Habari ya Kazi, Mimi ni mdau mkuu wa blog wako, kuna shida ambayo huwa inanitatiza sijui kama ni mi peke yangu au hata baadhi wateja yamewakuta haya. Mwaka jana Benki ya Exim imetambulisha huduma mpya au akaunti mpya inaitwa FAIDA akaunti kutokana na matangazo yao wanaonyesha kwamba ukipata hiyo kadi kuna faida nyingi ikiwemo ku nunua bidhaa kwenye mtandao (on-line purchasing), haya matangazo yamenishawishi kufungua akauti ya FAIDA, sasa mpaka leo hii asubuhi hii najaribu kuweka details ya hiyo Faida Card ambayo ni Debit Master Card naambiwa kuwa ajili kwa kununua bidhaa "You have entered an invalid number or partial credit card or debit card number. Please check your entry and try again", Tafadhali naomba wahusika wa Exim bank watupe statement yao kuhusu hilo suala, kwa sababu wametufanya tuhamishe fedha kutoka kwenye benki nyingine na kuweka kwenye hiyo account tukitaraji kwamba tuta purchase on-line kumbe hamna kitu, sasa huu sio uongo wa ki macho macho na kupoteza uaminifu wenu kwenye jamii ya Watanzania? Nawasilisha Meza kuu... Wake Mteja wa Faida na Mdau wa Blog ![]() mmoja wa walioathirika baada ya kutumia maji yaliyotiririka toka migodi Picha zinazoonekana hapa ni mali ya blogu ya Kijijini Kwetu ya Chacha o'Wambura (Ng'wanambiti) na zimewekwa hapa ili kusambaza habari hii kwa watu kwa matumaini kuwa yupo mwenye roho ya ubinadamu walao mmoja atakayesikia na mwenye uwezo wa kufanya jambo la haki au kufikisha suala hili kwa anayeweza kulishughulikia. Masuala kama haya yatatufababisha siku moja tudaiane haki na amani kwa ncha ya upanga, na hiyo si kauli yangu binafsi bali nukuu ya wenye hekima waliotutangulia, mwenye akili na afahamu. Ng'wanambiti anasema: Cha kushangaza ni kuwa kuchukuwa hatua kwa swala hili kumekuwa kukichukua muda mrefu sana. Tunachosikia ni majibu ambayo ni ya kiutawala ambayo Barrick, DC wa Tarime, RC Mara, NEMC, Wizara ya Mazingira, Wizara ya Afya na Wizara ya Madini wanayatoa ni sawa kuwa 'wenyeji wameiba lining za mabwawa ya kuhifadhia maji machafu'. Je na hawa ambao wako katika vijiji vilivyo mbali na mgodi ambao ndo wamedhurika kwa kiasi kikubwa ni wezi? Ndo kusema kuwa wataalamu wetu wa afya kuanzia Mkemia Mkuu wamewaasi wananchi walowasomesha kwa jasho la kodi zao na kuungana na wawekezaji kwa kisingizio cha 'attracting foreign direct investment? FDI kwa gharama za wananchi wetu? Je kuna mkono wa mtu (kisiasa na kampuni)ama ni kutojali kwa viongozi wetu? ![]() Hivi kwanini sisi wabongo tunapenda sana kufanyiana roho mbaya, ntimanyongo, ubangaizaji na short cuts? Wengi wetu hatupo honest... ukimpelekea fundi kitu atakulipulia ili mradi urudi tena... mwingine anaweza kukubadilishia kifaa akakupachikia kibovu akaondoa chako kizima... Ukienda kununua kitu unauziwa kwa kuangaliwa sura kwanza mimi nitaambiwa buku mbili, Supika kwa sababu kakaakaa kama Mzulu atapigwa kilo nzima... kitu kimoja bei tofauti kulingana na mtu... Ukijenga Uswahilini na nyumba yako ndo pekee ikawa na bomba la maji basi uwe mvumilivu kwa majirani... wengine wanaweza kukuamsha saa sita eti anataka kuchota maji... Ukipanga uswahili ukawa na ka-home thieta kako weka grill manake vibaka lazima waje kukutembelea... Una saa nzuri mkononi huna amani ukikatiza Magomeni mateja wanaweza kukufanyia kitu mbaya... Kwa walio ughaibuni unatuma pesa nyumbani ujengewe sahau hakuna cha tofali wala vumbi la kokoto litakalonunuliwa... Ukiharibikiwa na gari unaomba msaada wa kusukumwa kidogo lazima uwe na senti senti za kutoa... Ukipotea njia ili uelekezwe unaulizwa una hela? Nina barua ndogo ninahitaji bosi anisainie tu, utazungushwa wee na