Matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC yanasikika moja kwa moja mtandaoni kutoka Dar Es Salaam. NI matangazo maalum ya uchaguzi mkuu wa Raisi, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani. Yatakuwa yanasikika kuanzia asubuhi saa moja hadi usiku saa tatu majira ya Afrika Mashariki.
Unaweza kufuatilia matangazo haya katika radio washirika nchini Tanzania ambazo ni Radio One (ukiwa Unguja tega 94.1 na ukiwa Pemba tega 93.5), Radio Free Africa na Kiss FM.