Kitendo cha Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Shamsi Vuai Nahodha kuzomewa akiwa Mbeya kimetolewa ufafanuzi na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa kimetokana na kero mbalimbali za kiusalama ambazo zinaigusa jamii ya wakazi wa Tunduma ambazo zimeshindwa kutatuliwa. Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa CHADEMA wa mji mdogo wa Tunduma Bw. Herode Jivava alisema kuwa, CCM inapaswa kujilaumu kumtuma kiongozi mtendaji mwenye dhamana ya usalama wa raia kwenye mambo ya kisiasa ilhali yapo mambo ya msingi ambayo Waziri alipaswa kuyapata kutoka kwa wananchi wa mji huo wa mpakani. ‘Wapo viongozi wa chama ambao wangeweza kutembelea wana-CCM wenzao…huyu ni Waziri ambaye tunaamini kuwa anasimamia katiba ya Jamhuri ya Muungano katika wajibu wake bila kupendelea chama cha siasa… ni haki yake kuzomewa kwa kuwa amekuja nawanasiasa huku akitumia rasilimali za serikali’, alisema Bw. Jivava. Alifafanua kuwa CCM ni chama kinachojitosheleza katika uongozi angeweza kuja Katibu Mkuu au Katibu Itikadi na Uenezi ambao wangeweza kukutana na wanachama wenzao na kujadili mipango yao ya chama. Kitendo cha kumtuma Waziri wa mambo ya ndani kufanya mikutano ya kisiasa badala ya kusikiliza kero za wananchi ndiyo sababu yakuzomewa kwake. Alisema CHADEMA imejenga imani kuwa kuanzia sasa askari polisi wote wataanza kutumika kunyanyasa vyama vya upinzani kutokana na kiongozi wao kukubali kutumika kisiasa kwa maslahi ya chama kimoja. ‘Tunayo matatizo mengi hapa mpakani, pamekuwa ndiyo njia kuu ya kusafirisha bidhaa haramu kama dawa za kulevya, biashara ya kuuza binadamu, wakimbizi ambao wanatumia njia hii kuvuka nje ya nchi na mengi ambayo tungemweleza, anaacha mambo haya ya msingi anakuja kwa ajili ya chama akisindikizwa na magari ya serikali?… ni halali yake kabisa kuzomewa,’ alisisitiza Bw. Jivava. Jivava alisema, alichokifanya Waziri Nahodha kimedhihirisha namna ambavyo viongozi wakuu wanavyoamua kuikanyaga demokrasia kwa kukipendelea chama tawala, na kuwa amejipandia mwenyewe mbegu ya chuki miongoni mwa wananchi wa Tunduma jambo ambalo hapaswi kuwalaumu waliozomea bali waliomtuma kufanya ziara ya kisias abadala ya ziara ya utendaji. Katika hatua, nyingine Bw. Jivava alikanusha taarifa iliyotolewa na CCM kuwa kuna wanachama 96 waliojiunga na CCM kutokea CHADEMA na kusema kuwa wanachojua ni mwanachama mmoj atu ambaye alitimuliwa CHADEMA kwa kukiuka taratibu za kiuongozi ndio aliyerejea CCM ambaye ni aliyewahi kukaimu nafasi ya Katibu Kata wakati wa uchaguzi mkuu Bw. Julius Ndindilile. Alisema tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu CHADEMA imepokea jumla ya wanachama wapya 132 ambapo wawili kati yao wametokea chama cha TLP na 130 wametokea CCM. via blogu ya Mkwinda (ikiwa uliikosa taarifa ya Waziri kuzomewa, bofya hapa kuisoma) Add Comment Poem for London 2012 by Saleh Jaber 05/02/2012
It’s a beautiful world, it’s a beautiful day It’s beautiful people, on this special day What a joy this day brings, when you will see the queens and the kings Fifty three days before the start of the games Floating through the wonders of the river Thames Come to see today’s London Come to see the isles of wonder No matter where you are coming from London's diversity will make you feel at home It's more than London's diversity and its vibrant colours It's more than the names and the bearers of the Olympics flame Under the Olympics rainbow We are all the same As the world come together in London twenty twelve Be gold or silver, no matter what you have Be there to triumph in this adventurous race As the world will be watching, put a smile on your face If you care about what’s being said If you care about what’s being told Please share this peaceful message With the rest of the world. The Nairobi City Council is now planning to give commercial workers a license to operate freely in the Central Business District. The Mayor George Aladwa says he has received petitions from hundreds of twilight girls who claim they are harassed by city askaris while on duty. As James Smart of NTV reports, City Hall has chosen a rather significant day to make the big announcement. (THE ANTI-MONEY LAUNDERING (AMENDMENT) ACT, 2012 IKIWASILISHWA NA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KATIKA WIZARA YA FEDHA, MHE. KABWE Z. ZITTO (MB). Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni; Mhe. Kabwe Zuberi Zitto (Mb), na kwa mujibu wa kanuni za Bunge kanuni ya 86(6), toleo la mwaka 2007, naomba kuwasilisha maoni ya kambi ya Upinzani kuhusu Muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya udhibiti wa fedha haramu wa mwaka 2012.
