Wapinzani kuungana na Ukomavu wa Kisiasa 07/20/2010
Wiki hii limetokea jambo katika anga za siasa ambapo waliokuwa wanachama wa CCJ ambao awali walijitenga na CCM wameamua kujiunga CHADEMA. Hili si jambo geni kwa kuwa tumewaona baadhi ya viongozi wa vyama kadhaa pinzani wakijiunga na hata kuzungumzia tetesi za wao kutaka kuunganisha vyama kabisa. Kwa mtizamo wangu, nadhani hii ni mojawapo ya ukomavu, kukua na kupevuka katika uhuru na demokrasia. Nasema hivi kwani, tangu kuanzishwa kwa demokrasia ya vyama vingi, watu wengi walijiengua toka CCM na kutaka kutumia uhuru uliopatikana kwa kuanzisha vyama. Angalabu, vyama vingi vilianzishwa kwa kuwa baadhi ya watu waliona sera za vyama fulani haziendani na matakwa au sera zao. Vilianzishwa vyama zaidi ya ishirini. Baada ya uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995, na baada ya kuanguka kwa vyama hivyo katika ngazi za udiwani, ubunge hata uraisi, baadhi ya vyama hivyo vilikufa kifo cha kawaida. Vipo vilivyobaki na vipo vipya vilivyoanzishwa, ama kwa kuungana au kwa kufuta na vya zamani na kuunda vipya kabisa. Hiyo nayo ni hatua katika demokrasia ya kisiasa na matumizi ya uhuru wa kuchagua. Hivi sasa, vyama vya upinzani nchini Tanzania si utitiri mkubwa wa kumchosha mwananchi. Angalao vyama vinavyotoa changamoto vinahesabika kwa vidole vya mkono mmoja. Bado kwa mtizamo wangu, naona hii ni hatua muhimu katika ukomavu wa demokrasia na siasa. Kitendo cha viongozi wa CCJ kujiunga CHADEMA kinamsaidia mwananchi wa kawaida kupunguza utitiri wa idadi ya vyama anavyotakiwa kufahamu na kumwacha na jukumu la kukumbuka wagombea tu. Ikiwa siasa zetu zinaakisi zile za mataifa ya nje, tutakubaliana kuwa katika nchi hizo, mabadiliko yamekuwa yakifanyika ndani ya mpambano wa vyama viwili au vitatu vikuu. Mifano hii ni hai kwa nchi kama vile Uingereza, Marekani, Kenya nk. Nchi hizi zilianzia tulikoanzia sisi kwa kuwa na mlolongo wa vyama, vikapungua na hatimaye kusonga hadi kufika zilipo sasa. Jirani zetu Kenya wameweza kung'oa KANU baada ya kuungana hata ikiwa muunganiko huo ni wa mashaka na wenye mgogoro, bado lengo lao kuu la kuiondoa madarakani KANU lilifanikiwa. Sasa ni kwa namna gani wataitumia fursa hiyo kuwahimiza wananchi katika kujitelea maendeleo, hilo ni suala la wananchi kuuliza na kushinikiza kupata majibu na mwongozo unaofaa. Hivi ndiyo kusema, ninawapongeza kwa dhati kabisa viongozi wa CCJ kwa kitendo chao cha kuhamia CHADEMA na zaidi ya hayo, kuwahimiza wanachama wengine kufanya hivyo. Ni kweli kuwa yawezekana ukawepo msukumo wa ubinafsi au uroho wa madaraka katika kuhama vyama, lakini dhana hii si alama ya chama au watu fulani tu, hii ni hali dhahiri kwa kila chama, kwamba wapo wanachama wenye uroho kila mahali. Hawa ni watu tunaokutana nao na wanaotoka katika jamii tunamoishi. Ikiwa tunawafahamu kwa uthibitisho usiopingika kuwa nia zao ni chafu, basi wananchi ndiyo tulio na uwezo wa kuwakataa kwa njia halali ya kutokuwapa kura zetu za ndiyo. Kuwepo katika chama fulani tu haitoshi kuwa sababu ya kutokuonekana mroho au mbinafsi wa madaraka; hali kadhalika, kuwepo katika chama fulani tu haitoshi kumaanisha kuwa watu wake tayari ni wabinafsi na waroho wa vyeo na madaraka. Aliyesema, Umoja ni nguvu na Utengano ni udhaifu, hakuwa amekosea ijapokuwa wakati mwingine ni vyema na sahihi kabisa kutengana, hii ni kweli inapotokea mtoto anajitenga na familia ili kuanzisha mji au familia yake. Vivyo hiyo katika siasa, uwepo wa vyama zaidi ya kimoja ni muhimu ili kuleta changamoto kila linapoonekana jambo linakwenda kombo. Wakati mwingine inabidi awepo mtu nje ili kuweza kuona jambo kwa mapana na marefu yake, wenyewe wasemaji wa lugha ya Kiingereza wanasema, 'check and balance', yaani lazima wawepo wahakiki na hawa watafanikiwa vyema ikiwa watakuwa nje au kutokufungamana na upande wowote kama yafanyavyo mashirika ya kitaaluma. Natamani kuifikia siku ile ambapo nitaona na kusikia kuwa vyama vikuu vya kisiasa nchini Tanzania ni viwili ama vitatu na pia nafasi ya mgombea huru imethaminishwa. Ama kwa hakika picha hizi nikizilinganisha na makasri yaliyojengwa sasa, na jinsi wanavyochukua sheria katika kutetea na kuhalalisha ni kwa nini waishi katika makasri yenye thamani hiyo, ati "hali halisi hasa ya usalama kipindi cha sasa ikilinganishwa na nyakati za Mwalimu...", wingi wa maswali unazidi majibu! ![]() 'Hii ndiyo nyumba ya Mwalimu Nyerere aliyokuwa akifikia alipokuwa akisafiri kwenda Butiama akiwa kama Rais wa Tanzania kati ya miaka ya sitini hadi miaka ya themanini mwanzoni.' 'Ni nyumba ambayo ina vyumba vinne. Viongozi wenzake wa wakati huo walipomtembelea Butiama walistaajabishwa na udogo wa nyumba yake, na ndiyo wakafikia uamuzi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kumjengea nyumba nyingine kubwa zaidi ambayo ilijengwa miaka ya themanini katika eneo la Mwitongo. Ni nyumba ambayo ina vyumba vinne. Viongozi wenzake wa wakati huo walipomtembelea Butiama walistaajabishwa na udogo wa nyumba yake, na ndiyo wakafikia uamuzi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kumjengea nyumba nyingine kubwa zaidi ambayo ilijengwa miaka ya themanini katika eneo la Mwitongo.' - *Madaraka Nyerere. ![]() 'Hii ni nyumba ambayo Chama cha Mapinduzi (CCM) ilimjengea Mwalimu katika miaka ya themanini. Nyumba hii ilijengwa kwenye eneo la mwinuko la Mwitongo kijijini Butiama. Ni nyumba ambayo Mwalimu Nyerere aliishi kwa kipindi kirefu baada ya kustaafu uongozi wa Serikali akiwa kijijini Butiama. Msanifu wa jengo hili ni mwanamama ambaye jina lake sijaweza kulipata, ambaye aliandaa pia michoro ya hoteli maarufu ya Lobo iliyopo kwenye mbuga za hifadhi za Serengeti.' - *Madaraka Nyerere' Baada ya kwisha vita vya Kagera mwaka 1979, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) liliamua kumjengea Mwalimu Nyerere nyumba ya kuishi, ikiwa kama zawadi kwake kwa ushindi wa vita hivyo, akiwa Amiri Jeshi Mkuu wa wakati huo. Nyumba hiyo, ambayo ilijengwa Butiama ilijengwa na kitengo cha ujenzi cha JWTZ. Imejengwa katika eneo la Mwitongo, karibu na eneo ilipojengwa nyumba nyingine ya Mwalimu Nyerere aliyojengewa na Chama cha Mapinduzi. Ujenzi wa nyumba hii ulipoanza, wanajeshi walikatwa mishahara yao kuchangia gharama za ujenzi. Hata hivyo baadaye Serikali ya awamu ya pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi ilichukuwa jukumu la kuendeleza ujenzi ambao uliisha wakati wa Serikali ya awamu ya tatu ya Rais. Benjamin Mkapa, na kukabidhiwa kwa Mwalimu Nyerere mwaka 1999. Aliishi kwenye nyumba hiii kwa siku 14 tu kabla ya kwenda kwenye matibabu Uingereza ambako alifariki tarehe 14 Oktoba, 1999. - *Madaraka Nyerere ![]() 'Nyumba iliyojengwa kuzungukia kaburi la Mwalimu Nyerere, eneo la Mwitongo, Butiama.' 'Kabla ya kufariki, Mwalimu Nyerere alielekeza sehemu ambapo angependa kuzikwa, pembeni tu ya sehemu alipozaliwa. Haikuwezekana kumzika alipotamka kwa sababu ni sehemu ambayo ulijengwa mfereji wa maji machafu. Sehemu iliyochaguliwa baadaye haikuwa mbali na eneo aliloelekeza yeye.' - *Madaraka Nyerere' *Maelezo na Picha kama ilivyoainishwa, vimezipata kwenye blogu ya Madaraka Nyerere, mtoto wa Mwalimu. Hilo ni swali aliloliuliza kijiweni kwake juzi "mwananchi mimi" bloga Fadhy Mtanga. Swali lililotoa changamoto hasa kwetu ambao ni wapenda kufahamu mambo ili kupata ahueni ya kutokukaa 'Vilaza Room' muda wote. Kwa kuwa swali hilo halikupata majibu muafaka, na mimi nikiwa nishaingia "Vilaza Room" nikaona isiwe taabu, mguu mmoja hadi kijiweni Facebook, aidha nipate jawabu sahihi ama niongeze wafuasi 'Vilaza Room'. Maoni kadhaa yalitolewa na yalinifurahisha sana, mfano ni rafiki yangu Kalolo, yeye alichonifurahisha ni kwa kutokubali moja kwa moja kuingia 'Vilaza Room' bila ya kurusha ngumi kidogo, hivyo akajibu swali kwa kuuliza swali, ati, 'kuelekea wapi?'... Ama kabla ya hapo, alinifurahisha rafiki yangu Ng'wanambiti alipojibu katika blogu ya 'Mwananchi Mimi' kuwa inaanzia 'baharini'... sasa pamoja na 'umaimuna' wangu, nilishindwa kufahamu mwenzangu anagusia eneo lipi hasa la 'baharini' ndipo nikamwuliza mwenzetu wewe, "Kunduchi, Selander, Agha Khan, Feri, Bandarini, Kigamboni", wapi hasa? 'Schoolmate' wangu Chela pamoja na marafiki zangu wengine wa kijiji cha Facebook walijibu kuwa, inakoanzia sifuri ya umbali katika mkoa wa Dar Es Salaam ni katika Mnara wa Askari "Askari Monument", lakini saa chache baadaye kijiweni pale akafika 'schoolmate' wangu Carol, na 'uncle' Ray wakatukuta tupo katika gumzo na akina Kalolo, Abdala na Nico. Basi Carol na Ray wakatuasa, enyi wenye kutaka kupata ufahamu na kujua mambo, basi fahamuni ya kuwa, kwa hakika inakoanzia sifuri hii ni katika Mnara wa Saa, tena Carol akasisitiza kwa Kiinglish kabisa, "Clock Tower!!!"...! Majibu mawili yanajirudia sana hapa. Lazima moja kati ya hayo litakuwa ndilo jibu sahihi. Lakini unang'amua vipi usahihi wa jibu ikiwa huna si 'four table' ama 'past pepa' wala 'compass' la 'kugelezea' kujua jibu sahihi? Ndipo ikabidi kutumia ile kauli ya '...akili ya kuambiwa, changanya na yako...' nikakumbuka, ala, Baba ni Mhandisi Barabara, shida yote ya nini? Si "umtwange" swali hili akufahamishe katika upimaji wao wa barabara na mipango miji, kianzio au "center" huwa ni ipi? Yaani huanzia wapi kuihesabu hii sifuri? Sasa Baba naye akibanwa na shughuli, basi kusoma ujumbe kwenye barua pepe huwa si kipaumbele. Saa kadhaa zikapita bila majibu. Ilibidi 'nimkone' dogo Kevin aniulizie jibu 'fasta' hapo 'homu' maana niliona sasa pale kijiweni fesibuku karibu watu watatoana ng'eu. Basi jibu sahihi toka kwa Mhandishi wa Barabara na Mkazi wa Dar "ilipokuwa Dar kweli kweli enzi za Mwalimu", Engineer S. Tarimo akatoa 'fact' kuwa Kilometa sifuri katika Jiji la Dar Es Salaam inaanza kuhesabiwa katika MNARA WA SAA ndiyo CLOCK TOWER. Na ukweli ujulikane hivyo! Iweke hii katika kumbukumbu zako kwa faida yako na kizazi kijacho. Tusipoijua historia yetu na kuihifadhi, ni rahisi sana kubadilishwa na kupotoshwa. Imeandikwa hapa na itadumu hapa kwa urahisi wa kuirejea. Tukiwa tunahimizwa katika kauli mbiu ya Kilimo Kwanza, nimekuwa nikijiuliza ikiwa wakulima wanaohimizwa tayari wana mipango madhubuti ya kuuza au kuhifadhi mazao hayo punde msimu wa mavuno utakapowadia. ![]() Mkazi wa Kijiji cha Kipera Wilayani Mvomero mkoani Morogoro akiwa amepakia matenga ya nyanya katika pikipiki akiyapeleka sokoni kutoka shamba. Msimu wa mavuno wa zao la nyanya ambalo ni la biashara kwa wakazi wa Kipeara na vitongoji vyake umewadia lakini bei ya tenga moja la nyanya kama lililopakiwa katika pikipiki ni sh 3,000/= bei ambayo bado inaumiza wakulima. (credit: Mroki Mroki) Wasiwasi wangu ni kufanikisha dhana ya Kilimo Kwanza halafu mkulima ale hasara kwa kukosa soko litakalorejesha fedha ya mtaji na faida tarajiwa. Tunafahamu fika jinsi ilivyo taabu kupenyeza mazao ya chakula na maua katika nchi za nje hasa Ulaya. Sina uhakika tumeweza vipi hadi sasa kupenya katika masoko haya, hata na hivyo, mimi si mhusika wala mtaalamu wa nyanja hizo, hivyo siwezi kulisemea hili ama kinachonitia wasiwasi ni kuwa sijasikia wala kusoma taarifa za habari zinazoelezea jinsi Wakulima walivyonufaika na uuzaji mazao yao nje ya nchi. Ama pengine takwimu zake hadi kuzifuata katika Wizara, mashirika na taasisi fulani, kwa kuwa huu ndiyo mtindo uliozoeleka, yaani, kufanya tafiti na kuweka matokeo kwenye mafaili na kisha kuyafungia kwenye makabrasha na kuyaweka makabatini. Niendelee kuamini kuwa, pengine Kilimo Kwanza kitakuwa na kipaumbele katika mazao fulani tu, hasa mazao ya biashara ambayo huweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu. Natarajia kuwepo himizo na mkakati wa kuwasaidia Wanunuzi na Wafanyabiashara kujenga maghala muafaka ya kuhifadhia mazao. Natumai vile vile kuwa himizo litakuwepo kwa wenye mtaji wanaotaka kuanzisha viwanda vya kusindika malighafi ya mazao. Chonde chonde, yale tunayoyaona yakiyotokea mashambani na katika vituo vikuu vya mabasi kama vile Segera au Chalinze kwa matunda kuoza, yasigeuke kuwa janga la kitaifa la kauli mbiu ya Kilimo Kwanza. Sometimes "Google Translate" is 'retarded' 07/07/2010
Today I accessed "Google Translate" page and typed in 'natoka tanzania' which returned the translation, ' departed from kenya ', come again? Now this is what I call 'retarded' because the automated machine has been giving very funny translations sometimes to the extent of completely distorting the whole meaning. On the other hand, because the machine was fed those words by someone, who knew exactly what they were doing, and because those "ones" have issues, then every little text that is in Kiswahili is most probably skewed because it's translation came from non proper-Kiswahili speakers. The proper Kiswahili language was born in Tanzania and spread to other countries, that is undeniable, even if the stars were to fall from the sky, who ever says otherwise is a blatant liar. So please Google, and any other translating organisation, whenever you need a proper language, and in particular Kiswahili translation, make a little effort to verify the credentials of those applying for the job. No need to mislead innocent people who trust your services just because some ignorant people got their hands first into computers thought "we" would never reach that stage. Shame on whoever made that mistake intentionally, this and other shady business of yours will backfire. Sisi Waswahili nasi tumelala mno! Tumeanza kuamka lakini bado tuna maluweluwe. Tuchangamke. Tuwasake hawa waharibifu na kuwakemea, tuwatimue wasituletee umang'aa wao. Hat tip, mdau Japani via Issa Michuzi blog ♪ Shosholoza ♪ 05/23/2010
Ni wimbo wa asili ya Kusini mwa Afrika wenye kuhamasisha na kutia moyo. Uliimbwa na watu waliokuwa wakielekea vibaruani nchini Afrika Kusini, kwa asili wakitokea Zimbabwe (maelezo yapo hapo chini). Ni wimbo ambao nimekuwa nikiuimba kwa takribani wiki nzima sasa. ♫ Shosholoza, Shosholoza; Kule Zontaba, Stimela siphume South Africa Wen'uyabaleka, Wen'uyabaleka; Kule Zontaba, Stimela siphume South Africa ♪♪ ORIGINAL: Shosholoza Ku lezontaba Stimela siphum' eSouth Africa. Wen' uyabaleka, Wen' uyabaleka Ku lezontaba Stimela siphum' eSouth Africa. (ROUGH TRANSLATION: Move fast on those mountain strain from South Africa. You are running away on those mountain strain from South Africa). Shosholoza is a traditional Southern African folk song. The song was traditionally sung by all-male work gangs in a call and response style. The song has been recorded by a variety of artists, including Helmut Lotti, Ladysmith Black Mambazo, PJ Powers, The Glue, Soweto Gospel Choir, Peter Gabriel and Drakensberg Boys' Choir, as well as being a standard of most gumboots bands. The song gained further popularity after South Africa won the 1995 Rugby World Cup, and is a favourite at sport events in South Africa. The South African boy band Overtone recorded the song for director Clint Eastwood's movie Invictus (2009), in which the 1995 World Cup victory plays a central role in newly-elected president Nelson Mandela's desire to unite the racially-divided country. The word Shosholoza means go forward or make way for the next man, and is also reminiscent of the sound made by the steam train (stimela) described in the song. The song was originally sung by Ndebele migrant workers travelling home from South Africa, hence the lyrics. The Ndebele live predominantly in Zimbabwe (at the time known as Rhodesia), and whilst Ndebele and Zulu are very similar, the song is Zimbabwean in origin. The song has also given its name to Team Shosholoza, the first African challenger for the America's Cup, and to Shosholoza Meyl, the long-distance passenger train service operating in South Africa. This was not originally a song of joy or victory. It was sung by workers on way to the mines, a harsh and dark reality of hard labor for low pay. It has since come to represent the banding together of a people, their pride and dignity, and their progression into a new and free world. Explanation of the song "Shosholoza" was retrieved from Wikipedia - the free encyclopedia . Vijana, Kwanini hatushiriki kupiga kura? 05/15/2010
![]() Dakika kadhaa zilizopita nilikuwa nikitazama ukurasa wangu wa facebook. Nilishtuka sana baada ya kusoma maoni ya mmojawapo wa marafiki zangu. Sikuamini alichoandika ilibidi nikirudie mara mbili mbili kujiaminisha ndicho. Kifupi alikuwa anamueleza rafiki yetu mwingine kuwa yeye hajajiandikisha kupiga kura na wala hana mpango wa kwenda kupiga kura wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Nilishtuka sana kwa sababu kuu mbili. Kwanza sikutegemea uamuzi kama ule utoke kwa kijana msomi kama yeye. Lakini pia sikutarajia uamuzi kama ule utolewe na kijana anayelilia mabadiliko katika nchi yake. Nilishindwa kujizuia, nikaamua kumuuliza kujiaminisha kuwa asemacho ndicho, na ndivyo alivyokiri kwa hakika kabisa kuwa hatapiga kura. Sababu kuu zikiwa haoni ni kwanini apoteze muda wake kupiga kura wakati anadhani hakutakuwa na mabadiliko yeyote na hivi kupiga au kutokupiga kwake kura hakutaleta tofauti yeyote. Lakini jingine lililomfanya afikie uamuzi huu ni kuwa hotuba ya mheshimiwa Rais ambayo kwake anasema ilimkatisha tamaa na hakuona umuhimu wa kupiga kura tena. Uamuzi wake huu bila shaka unaakisi kelele za muda mrefu kuhusu ushiriki wa vijana katika uchaguzi wa viongozi wa Taifa letu. Ni mara kadhaa tumesikia watu ama makundi ya watu wakisisitiza kuhusu umuhimu wa vijana kushiriki katika kupiga kura ama hata kugombea uongozi. Wakati wa uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi wa mwaka 1995, mgombea mmoja wa urais kwa chama cha upinzani alidanganywa na idadi kubwa ya vijana waliokuwa wakijitokeza kwenye mikutano yake ya kampeni. Kundi hilohilo pia lilikuwa likijitokeza katika kulisukuma gari lake na kumshangilia, lakini ambacho mgombea yule hakuelewa ni kuwa vijana wale wala hawakuwa wamejiandikisha kupiga kura wala hawakupiga kura. Na hivi hata idadi ya kura zake haikuwa kama alivyotarajia. Hapo utaona kuwa kumbe vijana wale walitamani mabadiliko lakini walitaka mabadiliko hayo yaletwe na nani na kwa njia gani kama si wao kujiandikisha na kupiga kura? Swali la kujiuliza hivi ni kwanini vijana hawapendi ama hawataki kujihusisha katika kuchagua au kuchaguliwa? Inawezekana kukawa na majibu mengi kwa kila mmoja wetu, lakini je hayo majibu yanatosheleza sababu za kutokutumia haki yako ya kikatiba ya kuchagua au kuchaguliwa? Ifahamike kwamba katika kufanya mabadiliko kuna kadhaa lakini zilizo kuu ni mbili, ama za kutumia demokrasia au kutumia mabavu katika kuuondosha au kuubadilisha uongozi uliopo. Na katika nchi inayojidai inajiendesha kidemokrasia hili la kwanza ndilo linalotumika. Sasa inapotokea kuwa kundi kubwa zaidi katika jamii ambalo ndilo kwa namna moja ama nyingine litaathirika na maamuzi yatakayofanywa na kundi dogo halitaki kutumia fursa yake katika kufanya maamuzi, hali hiyo si ya kufurahisha hata kidogo. Vijana wa Tanzania ambao ndo wazalishaji na wajenga nchi wakuu, wana kila sababu ya kuhitaji mabadiliko. Wana kila sababu ya kuhitaji maendeleo yanayoendana na umri wa nchi yetu, wana kila sababu ya kuhitaji hali bora kwa ajili yao na wazee wao pamoja na wadogo na watoto wao. Lakini kwa vile mabadiliko hayaji kwa kusubiri mwingine akae kukufanyia maamuzi, ni jukumu letu vijana kuhakikisha tunashiriki katika kuleta mabadiliko haya, ama kwa kupigiwa au kwa kupiga kura. Vijana tunapolalamika kuwa kiongozi fulani hafai kwa sababu hafanyi hivi au hivi au tunataka hiki na hiki na yeye hakitimizi wakati hatukupiga kura kumkataa tutakuwa hatujitendei haki sisi wenyewe na wala hatuwatendei haki wenzetu. Kupewa nafasi uifanyie kazi halafu huifanyii, lolote baya likitokea basi nawe pia unahusika katika kutokea kwake na hivi huna haki ya kulalamika. Kwa hivi vijana, sisi ambao tunafanya kundi kubwa la jamii ya watanzania tutumie nafasi yetu tuliyonayo katika kupiga kura kuwakataa wagombea wote ambao tutaona hawafai na wale ambao wana uwezo wa uongozi tuchukue nafasi hii kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwa manufaa ya Taifa letu. Taifa linahitaji mawazo mapya, taifa linahitaji sura mpya, taifa linahitaji nguvu mpya. Lakini hivyo vyote vitatoka wapi kama sisi vijana tutakaa kuachia wengine watupigie kura na kutuchagulia watu walewale, wenye sura zilezile, wenye muono uleule, wenye mawazo yaleyale ya kichovu yasioendana na mabadiliko ya ulimwengu kwa sasa. Kijana fahamu kuwa usipopiga kura umeisaliti nafsi yako, umetusaliti vijana wenzako wenye kutaka mabadiliko ya maendeleo ya kwenda mbele (maana kuna mabadiliko ya mendeleo ya kurudi nyuma pia), umewasaliti wadogo zako wanaokutegemea na umewasaliti watoto wako ambao kesho watakuuliza mama au baba ulikuwa na nafasi ya kuleta mabadiliko kwa kupiga au kupigiwa kura lakini hukutimiza wajibu wako. Na hapo sijui utajitetea nini. Tanzania yenye mabadiliko inawezekana, acha kulalamika na kulalamikia viongozi wasiofaa, timiza wajibu wako, waondoe madarakani. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu tubariki vijana. Monsignor "Mtaka cha uvunguni, inua kitanda juu" Kama ningekuwa Waziri wa Afya... 05/14/2010
Tarehe 13 Mei 2010 niliandika ujumbe kwenye kundi pepe la "Porojo Club" alias "PiCii Family" na haya ndiyo niliyoyasema (imefanyiwa uhakiki kidogo). Kama ningekuwa Waziri wa Afya, nakuapieni leo mbeye yenu na mbele ya Mwenyezi Mungu, ningetoa kozi ya mafunzo maalumu kwa watu maalumu hata ikibidi Mimi kama Waziri kusimamia utenenezwaji na kisha utumiaji wa DDT katika kaya ili kuua mbu. Katika dunia hii huwezi kufanya kazi na hao mabwana wa upebari na ukomunisti ukitarajia wao wana malengo mazuri ya kukuokoa kwa asilimia mia moja. Hivi hamuoni kuwa kwa kuua malaria watakosa soko kubwa sana la dawa na mahali pa kufanyia majaribio ili wapate fedha na utajiri zaidi? Umewahi kuona nchi yoyote iliyoendelea kwa kusikiliza Wamagharibi au Wamashariki kwa yale wanayotuambia tufanye au tusifanye? Siku zote tunajua kuwa ili kupata maendeleo na kufanya kitu cha maana, lazima watu watofautiane, wakosane na hata ikibidi damu imwagike na wengine wafe ili kufikia maamuzi mtu anayoyaona sahihi. Leo hii tunajisifia tulipata uhuru bila kumwaga damu lakini ni uongo mtupu, walikufa mababu zetu, tusipende kudanganyana kwa kuwa ni watu wachache basi tusiwape thamani ya uhai wao waliopoteza, hawakuwa wajinga, na hao waliokufa ndiyo waliochagiza wale waliodai uhuru wetu. Sasa basi nimetoa mfano huo kusema, ingekuwa mimi ni Waziri, basi lawama zote ningezibeba juu yangu lakini DDT ningeisimamia itumike kwa uangalifu ili kuzuia watu kufa na malaria. Watu wangenilaumu sasa na pengine miaka michache ijayo lakini baada ya kuisha malaria wangenikumbuka na kuniweka kwenye kuta zao kama Waziri aliyetoa uhai wake na kukubali kejeli na kifo kwa ajili ya kuokoa wengi. Ningekuwa mpumbavu na mkaidi kwa sasa lakini potelea mbali wanifananishe na madikteta wengine, mimi ninachojua nitakuwa nimeokoa Taifa langu kama wao (Wamagharibi) walivyookoa mataifa yao ndipo wakazuia matumizi ya DDT. Ikumbukwe kuwa matumizi ya DDT hayakatazwi,ila kiasi na aina ya utumiaji wa DDT. Sisi hatuendi kuitumia kwenye mashamba ya chakula, hata kiasi kidogo kitakachotoka majumbani kwa upepo hadi mashambani hakitoshi kudhuru binadamu. Ikumbukwe kuwa mimi ninayeandika nimezaliwa na kukua katika eneo tulilokuwa tunatumia DDT katika kahawa. