wavuti
wavuti logo Facebook icon Facebook icon Twitter icon Subscribe RSS
 
Ndiyo, ujumbe umefika, lakini, lugha imenyewa! Haifai kuwa hivi.
Picture
Usahihi ni: Hapauzwi. Utatapeliwa. (picha imepigwa eneo moja huko Tegeta, Dar Es Salaam)
Lipo tatizo kubwa kwa baadhi ya watu wa makabila fulani nchini Tanzania kuhusiana na matumizi ya herufi, 'R' na 'L' au 'H' na 'U' katika matamshi na hata kwenye maandishi. Pia, wapo wale ambao hushindwa kutofautisha kati ya herufi 'S' na 'Z' au 'P' na 'B' ama 'V' na 'F' na 'DH' na 'Z' na kadhalika.

Ingawaje kwa maneno mengine huwa si rahisi kupoteza maana kusudiwa, makosa hayo bado huweza kuleta maana tofauti kabisa na iliyokusudiwa, hasa kwa mgeni au mwanafunzi wa lugha ya Kiswahili.

Kwa mfano, neno 'ukiri' ni tofauti na neno 'ukili' au 'karamu' na 'kalamu'. Vile vile 'kazi' ni tofauti na 'kasi' kama ilivyo 'vuma' ikawa tofauti na 'fuma'. Kadhalika, 'barua' ni tofauti na 'parua' ama 'dhana' na 'zana'.

Matumizi yasiyo sahihi ya maneno hayo humlazimisha msomaji kujua maudhui ya habari kwanza ili kuweza kupata maana kusudiwa. Hii si vyema kwa wageni wanaojifunza lugha tunayojisifia kwayo kuwa ni asili yetu.
 
 
Kusema, 'both adults & students' nadhani ni tafsiri ya moja kwa moja toka Kiswahili, haijakaa sawa. Mlinganisho uliotumika hapo ni wa makundi mawili ya nyanja mbili tafauti. Ni sahihi kulinganisha, 'Adults and Youths' au 'Students and Non-Students' kwa maana 'adult' akiingia darasani anakuwa 'student' vile vile 'student' anaweza kuwa 'adult'... namna gani vipi pale? Ipo haja ya wataalamu wa lugha kurekebisha haya.
Picture
neno sahihi kwa lugha ya Kiingereza ni 'adults' kwa maana ya 'watu wazima' kwa lugha ya Kiswahili
"Classes za Kiingereza..." yaani ni mwendo wa "ku-mix" lugha tu, haijalishi ni shuleni, mtaani, bungeni....!l

Ukiuliza sana utajibiwa, 'lakini si umeelewa?' mmh! Wewe weka bango lako hivyo, kisha washindani waweke lao lililoandikwa kwa ufasaha, hapo ndipo utaelewa maana ya 'akili ya kuambiwa, changanya na yako...".

Ndivyo tutakavyozungumza katika ushindani wa "Isti Afrikan Markiti"? 'ndo twaboronga hivyo halafu soko la pamoja likikolea, twakubali na kulalamika 'wenzetu wanatuzidi sisi hatujui chingereza', il hali wakati wa kukosoana kuwekana sawa, twaishia kuzodoana! Afanaleki! sisi ni sisi tu, chapa mfanowe "nehi".
 
 
Picture
Wafanyakazi wa Manispaa wakizoa taka katika soko la Ilala jijini Dar es Salaam. (credit: Prona Mumwi/DarLeo)
Mtizamaji, shuhudia jinsi gari hilo, ambalo hakuna uhakika kama ni maalumu kwa uzoaji taka au la, lilivyojazwa taka kiasi cha kuziba vioo vyote anavyotakiwa kuvitumia dereva wakati akiendeshagari awapo barabarani. Tizama nafasi ya upana iliyochukuliwa na taka hizo ulinganishe na ukubwa wa bodi ya gari ufikiri dereva aliyeko nyuma na anayepishana naye pembeni anatakiwa kukadiria vipi ukubwa halisi wa gari hilo.

Kwa mwendo huu kweli ajali za barabarani tunapambana nazo vilivyo au ni nadharia tu?

Vikosi vya kusimamia na kuhakikisha uwepo wa usalama barabarani wangekuwa wanafanya kazi yao ipasavyo, huenda wazoa taka hawa wasingethubutu kujaza uchafu kwa kipimo hiki. Lau, wananchi tungekuwa tunajali afya zetu na kutii sheria, tusingekuwa tunafanya au kukubali mambo hatarishi hivi.

