Google invests In "wingu" startup 07/07/2011
Information provided by CrunchBase says, Google Ventures has quietly invested in a stealth startup called Wingu, reports StrategyFacts (subscription required). Indeed, while the Google Ventures website lists four career opportunities for one of its portfolio companies located in Cambridge, Massachusetts without naming Wingu, the stealth startup published the exact same job openings on its job board, leaving nothing to the imagination. Wingu is building a enterprise-grade cloud platform dubbed Elements that will enable research teams to collaborate more effectively and use data in ‘new ways’. Umesema Wingu? Ndiyo, umesoma vyema. Wingu kama tulijuavyo kwa Kiswahili! Ni neno mojawapo la Kiswahili kati ya mengi ambayo yametumika vyema katika ulimwengu wa sayansi na TEHAMA. Pamoja na kujivunia lugha yetu, pia tuitumie kwa faida. Siyo sisi tubakie tukidai, sisi ni Waswahili, ni wazawa, ni wenye lugha, while others are making use of it! Tupo mbio kutunga maneno yasiyo na kichwa wala miguu, kila leo kuchanganya maneno hata inafika pahala hatuelewani wala kuamini kuwa sote tunasema Kiswahili. Wakati wengine wanayanyemelea na kuyatumia kwa faida, sisi tuendelee kuboronga Swanglish? Hapana. Watu hawa wametengeneza 'wingu kemia' soma maeleoz kwenye blogu yao http://blog.wingu.com Hakuna ubaya wowote kwa wao kutumia maneno ya lugha hiyo, ila nasi Waswahili tuchangamke. Add Comment Nkyea releases Swahili iPhone and iPad App. 13/06/2011
Nana Sarpong and Isaac Ameyaw who started in Nkyea Learning Systems in 2009 to develop desktop and mobile applications for learning African languages have released Nkyea Basic Swahili on the Apple App Store. Nkyea Basic Swahili, which sells for $2.99, contains more than 650 essential words and phrases in 18 lessons of basic grammar, vocabulary and pronunciation packed with over 1600 sound files of high audio instruction by a Swahili language professional from Kenya! The user can then choose a lesson, listen to the native speaker, read and record, play back and compare with the native speaker. The app also presents you with a quiz after each topic, which means users can reinforce what they learn and earn motivation badges for scoring high marks. “This is a very user friendly language learning application, “Sarpong explains. “It’s really easy to learn Swahili with Basic Swahili.” Nkyea Basic Swahili is targeting four primary markets: Tourists traveling to East Africa, students learning Swahili at a beginner level in school, anybody who has an East African relative or friend and lastly, language enthusiasts. Nkyea remains a bootstrapped endeavor, wholly financed through the startup’s PC, Mac and iPhone application sales. For more information on this App contact Nana Sarpong, at (233) 244153566 or send an email to nana.sarp@gmail.com Nadhani ilipaswa isomeke, "Abiria toa hela" lakin pengine maneno sahihi ni "Abiria lipa nauli", kwa maana ukimwambia abiria atoe hela bila makubaliano maalumu, anaweza kushindwa kuelewa atoe pesa ngapi. Picha hii imenaswa na kamera ya McKepha akiwa ndani ya daladala, Tanzania. BAKIZA yazindua Kamusi la Kiswahili Fasaha 18/10/2010
Ndiyo, ujumbe umefika, lakini, lugha imenyewa! Haifai kuwa hivi. Lipo tatizo kubwa kwa baadhi ya watu wa makabila fulani nchini Tanzania kuhusiana na matumizi ya herufi, 'R' na 'L' au 'H' na 'U' katika matamshi na hata kwenye maandishi. Pia, wapo wale ambao hushindwa kutofautisha kati ya herufi 'S' na 'Z' au 'P' na 'B' ama 'V' na 'F' na 'DH' na 'Z' na kadhalika. Ingawaje kwa maneno mengine huwa si rahisi kupoteza maana kusudiwa, makosa hayo bado huweza kuleta maana tofauti kabisa na iliyokusudiwa, hasa kwa mgeni au mwanafunzi wa lugha ya Kiswahili. Kwa mfano, neno 'ukiri' ni tofauti na neno 'ukili' au 'karamu' na 'kalamu'. Vile vile 'kazi' ni tofauti na 'kasi' kama ilivyo 'vuma' ikawa tofauti na 'fuma'. Kadhalika, 'barua' ni tofauti na 'parua' ama 'dhana' na 'zana'. Matumizi yasiyo sahihi ya maneno hayo humlazimisha msomaji kujua maudhui ya habari kwanza ili kuweza kupata maana kusudiwa. Hii si vyema kwa wageni wanaojifunza lugha tunayojisifia kwayo kuwa ni asili yetu. Kiswanglish matege: Both 'adullts'... 22/07/2010
Kusema, 'both adults & students' nadhani ni tafsiri ya moja kwa moja toka Kiswahili, haijakaa sawa. Mlinganisho uliotumika hapo ni wa makundi mawili ya nyanja mbili tafauti. Ni sahihi kulinganisha, 'Adults and Youths' au 'Students and Non-Students' kwa maana 'adult' akiingia darasani anakuwa 'student' vile vile 'student' anaweza kuwa 'adult'... namna gani vipi pale? Ipo haja ya wataalamu wa lugha kurekebisha haya. "Classes za Kiingereza..." yaani ni mwendo wa "ku-mix" lugha tu, haijalishi ni shuleni, mtaani, bungeni....!l Ukiuliza sana utajibiwa, 'lakini si umeelewa?' mmh! Wewe weka bango lako hivyo, kisha washindani waweke lao lililoandikwa kwa ufasaha, hapo ndipo utaelewa maana ya 'akili ya kuambiwa, changanya na yako...". Ndivyo tutakavyozungumza katika ushindani wa "Isti Afrikan Markiti"? 'ndo twaboronga hivyo halafu soko la pamoja likikolea, twakubali na kulalamika 'wenzetu wanatuzidi sisi hatujui chingereza', il hali wakati wa kukosoana kuwekana sawa, twaishia kuzodoana! Afanaleki! sisi ni sisi tu, chapa mfanowe "nehi". Neno sahihi ni 'parking' 21/06/2010
Ipo herufi 'r' katikati ya 'a' na 'k' katika neno la Kiingereza, 'parking' lenye maana ya 'maegesho' kwa Kiswahili. Tutumie lugha fasaha, tusichoke kukosoana tunapokosea. Nami hukosea na hukubali kukosolewa. Neno sahihi ni 'passport' 19/06/2010
Neno 'passport' la lugha ya Kiingereza lina maana ya 'pasi' kwa lugha ya Kiswahili. Nadhani walipaswa kuandika, 'passport size photo' kwani sehemu hii kwa uzoefu wa 'vijiwe vya mjini' hapa ni mahala pa kupigia picha kwa ajili ya pasi mbalimbali za utambulisho, asilani, hili si eneo maalum la Serikali kwa kutolea 'pasi'. Unaelewa nini hapa? Swanglish matege! 02/06/2010
Siyo utani, kejeli au kukebehi, ukweli ni kwamba sijaelewa maana ya tangazo hili. Kwa kuitizama picha napata wazo kwamba tangazo linahusiana na mikanda ya filamu inayoonekana hapo. Hivi kweli lugha ya Kiswahili imeshabadilika na kujaa maneno hivi? Haya maneno tafsiri yake inapatikana kirahisi kweli? Mlengwa katika lugha hii ni kijana wa kijiweni, Mtanzania, Mgeni au mtu gani hasa? Nadhani neno 'mtaharam' aliataka kuandika, 'mtaalamu' Je, neno 'kupwenti' alitaka kuandika, 'ku-point' ama neno hili tayari lina maana tafauti? Na neno 'muvu' ni Kuswahilisha neno la Kiingereza, 'move' ama maana kusudiwa ni nyingine? Pengine wakati mwingine mambo mengine yanahitaji kupuuziwa kwa kuwa 'hayanihusu', wale yanaowahusu watakuwa wameupata ujumbe. Tatizo nililo nalo, akiniuliza mtu mwingine maana ya ujumbe huo nitamjibu vipi? Pengine nitabaki tu kumwambia 'sijui' au 'nadhani' kama nilivyonyambulisha hapo juu, na pengine nitamweleza tu kuwa, 'kwa hilo, mimi kama wewe nimetoka kapa'. Mbaya zaidi ni ikiwa atakuwepo mgeni au mtalii akapekenyua kamusi yake na asione maneno hayo, kisha aniulize maana yake, pengine nitamjibu, 'lugha ya wahuni hiyo' au 'lugha nisiyoijua maana yake' na sidhani kama inawakilisha kabila lolote. Nia nzuri. Tatizo lugha; Swanglish matege! 01/06/2010
Nimefahamishwa, "hii GH ipo Ifakara, ni nzuri na huduma poa kabisa, ila kwa hiyo 'ICE' no comment". Wito wangu ni kuwa tujitahidi kuandika lugha mojawapo kwa ufasaha. Hata mgeni anayezungumza Kiingereza anatarajia kusoma Kiswahili fasaha ndipo aweze kutafsiri kwa kamusi aweze kupata maana kusudiwa. Ikiwa unaweza kuandika Kiingereza fasaha, basi fanya hivyo, la inashindikana, basi tafuta mtafsiri. Hiyo itaisaidia biashara yako kukua. Tujifunze kutokana na makosa haya na tuwasaidie wengine kurekebika. | Vitabu vya WatanzaniaBofya picha ya kitabu unachokitaka ili ujinunulie nakala
Yaliyomo/CategoriesAll Hifadhi/ArchivesFebruary 2012 |














RSS Feed