Sekretari wake mpaka utakata tamaa, kisa anajua ikisainiwa utapata mshiko, ukitaka umuone kwa chai kidogo... Unadai pesa za malimbikizo bosi anakuzungusha tu makusudi ili usiipate pesa yako au ukate tamaa kufuatilia wakati pesa haitoki mfukoni mwake. Hizi roho mbaya sijui zinatoka wapi? Kwa nini tupo hivi sisi? Mpaka tutwangane bakora? Yaani watu hawawezi kuwa honest japo kidogo? Yaani tabu tabu tabu... ah bubu husema... Monsignor, China Shaffi Ramadhan Kondo ameishi gerezani kwa miaka kumi. Hapa anamwelezea mwandishi wa BBC, Josephat Mwanzi, hali halisi ya magereza ya Tanzania. Bofya kifute cha play upate kusikiliza mahojiano hayo mafupi. Video ya awali na hii inayofuatia zote waweza kuzitizama katika ukurasa wa video ama bofya picha hapo chini kupelekwa zilipo video hizo. Video ya pili imerekodiwa na kuwekwa mtandaoni kwa hisani ya Kennedy Kimaro. TheUwazi wamerekodi na kuweka kwenye mtandao video inayoonesha taswira ya ilivyokuwa eneo lilikotokea mauaji ya wanafamilia 17, mauaji ya kinyama yaliyofanyika katikati ya mwezi Februari 2010. Tafadhali bofya picha hapo au nenda kwenye ukurasa wa video kuitizama video yenyewe. Tafadhali soma onyo kabla ya yote. Ombi kwa NECTA toka kwa mzazi 02/08/2010
Rai ya George kwa NECTA kuwasihi waboreshe tovuti ya matokeo ya mtihani na kuweka aina mbalimbali zaidi za chaguzi ya jinsi ya kuperuzi kwa urahisi wa kupata matokeo. Maoni alivyotutumia yanasomeka: Ifike muda watu wafikiri kuhusu wateja. Sisi wazazi na wengine ni wateja wa necta inapofika wakati wa matokeo. Kwa nini wasipange shule kwa herufi au kimkoa ikawa rahisi kupata unachotaka? Imenichukua muda mwingi kupata shule niliyotaka matokeo yake. Badilikeni zingatieni wateja wenu kwanza. Posti iliyotangulia nimeandika namna ya kupata matokeo ya kidato cha nne. BOFYA HAPA kusoma. Nimeshindwa kuvumilia, acheni tu leo niseme, nimeshikwa na hasira ni vile nimekosa viwembe na chupa za kutosha za kujimaliza. Nitatafuta sumu ya panya baadaye nikishamaliza kumwaga hasira zangu leo. Nasema wizara ya Elimu na vitengo husika hasa cha IT na mambo ya tovuti mnatia aibu, mnakera na kuchefua. Nasema hivi kutokana na usumbufu ambao wahitimu wa kidato cha nne na sita wamekuwa wakiupata kila msimu wa matokeo unapowadia. Leo najivisha cheo cha kuwasemea wadogo zangu hawa. Iko hivi: Kila matokeo yanapotangazwa kuwa yametoka rasmi, vijana wamekuwa wakijituma kwenda Wizarani; punde wanapofika huko hutakiwa kupunguza msongamano na kuelekezwa kwenda mashuleni ambako nakala za vitabu vyenye matokeo hayo vimewekwa. Huko kwenye mashule nako ni usumbufu ule ule. Mara mwalimu husika na vilipo vitabu hivyo haonekani. Mara ofisi yenye vitabu haijafunguliwa. Mara mwalimu ana shughuli maalumu subirini. Alimradi tu watapewa vijisababu mia kidogo wakitakiwa kusubiri pasina kujua wasubiri hadi muda gani. Hivi lengo lenu kuwafanyia hivyo ni kuwakatisha tamaa au mnadhani kwa kufanya hivyo mnakwepa usumbufu? Kwa taarifa yenu tamaa hawakati wala usumbufu hauondoki msipowaonesha matokeo; zaidi sana mnawatia hasira tu za bure, bure kabisa! Mtu mwenye akili timamu lazima ajifunze kuona mbele kuwa mtu uwapo katika hali ya uhitaji iliyo na simile ndogo (desperation) ni rahisi kupandwa jazba (to be provoked) kutokana na kunyimwa iliyo haki yako. Hili likitokea bila shaka tutasikia katika vyombo vya habari wahusika wakisema wanafunzi si wastaarabu na wavumilivu. Nashindwa kuelewa wahusika hao wanashindwa vipi kukumbuka saikolojia ya vijana? Lau hawana elimu ya saikolojia hiyo, japo wakumbuke wao wakiwa katika umri huo walikuwa wakijisikia vipi wanapohangaishwa na majibu yao? ule