Mheshimiwa Spika, fedha haramu ni biashara ambayo hufanyika bila kuwepo kwa mteja wa kuinunua biashara hii kwani mteja na mpokea mapato huwa ni mtu mmoja, kwa mujibu wa wataalamu wa kushughulikia uhalifu huu wanasema kuwa, huwa inapitia katika hatua tano muhimu kabla ya kukamilika katika mzunguko wake, hatua hizo ni; 1. Tendo la kihalifu , hii ni kujipatia fedha kwa njia ambazo sio halali kama vile kufanya biashara haramu kama za madawa ya kulevya,ufisadi, rushwa n.k 2. Fedha haramu kuingizwa kwenye mzunguko kupitia taasisi mbalimbali za fedha, hii ni mbinu ambayo hutumika katika kuhalalisha fedha hizo , kwa mfano mtu kufungua kampuni ambayo inajihusisha na biasahara mbalimbali tofauti hivyo kuweza kufungua akaunti benki kulingana na majina ya biashara husika na kwenye mabenki mbalimbali na hivyo hutumia akaunti hizo kuingiza fedha haramu kwa lengo la kuzisafisha. 3. Fedha haramu husafishwa ili kuficha hatua ya kupatikana kwa fedha hizo kihalifu,hii ni mbinu ambayo hutumiwa na wahalifu katika kuhakikisha kuwa hawawezi kufahamika na vyanzo vya fedha husika , kwa mfano mtu huamua kununua vitu mbalimbali kama magari, kusafirisha fedha nje kwa kutumia mifumo ya kibenki , kuanza kujipatia mikopo, tenda n.k 4. Fedha halali kuzaliwa, hapa ni hatua ya mtuhumiwa kuanza kupokea faida kutokana na vitega uchumi mbalimbali alivyojiwekea kutokana na fedha haramu na hivyo kuwa na uwezo wa kuonyesha vyanzo halali vya fedha zake . 5. Fedha hutumika kihalali kwa mujibu wa sheria, mzunguko huishia kwenye hatua ya matumizi kuwa halali na hakuna uwezo wa kuendelea kumfuatilia tena . Mheshimiwa Spika , kwa mujibu wa taarifa ya shirika la Maendeleo la Umoja wa mataifa (UNDP) ya mwaka 2011 mwezi mei , ilinaonyesha kuwa mataifa yanayooendelea yameathiriwa zaidi kiuchumi na biashara hii ya fedha haramu kwani iliongezeka kutoka dola za kimarekani 9.7 bilioni mwaka 1990 na kufikia kiashi cha dola 26.3 bilioni mwaka 2008 kwenye nchi zinazoendelea (LDCs), na madhara yake ni makubwa kwani ilichangia kushusha kiwango cha thamani ya fedha za nchi hizo kwa kiwango cha asilimia 6.2 kwa mwaka katika kipindi husika , hii inaonyesha kuwa Tanzania hatuko kisiwani kwani nasi tuliathiriwa kwa kiasi hicho hicho. Mheshimiwa Spika, taifa letu limekuwa na sheria nyingi ambazo ziliwahi kutungwa kwa ajili ya kukabiliana/ kuondoa tatizo la fedha haramu,rushwa na uhalifu uliopangwa hapa nchini mwetu tangu tupate uhuru na hii inathibitishwa na uwepo wa sheria zaidi ya 15 kuwahi kutungwa tangu uhuru kama ifuatavyo: Nashukuru kwamba walau tofauti na tarehe 02/02/2012 ambapo Naibu Spika Ndugai alipotosha muongozo nilioomba akadai kuwa ni hoja isiyoungwa mkono na kuipuuza; tarehe 03/02/2012 amezingatia muongozo nilioomba na kutoa mwelekeo ambao umeongeza msukumo katika bunge kufanya kazi yake ya kuisimamia serikali. Hata hivyo, bado muongozo uliotolewa haujitoshelezi kwa kuwa jukumu hilo kwa kamati ya huduma za bunge halikuelezwa bayana limeanza lini na litamalizika lini. Vyanzo kadhaa vimeeleza kwamba taarifa ya kamati husika itawasilishwa kwenye mkutano ujao wa bunge (Mkutano wa Saba), suala ambalo halipaswi kukubaliwa. Kutokana na uzito na udharura wa mgogoro huu ni muhimu taarifa ya awali ya kamati iliyopewa jukumu ikawasilishwa katika mkutano huu wa sita unaoendelea ili hatua za haraka zikachukuliwa katika kushughulikia madai ya madaktari na kupata taarifa ya kweli kuhusu athari za mgogoro na mgomo ulioendelea ikiwemo vifo vilivyotokea. Aidha, Kamati husika ingepewa hadidu rejea za wazi ikiwemo ya kufanya kazi ya usulushi na upatanishi katika mgogoro ambao umetokea baina ya madaktari na serikali na pia kuwezesha bunge kusimamia ipasavyo na kwa haraka serikali katika kushughulikia madai ya wafanyakazi. Kwa upande mwingine, kwa kuwa imebainika wazi kwamba kuna uzembe na udhaifu miongozi mwa watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakiongozwa na Waziri wa Wizara husika ambaye amefikia hatua hata ya kutoa taarifa ya kulidanganya