Picha kama hizi pia za uvunjaji sheria kwa magari yanayozoa taka jijini Dar Es Salam, amekuwa akizipiga na kuziposti katika blogu yake bwana Othman Michuzi / Mtaa kwa Mtaa blog
 
 
Ama kwa hakika picha hizi nikizilinganisha na makasri yaliyojengwa sasa, na jinsi wanavyochukua sheria katika kutetea na kuhalalisha ni kwa nini waishi katika makasri yenye thamani hiyo, ati "hali halisi hasa ya usalama kipindi cha sasa ikilinganishwa na nyakati za Mwalimu...", wingi wa maswali unazidi majibu!
Picture
'Hii ndiyo nyumba ya Mwalimu Nyerere aliyokuwa akifikia alipokuwa akisafiri kwenda Butiama akiwa kama Rais wa Tanzania kati ya miaka ya sitini hadi miaka ya themanini mwanzoni.' 'Ni nyumba ambayo ina vyumba vinne. Viongozi wenzake wa wakati huo walipomtembelea Butiama walistaajabishwa na udogo wa nyumba yake, na ndiyo wakafikia uamuzi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kumjengea nyumba nyingine kubwa zaidi ambayo ilijengwa miaka ya themanini katika eneo la Mwitongo. Ni nyumba ambayo ina vyumba vinne. Viongozi wenzake wa wakati huo walipomtembelea Butiama walistaajabishwa na udogo wa nyumba yake, na ndiyo wakafikia uamuzi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kumjengea nyumba nyingine kubwa zaidi ambayo ilijengwa miaka ya themanini katika eneo la Mwitongo.' - *Madaraka Nyerere.
Picture
'Hii ni nyumba ambayo Chama cha Mapinduzi (CCM) ilimjengea Mwalimu katika miaka ya themanini. Nyumba hii ilijengwa kwenye eneo la mwinuko la Mwitongo kijijini Butiama. Ni nyumba ambayo Mwalimu Nyerere aliishi kwa kipindi kirefu baada ya kustaafu uongozi wa Serikali akiwa kijijini Butiama. Msanifu wa jengo hili ni mwanamama ambaye jina lake sijaweza kulipata, ambaye aliandaa pia michoro ya hoteli maarufu ya Lobo iliyopo kwenye mbuga za hifadhi za Serengeti.' - *Madaraka Nyerere'
Baada ya kwisha vita vya Kagera mwaka 1979, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) liliamua kumjengea Mwalimu Nyerere nyumba ya kuishi, ikiwa kama zawadi kwake kwa ushindi wa vita hivyo, akiwa Amiri Jeshi Mkuu wa wakati huo. Nyumba hiyo, ambayo ilijengwa Butiama ilijengwa na kitengo cha ujenzi cha JWTZ.
Imejengwa katika eneo la Mwitongo, karibu na eneo ilipojengwa nyumba nyingine ya Mwalimu Nyerere aliyojengewa na Chama cha Mapinduzi.

Ujenzi wa nyumba hii ulipoanza, wanajeshi walikatwa mishahara yao kuchangia gharama za ujenzi. Hata hivyo baadaye Serikali ya awamu ya pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi ilichukuwa jukumu la kuendeleza ujenzi ambao uliisha wakati wa Serikali ya awamu ya tatu ya Rais. Benjamin Mkapa, na kukabidhiwa kwa Mwalimu Nyerere mwaka 1999.

Aliishi kwenye nyumba hiii kwa siku 14 tu kabla ya kwenda kwenye matibabu Uingereza ambako alifariki tarehe 14 Oktoba, 1999. - *Madaraka Nyerere
Picture
'Nyumba iliyojengwa kuzungukia kaburi la Mwalimu Nyerere, eneo la Mwitongo, Butiama.' 'Kabla ya kufariki, Mwalimu Nyerere alielekeza sehemu ambapo angependa kuzikwa, pembeni tu ya sehemu alipozaliwa. Haikuwezekana kumzika alipotamka kwa sababu ni sehemu ambayo ulijengwa mfereji wa maji machafu. Sehemu iliyochaguliwa baadaye haikuwa mbali na eneo aliloelekeza yeye.' - *Madaraka Nyerere'
*Maelezo na Picha kama ilivyoainishwa, vimezipata kwenye blogu ya Madaraka Nyerere, mtoto wa Mwalimu.
 