mchecheto walikuwa wanauzima vipi? wao wanadani vijana wa sasa hawana mchecheto? Historia ya tatizo: Kwa mara ya kwanza kusoma vilio hivi ni wakati wahitimu wakitafuta matokeo ya mtihani wa mwaka 2007. Tukajipa moyo kuwa kwa bahati mbaya huenda maji yamezidi unga, si neno, tusubiri mwakani. Mwaka ulofuatia kelele ilikuwa ni ile ile na pengine kuzidi. Tena mwaka huu 2009! Jamani eeh, imezidi hii. Miaka mitatu (2007, 2008, 209) mfululizo tatizo ni lile lile, ina maana kuwa hamsikii au hamtilii maanani kadhia hii mnayosababishia vijana wetu? Yaani ni kweli kuwa Wizara imeshindwa kutenga fungu la kununua bandwidth kubwa kwa wizara hii nyeti ya Elimu ili kukidhi mahitaji ya muda huu mfupi? Isisingiziwe gharama au hasara hapa jama. Sioni hasara yoyote kwani bandwidth itakayotumika ni maalumu kwa kipindi kifupi tu lakini muhimu sana hivyo inaweza kulipiwa kwa kipindi fulani tu. Naomba mtu asiniongopee kuwa haliwezekani kwani ninafahamu, tena si kufahamu tu, ninajua kuwa inawezekana. Tatizo lililopo ni la wahusika kutokutaka kuuliza na kupata maoni ya kipi cha kufanya. Wahenga walisema kuuliza si ujinga, na asiyeuliza hanalo ajifunzalo. Enyi wahusika wa kigengo hiki, kila leo mambo hubadilika; ulilojifunza jana leo laweza kuwa halifai, elimu ya usiku yaweza kuwa kiporo cha asubuhi, tena katika ulimwengu huu wa teknolojia ambapo kila leo zinazaliwa scripts na codes mpya. Tafadhali muache 'kujiona' na mkubali kupatiwa ushauri na kuufanyia kazi ule unaofaa. Suluhisho ama pendekezo langu? Mi nadhani suluhisho mojawapo ni kwenu ninyi wahusika wa IT kuwa elekezeni maswali yenu kwenye kundi la eThinkTankTz (eTTTz) kwani ninayo imani kubwa kuwa mtapatiwa ufumbuzi kutoka kwa wataalamu wengi wanachama wa kundi hili. Nafahamu mnaifahamu eTTz, ila ni 'ego' yenu imekuwa kubwa kuliko masilahi yetu tulio wengi. Linki yake ni www.ethinktanktz.org. Humo wapo watu ambao wamejitolea kabisa ku-host tovuti hii bila malipo yoyote ili tu kuondoa kadhia hii. Ninajua Wizara itajitetea kuwa ni chombo cha Serikali hivyo mtu binafsi au shirika lisio la kiserikali haliwezi kupewa ruhusa ya kufanya hivyo; ikiwa huo ndiyo utetezi na taratibu za kiserikali, basi tupatieni tovuti inayofanya kazi hasa katika kipindi inachohitajika kuliko wakati mwingine wowote. Nimekasirika? Ndiyo! Tena sana tu! Ni aibu na inakera! Ninyi watu kweli mfikage mahali muondoe 'ego' zenu zilizojaa maringo mbuzi na mvae utu na maslahi ya wote mbele. Yaani mi nachukiaga! Sasa nimesema sana, naweza kwenda kutafuta ile sumu ya panya ninywe.... Loh! Thubutu yake. Hanywi mtu sumu wala nini hapa. Ttutapambana na kero hizi hadi liamba walahi. Ala! Indiketa hatari kwenye mahusiano 01/22/2010
Inaaminika kuwa, unapokuwa katika mahusiano ya urafiki wa karibu au mapenzi kisha kuanza kuona majibu ya aina hii, basi ng'amua kuna kiti si sawa hapo. Ila, wapo ambao majibu yao yapo hivi tangu siku ya kwanza kabisa ya mahusiano. Wanaozungumziwa hapa ni wale wanaoanza kwa mahaba moto moto kisha inafuata: Sms: “Sweet, nimekukumbuka sana leo, natamani tungekuwa sote mida hii. Upo wapi mpenzi?” Jibu: “Nipo” Sms: “Yaani nimekutafuta kweli mpenzi, mbona ulikuwa hupatikani? Mwenzio sijalala nakufikiria wewe my love. Umenimiss?” Jibu: “Simu iliisha charge” Sms: “Baby leo nakula chakula kitamu kweli. Sijui wewe unakula nini. Natamani tungekuwa wote. Karibu mpenzi” Jibu: “Poa” Sms: “Honey, yaani ile perfume uliniletea inanukia vizuri ajabu. Yaani hapa nipo nasikia harufu yake na kukuwaza wewe, tena nakumbuka leo umetoka fresh na ile tshirt nilikununulia. Ukisoma hii sms wewe unapata hisia gani?” Jibu: “Tshirt inanibana” |