Shukrani kwa Mubelwa Bandio "mzee wa changamoto" kwa maelezo na video hii.
----

Hotuba ya Bw. Hodari Abdul-Ali. Mmarekani mwenye asili ya Afrika aliyezungumzia ziara yake ya Tanzania akiwa mwanafunzi, uelewa wake kuhusu Tanzania, Afrika na pia umuhimu na faida ya ushirikiano kati ya waTanzania na waMarekani wenye asili ya Afrika.

Bw. Hodari ni Mkurugenzi wa Give Peace a Chance Coalition (G-PAC), mtangazaji wa WPFW Pacifica Radio na mmiliki wa duka la vitabu liitwalo Dar Es Salaam lililopo Maryland nchini Marekani.

Hotuba hii aliitoa siku ya kuenzi kazi na Maisha ya Hayati Mwl Julius K. Nyerere iliyoadhimishwa Oktoba 16, 2010 chuo kikuu cha Howard, Washington DC.
 


Comments


Comments are closed.