 
Today I accessed "Google Translate" page and typed in 'natoka tanzania' which returned the translation, ' departed from kenya ', come again? Now this is what I call 'retarded' because the automated machine has been giving very funny translations sometimes to the extent of completely distorting the whole meaning. On the other hand, because the machine was fed those words by someone, who knew exactly what they were doing, and because those "ones" have issues, then every little text that is in Kiswahili is most probably skewed because it's translation came from non proper-Kiswahili speakers.
Picture
The proper Kiswahili language was born in Tanzania and spread to other countries, that is undeniable, even if the stars were to fall from the sky, who ever says otherwise is a blatant liar.

So please Google, and any other translating organisation, whenever you need a proper language, and in particular Kiswahili translation, make a little effort to verify the credentials of those applying for the job. No need  to mislead innocent people who trust your services just because some ignorant people got their hands first into computers thought "we" would never reach that stage.

Shame on whoever made that mistake intentionally, this and other shady business of yours will backfire.

Sisi Waswahili nasi tumelala mno! Tumeanza kuamka lakini bado tuna maluweluwe. Tuchangamke. Tuwasake hawa waharibifu na kuwakemea, tuwatimue wasituletee umang'aa wao.

Hat tip, mdau Japani via Issa Michuzi blog
 
 
Picture
Ipo herufi 'r' katikati ya 'a' na 'k' katika neno la Kiingereza, 'parking' lenye maana ya 'maegesho' kwa Kiswahili. Tutumie lugha fasaha, tusichoke kukosoana tunapokosea. Nami hukosea na hukubali kukosolewa.
 
 
Picture
Neno 'passport' la lugha ya Kiingereza lina maana ya 'pasi' kwa lugha ya Kiswahili. Nadhani walipaswa kuandika, 'passport size photo' kwani sehemu hii kwa uzoefu wa 'vijiwe vya mjini' hapa ni mahala pa kupigia picha kwa ajili ya pasi mbalimbali za utambulisho, asilani, hili si eneo maalum la Serikali kwa kutolea 'pasi'.
 
 
Watu wawili wamekufa na wengine kiasi cha 58 wameugua au wanaugua ugonjwa wa kuharisha na kutapika katika kiijiji cha Gomelo kilichopo katika kata ya Kisaki , tarafa ya Bwakila, Morogoro.

(credit: Mdau wa Morogoro via Beda Msibe/Lukwangule blog)
YATOKANAYO

Katika hali kama hii, wa kubeba lawama ni wahudumu wa afya, wananchi, Serikali ya Kijiji, Kata, Tarafa, Wilaya, Mkoa, Wizara?

Nasema wahudumu wa afya hasa Wauguzi kwani imezoeleka kuwa Muuguzi ndiye huyo huyo ahudumie wagonjwa na afanye shughuli nyingine zozote katika eneo la afya, ikiwa ni pamoja na kufanya usafi wa mazingira. Inawezekana kabisa kuwa jukumu hilo limekabidhiwa fani ya Uuguzi kwa kuwa uwezo wa kuajiri Idara ya Usafi ni mdogo. Lakini utekelezaji wake haumaanishi kuwa Muuguzi ndiyo anawajibika moja kwa moja kutenda yale yaliyo nje ya fani ya Uuguzi. Yaani inakuwa kana kwamba wenye taaluma ya usafi na mazingira hawapo. Ninawalaumu wauguzi wenyewe moja kwa moja kwani inadhihirisha kuwa hawafahamu jukumu lao kuu ni UUGUZI. Wengi hujifanyia kazi kwa mazoea tu na itokeapo yupo atakayehoji iweje Muuguzi ndiye ashike ufagio, tando la kuondolea buibui, keni la maji, shimo la taka, incinerator, ufunguo wa stoo, daftari la stoku, uagizaji vifaa... na kumhudumia mgonjwa kwa wakati - huyo atakiona cha mtema kuni! Ataitwa mkorofi na mshari, mpenda ukuu, mpenda kujilinganisha, asiye na utii nk nk. Mimi nasema hii ni kutokuwa na mwelekeo (lack of focus) na kujiona kuwa waweza kufanya kila kitu (multi-tasking) ambapo matokeo yake ni kutokutimiza kikamilifu shughuli yoyote kusudiwa ikiwemo ya kutoa huduma kwa mgonjwa (under-performance or lack of, all together). Mwaichanganya jamii nzima, kwani hamueleweki haswa jukumu lenu lipi kwa maana hata kuhudumia wagonjwa bado ni lawama debe!

