|
|
Video ya Kwanza ya sehemu ya Utangulizi, inapatikana Youtube, haijawekwa hapa kwa kuwa sauti haisikiki hivyo nimeweka sahemu ya Pili - Mawaziri na Manaibu wa Wizara wakitangazwa ambayo sauti inasikika. credit : Mwanakijiji CommentsMsuya 24/11/2010 1:33pm
Ninamsifu Rais Kwa baraza jipya la mawaziri hususani wizara ya Ujenzi pamoja na wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi mambo mambo 24/11/2010 3:10pm
kwa kweli Rais amejitahidi kuteua baraza la mawariri, lakini issue ya kumuacha aliyekuwa Waziri wa afya na ustawi wa jamii naona amepoteza hazina ya mtu mchapakazi. au waungwana mwaonaje hapo? 24/11/2010 3:18pm
Napenda kutoa pongez zangu kubwa kwa Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa na ngumu aliyokamilisha ya kulitengeneza baraza la mawaziri.Sina shaka na uteuzi huo,naamini kabisa wale wote waliopewa nafasi hizo watazifanyia kazi kwa maendeeo ya Tanzania wote.Hongear sana ila nikuombe uangalie pia nafasi ya Mratibu wa huduma ya viungo bandia katika ngazi ya wizara,nadhani tunahitaji kuwa na mwakilshi ,kwani huduma hiyo hapa nchini imekuwa ikitolewa tu bila ya unagalizi.Niwatakie wote kazi njema na umoja kamili KADA 24/11/2010 4:06pm
Hongera sana Rais wetu Kikwete umefanya kazi nzuri sana. Wapinzani sasa tufanye kazi karibuni kushirikiana nasi MAKUNGU 24/11/2010 4:42pm
Hongera JK kwa kumchagua Dk. Mwakyembe ili naye apambane na changamoto Mwl. Ezekiah T. Oluoch 24/11/2010 4:49pm
Nawapongeza wote waliochaguliwa na Mheshimiwa Rais amefanya kile alichoweza isipokuwa Mheshimiwa Shukuru Kawambwa hatakabiliana na changamoto za elimu nchini, Mheshimiwa Hawa Ghasia ataendelea kumwangusha Mheshimiwa Rais kama alivyofanya kwa miaka mitano iliyopita. Matumaini yangu makubwa yako kwa Kaptain Mkuchika kwa kuwa atasaidiwa na Kassim Majaliwa kuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI anayeshughulikia Elimu. Kama Majaliwa hatawageuka walimu waliomlea toka amekuwa kiongozi wa Chama cha Walimu Tanzania hadi alipokuwa Mkuu wa Mkoa, walimu wa nchi hii watasonga mbele. Kama Mheshimiwa Mkuchika atakuwa msikivu kwa wafanyakazi bila ya kuleta ubabe, atakuwa Waziri atakayekuwa na mafanikio makubwa. Ery 24/11/2010 5:52pm
Kwaweli safari hii Rais amesikia kilio cha wananchi Baraza zuri sana;waheshimiwa Magifuli,Nahodha,Sitta Huseni mwinyi pamoja wengine wote kwa ujumla wake bila shaka wamewekwa mahali pake. Naona sasa kazi itafanyika namatumaini yanaanza kurudi. Big sana JK); i 24/11/2010 6:02pm
kwa watu kama magufuli,mwakyembe, samweli sita,na wengine wachache wanafaa lakini wengine wote fiki kama vile ngeleja hakuka jipya,hawezi kazi hakuna alichokifanya zaidi ya ubinafsishaji ambao unanufaisha makaburu ambao wanabeba hadi mchanga.hata Rick,cuf,zaker osward wanalijua hilo. sam 24/11/2010 6:07pm
soma hapo juu,i know utakubaliana na mimi.na kama ccm hamtaki kuchakachua sana so that next election msiloose kabisa attend to your promis mr president na watu wako.ila kama utafanya changes samweli sita mpe nafasi ya waziri wa sheria na katiba na ngeleja umpoteze kwa rasilimali endelevu kama vule madini. Yusufu R.Masai 24/11/2010 6:14pm
Hakika Baraza jipya la mawaziri ni la kimapinduzi sana.Ukweli ni kwamba kuwa na vijana wengikatika uwaziri siyo mwarobaini kwa maswahibu yetu vijana. ROBERT K.GEORGE 24/11/2010 7:42pm
NAMPONGEZA MH.RAIS KWA KUMALIZA KAZI YA UTEUZI WA MAWAZIRI ILA BAADHI WALIORUDI HAWANA JIPYA LA KUWAPA WATANZANIA KAMA MH. NGELEJA HANA JIPYA ZAIDI YA KUJINUFAISHA KWA UBINAFSISHAJI WA MALI ZA WATANZANIA KWA MAKABURU AMBAO HAWAWALETEI WATANZANIA MAENDELEO YOYOTE BALI KUWANYONYA KWENYE UDONGO WAO. Dizo 24/11/2010 8:16pm
Madini=o% kimera 24/11/2010 10:36pm
Nakupongeza sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg Jakaya M. Kikwete kwa kuunda Baraza nzuri la Mawaziri. Kwa baraza hili tunategemea maendeleo mazuri hasa barabara. Ushindo wa kishindo mwaka 2015. "kazi nzuri". james godfrey 24/11/2010 11:22pm
nasifu muheshimiwa rais kwa kutangaza baraza la mawaziri makini waliojaa na hekima katika jamii. mungu amzidishie maisha mema na majukumu yake ya kuliongoza taifa letu masangu LAMECK 24/11/2010 11:28pm
hilo ni baraza zuri sana! hongera sana rafikiyangu ELIAS 24/11/2010 11:31pm
hongera sitta na magufuri najua mtashirikiana na rais kuleta maendeleo kwa watanzania! sina shaka na nyinyi eeeeeeti mc 25/11/2010 6:17am
Na mshukuru sana muheshimiwa JK. ktk kumuweka magufuli kwenye hiyo nafasi na nina uhakika kazi itafanyika katika nafasi yake bila shaka wapenda wote waliko katika nafasi zao wasimamie kazi pasipo kuchekana katika kujenga taifa letu ili kusonga mbele daima. wote tushughulike katika kujenga mazingira safi ya taifa letu pasipo kuangalia upinzani wa vyama bali tukumbuke sisi sote ni watanzania na ni ndugu. USHIRIKIANO DAIMA, KAZI BORA, FIKIRIENI MAENDELEO YA NCHI, HAKI SAWA, UMASKINI TUUFUKUZE. mukobo 25/11/2010 9:27pm
Dk Magufuli,anza kwa kasi ya ajabu kwanza kabisa foleni za barabarani dar kwa kujenga barabara zote za pembezoni ili zitumike hasa hii ya tegeta kupitia mpiji magoe hadi kibamba/mbezi luisi, BETH KAANAEL 26/11/2010 8:46am
Hongera sna raisi Jakaya Mrisho kwa kuwaweka mawaziri makini kama Magufuli na Sitta kwenye wizara muhimu. Be blessed. Comments are closed. |