bunge; ni vizuri baada ya Kamati husika kusikiliza pande zote mbili Waziri na watendaji husika walazimishwe kujiuzulu ili hatua za kushughulikia madai ya madaktari na kuboresha huduma za afya katika hospitali za umma zitekelezwe na wateule wengine wenye uwezo na dhamira ya kweli ya kushughulikia matatizo yaliyojitokeza. Itakumbukwa kwamba Juzi (03/02/2012) kabla ya kusomwa kwa kauli ya serikali kuhusu mgomo wa madaktari niliomba muongozo wa Spika kwa mujibu wa kanuni ya 5 ambayo inamtaka Spika kuendesha bunge kwa kuzingatia kanuni na pale ambapo kanuni hazijaelekeza kutumia sheria, katiba, maamuzi yaliyopita ya bunge na mila na desturi za kibunge. Nilitumia kanuni hiyo kutaka Naibu Spika Job Ndugai atoe muongozo ili kuwezesha badala ya kufuata masharti ya kanuni ya 49 pekee ambayo inasema kauli ya serikali ni ya jambo linaloihusu serikali na lisilozua mjadala afuate katiba ya nchi na maamuzi mengine ya bunge ili maudhui ya kauli hiyo ya serikali yaweze kujadiliwa na bunge. Nilinukuu ibara ya 63 (2) ya katiba ambayo inasema mamlaka ya bunge ni kuisimamia serikali na kwamba katika suala la mgomo wa madaktari ni muhimu bunge likachukua wajibu huo kwa sababu kauli itakayotolewa inahusu serikali wakati mgomo wenyewe unaathari kwa wananachi hivyo wabunge kama wawakilishi wa wananchi wanapaswa kupewa fursa ya kuisimamia serikali katika suala hilo linalohitaji hatua za dharura. Aidha, nilieleza kwamba kauli ya serikali inaihusu serikali ambayo katika mgogoro na madaktari na yenyewe ni mtuhumiwa hususani Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii ambayo Waziri na watendaji wake wameonyesha udhaifu katika kushughulikia mgogoro na madai ya madaktari hivyo bunge linapaswa kujadili ili kuweza kuwawajibisha. Baada ya kauli ya Serikali Naibu Spika Job Ndugai alitoa muongozo ambao alieleza kwamba ni kweli kauli za mawaziri hazijadili lakini akaelekeza kwamba kauli hiyo ipelekwe kwenye Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii ili ichukue hatua ‘haraka iwezekanavyo’ na hatimaye kuleta taarifa bungeni. Katika maelezo yake alieleza kwamba kuna haja ya kanuni za bunge kubadilishwa lakini pia alieleza kwamba kuna watendaji wa serikali wamelalamikiwa kuhusu suala la mgomo wa madaktari. Tayari imeeelezwa kwenye vyombo vya habari kwamba Kamati husika ya Bunge itakutana na madaktari kesho (06/02/2012) na kwamba madaktari kwa upande wao nao wameonyesha nia ya kukutana na kamati hiyo. Kama tulivyoanza awali, tutaendelea kufuatilia suala hili hatua kwa hatua mpaka kieleweke. John Mnyika (Mb) Bungeni-Dodoma (05/02/2012) Mnyika.blogspot.com Mchezo wa mpira wa miguu kati ya wanamuziki na waigizaji umefanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo ili kuchangia walioathirika na mafuriko yaliotokea hivi karibuni jijini humo na kusababisha vifo na uharibifu wa mali. Mgeni wa heshima katika pambano hilo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik. Habari na picha blogu ya Father Kidevu Kampeni mpya inaanzishwa nchini Saudi Arabia kuwahimiza wanawake wachukue hatua za kisheria kupinga amri inayowakataza kuendesha magari. Mwanamke aliyeongoza juhudi za kutaka amri hiyo ibadilishwe, Manal Al Sharif, ameiambia BBC, kwamba atatokeza kwenye kipindi maarufu cha televisheni hii leo, kutangaza hayo. Anasema ataeleza vipi wanawake wanaweza kufuata mfano wake, kuchukua hatua kisheria, baada ya ombi lake la leseni ya kuendesha gari kukataliwa. Katika hatua isiyopata kuonekana Saudi Arabia, Bibi Al Sharif ameishtaki serikali - mashtaka ambayo sasa yanazingatiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. - BBC Swahili A security guard was found dead and another one is in police custody following a midnight attack in Kisauni, Mombasa. The deceased is said to have been murdered by his colleague after an argument. Here is an NTV video on the sad news. | Vitabu vya WatanzaniaBofya picha ya kitabu unachokitaka ili ujinunulie nakala
Yaliyomo/CategoriesAll Hifadhi/ArchivesFebruary 2012 |





RSS Feed