Nasema Wananchi kwani upo wito kwa wananchi kujisushulisha katika kuboresha mazingira ya huduma za kijamii mojawapo ikiwa ni katika Zahanati na vituo vya afya. Wananchi wanaweza kujitokeza ana kwa ana kwa shughuli hizo au kutoa kiasi fulani cha fedha au malipo yatakayokubalika kwa ujira wa yule atakayekuwa tayari kufanya kazi husika.

Nasema Serikali ya Kijiji, Kata, Tarafa, Wilaya, Mkoa na Wizara kwani hizi ndizo ngazi za ufuatiliaji wa maeneo yanayotoa huduma katika jamii. Hizi ngazi za utendaji na ufuatiliaji zimewekwa kwa makududi kwa minajili ya kurekebishana na kuhakikisha kila jambo linakwenda sawa. Uonapo hali kama hii, bila kujali kwamba ni sekta ya Afya, Elimu, Miundombinu nk, basi fahamu fika kuwa upo uzembe mahali fulani katika ngazi ya utendaji na utekelezaji.

Inashangaza kabisa kuona kwamba hakuna aliyewajibika wala anayewajibisha katika hili. Huku ni kufeli.
 
 
Picture
Kulingana na maelezo, huenda neno sahihi lilipaswa kuwa, Communication (English) Mawasiliano (Kiswahili).
Hilo neno 'commucation' ingekuwa limeandikwa kwa kutumia tarakilishi tungesema, 'typos' (yaani bahati mbaya limeponyoka) sasa hapa pengine kosa lilitendeka kutokana na kukosekana umakini kwa mwandishi? au kutokuwepo uhakiki kwa mmiliki wa sehemu husika? ama wote walighafilika kutokana na kiwango cha elimu? Sasa hata wateja au marafiki nao hawawezi kukosoa japo kumsaidia mwenye biashara? Au mwenye bishara naye kichwa ngumu? Kwa maana wapo wafanya biashara wanaosema, 'acha tu wataelewa hivyo hivyo"... na huo ndiyo mwendelezo wa uharibifu na matumizi mabaya ya lugha, hasa lugha ngeni.
 
 
Picture
Wanafunzi wa shule ya Msingi wakicheza mchezo wa kuteleza katika eneo la ngazi za kupandia kwa miguu zilizopo Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam huku mvua ikinyesha jana. (photo credit: Fadhili Akida via Haki Ngowi blog)
Mara nyingi watu wazima wamekuwa wakisahau au kutokutambua umuhimu wa michezo kwa watoto. Imezoeleka kwa wazazi kuwakataza watoto wao kucheza kana kwamba michezo ni dhambi. Heko ni kwa wazazi na walezi wanaokataza watoto kutumia muda mwingi katika michezo na badala yake wakawasaidia kupanga ratiba ya kuweka uwiano kati ya michezo na shughuli nyingine za kawaida ikiwamo shunguli za kukamilisha maihitaji ya mwanadamu kama vile usafi, kilimo, biashara na kuzingatia masomo.

Tatizo kubwa nililoliona hapa lipo katika kuwanyima kabisa nafasi ya michezo!

Wapo watakaokejeli kuwa, 'yaani badala ya kujali kujenga nyumba unasema watoto wakacheze? we vipi, unataka wakalale wapi sasa wakishamaliza kucheza?'

Nami ningependa kujibu swali kwa swali, tatizo lako la kutaka kuishi mjini na maeneo yaliyobanana isiwe adhabu kwa wanao wa kuwazaa. Ulitumwa kuwazaa ujewatesa kwa kuwanyima haki zao za michezo?

Tumesahau kuwa katika  maisha ya sasa ambayo ajira ni adimu, michezo nayo imekuwa sehemu ya ajira. Hivyo kuwanyima watoto na vijana maeneo ya michezo ni kuwanyima uwezekano wa kupata ajira katika nyanja za michezo.

Maisha ni kupanga, hujalazimishwa kung'anga'ania mjini. Wengi husema 'tutabanana hapa hapa' ndiyo penye 'dili' na maisha yanakwenda, lakini ikumbukwe pia kuwa hata wanaoishi nje ya mji maisha yanakwenda.

Tukizaliana wengi, basi tuwe na mipango ya kutuwezesha kumudu mahitaji yetu. Tunang'ang'ania mahali pamoja ndiyo maana shughuli zote badala ya kupanuka kwenda kufuata makazi, watu wanapeleka makazi katika maeneo ya kazi. Hii ndiyo mojawapo ya matokeo ya msongamano barabarani.