendelee kuwa mambumbumbu ni nini? kama si kutaka watanzania tuendeleee kuwa watumwa ni nini?

Ni Dr. Slaa anayeongelea treni ya umeme kwenda Kigoma, Dodoma, Tabora, na Mwanza. Waulize mpango wao ccm kama si kuwapa wahindi wanaoleta mabehewa ambayo mababu zetu walitumia wakati wa ukoloni. Sasa wahindi wanabaki kutudanganya na bajaji wakati vyuma chakavu vya reli sasa vinatumika kujenga vyoo. Hawa hawatutakii mema. Hawana tofauti na akina Carl Peters.

Ni Dr Slaa anayeongelea mfumko wa bei -nani hajajua dola leo hii ni sawa na tsh 1500. Uchumi unadidimia kwa kasi. Ahadi nyingine za uongo lukuki zinatolewa tena, wakati zile tulizoahidiwa mwaka 2005, hata moja haijatekelezwa. Watanzania walio wengi na hasa wa vijijini, wamelala usingizi. Wanafumbuliwa macho, lakini wamesinzia bado! Wanatabasamu, wanachekelea na kuridhika na vitisheti vya kijani na vikofia za njano. Wamekwishazoea shida kiasi kwamba wanadhani ni sehemu ya maisha yao. Ee mwenyezi Mungu, tunusuru na hili balaa..

Ni Dr.Slaa anaweza kuzuia wizi wa matrilion ya pesa kutoka migodi yetu ya Buzwagi, Geita, Bulyankulu, Buhemba, Nyamongo, Tulawaka, Nzega na Tanzanite. CCM wameshindwa kwa sababu ni washirka wakubwa na wameruhusu wizi huo. Ni Dr Slaa anaeweza kuwalipa wafanyakazi zaidi ya shilingi 350.000 achana na CCM ambayo imeshindwa kusimamia maliasili ambazo zingeliwapa wafanyakazi kima cha chini kinachokidhi mahitaji yao.

Ni Dr.Slaa anayeweza kusimamia mashirika ya umma kuleta tija achana na CCM wanaofyonza michango yetu kule, kwani haya mashirika yameshindwa nini kuwajengea nyumba wanachama wake? Mbona kwingine yameweza? Ni Dr.Slaa anayeweza kuongoza nchi bila woga, kwa utawala wa kweli wa sheria bila kuwaonea watu wala bila kulipiza visasi.

Ni Dr. Slaa ambaye amepanga kubadili katiba ili Rais afuate matakwa ya walio mwajiri ambao ni wananchi. Waulize CCM hata kama mtu kaiba anapewa mda arudishe pesa. Hivi inaingia akilini kweli? Utawala wa sheria uko wapi? Naomba niwape heko ITV kwa kuturejeshe kwenye hotuba za mwalimu. Katika hotuba yake moja alisema waziri mmoja kule uingereza aliandikwa kidogo tu gazetini juu ya kashfa, yule waziri alijiuzulu na waziri mkuu hata hakumjibu bali aliteua mtu mwingine.

CCM hawawezi hayo? Eti wanataka ushahidi. Nani kawambia rushwa tule wawili harafu tutoe vielelezo? Tunaiona rushwa kwa matokeo yake. Matengenezo ya barabara ya bilion 200, baada ya siku mbili imeharibika. Kwanini usimfukuze waziri na katibu wake wa wizara kwanza? CCM hawawezi! eti wanataka vielelezo!

Ni Dr Slaa anayeweza kufanya hayo. Si tumeona mnazi mmoja alivyowataja mafisadi wote! hapo akiwa ni mbunge tu! Je akiwa rais si watakimbia nchi? Jamani nawambia tumpe miaka mitano tu awakurupushe muone moto utakavyowaka.. Tutapata dawa, tutapata shule za bure, tutapata madawati. Jamani hivi kweli karne ya leo watoto wanasoma wamekaa chini? we must be serious! Hivi kweli dunia ya leo watu wanavuliwa nguo njiani kwenda Mwanza, Shinyanaga, Tabora, Kigoma, Mbeya, Lindi na Mtwara kwa sababu ya usafiri wa malori?

Nani asiye jua madaktari wetu wengi bingwa wapo botswana kwa sababu ya maisha duni Tanzania na hivi kwenda kutafuta maisha bora wakati hapa kwetu wananchi maskini wanakufa bila madawa? Nani asiyejua matatizo ya umeme, maji, makazi, maradhi, yanavyotutesa? Nani asiyejua wakulima wetu wasivyokuwa na masoko ya mazao yao? Nani asiejua asilimia 85 ya watanzania wanatumia vibatari au makoroboi kama mwanga? nani asiejua tunavyonyonywa na hawa wakoloni waliokuja kuchukua kila kitu??

Jam

Reply
Aisee
28/09/2010 6:00am

Hio clip ya JK kudondoka Jangwani bado ipo? Inaonekana serikali imeshindwa kuidhibiti. The same way, itashindwa kumdhibiti Dr. Slaa.
Ingawa amedondosha "western values" kwa Tanzania values, ni bora kuliko kuwa na nyumba ndogo na watoto kibao kiashi kwamba mtu unashindwa ku-track nani ni mama yake, hizo ndio values za viongozi wa kibongo. Hakuna kiongozi wa CCM ataeweza kusimama jukwaani na kusema hivyo kwani wote ni wachafu.......si uliona Mpiganaji Makamba alivyofungwa "bakuli" lake!
Tusubiri tuone tunaenda wapi

Reply
emman80tz@yahoo.com
29/09/2010 6:20pm

Uongozi haupimwi kwa gigezo cha ndoa. Nani asiyejua madhila yanayoweza kutokea katika ndoa? Suala la ndoa kuvunjika sio suala la kukurupuka kulitolea hukumu. Je nani mwenye uhakika kwamba chanzo cha ndoa ya Dr. Slaa kuvunjika kilitokana na yeye au Mkewe Rose? Hapa tunampima Dr. Slaa kwa ubora wa uongozi wake tangu jimboni karatu na sio habari ya ndoa yake. Lini umesikia wananchi wa karatu wakilalamika kwamba Slaa amepoteza sifa ya kuwa mbunge wao kwa sababu ameachana na mkewe? Kwani unayajua mangapi juu ya maisha ya unyumba ya Kikwete? sasa na walio na taarifa za Kikwete wakijitokeza nani wa kuwalaumu? Kama ni suala la uchafu basi Kikwete ni mchafu mara dufu kuliko rais yeyote aliyepata kutawala Tanzania. Msitutoe kwenye mada...Hapa suala ni ukombozi wa watanzania na sio nani kaolewa na nani na kwa nini. nahisi muandishi wa habari hii umekuwa mnafiki kwa kutufanya tuamini kwamba masuala binafsi ya ndoa ni zaidi ya ukombozi wa taifa letu.

Reply
sika
01/10/2010 12:44pm

Wewe mwandishi ndioo unaye tutania umesahau kuwa uongozi ni wito sioo kukurupuka tuu ndoa sii wito na ndioo inamambo mengi ambayo kwa wakati mwingine kila mtu ana maamuzi yake kulingana na linalo mkuta ndani ya ndoa hiyo wengi yana wakuta kama huyo wewe unaye mwona anandoa imara lakini kwa taharifa yako sioo ndioo imara kwa kuwa anavimada na nyumba ndogo kuliko raisi yeyote aliye wahi kuitawala tanzania hii ikiwa inaonyesha kwamba sii muwazi na wala sii muaminifu...Pili kiongozi ni uwezo wake wakuchanganua mambo na uwezo wakuwaongoza watu katika mafanikio sio katika kuwa nyonya wala kuwa danganya,kwanini tunakubali dr slaa ni chaguo letu kwakuwa ni muwazi anapiganaia maskini na uongozi ni wito wake kuna ushahidi mwingi sana toka akiwa anaongoza shule ya dongobesh mpaka hivi ubunge karatu huyo mtalii wako wewe mwandishi wa blog hii unaye mpigia debe anasifa zipi zaidi ya utalii mfano mdogo tuu angalia bagamoyo kwa kipindi chote alichokuwa mbunge waoo alifanya lipi la maana au pali badilika kwa kiasi gani kisha fananisha na karatu utakuwa umepata jibu la nani ni mtendaji mzuri na nani ni mzugaji...chadema oyeee

Reply

Comments are closed.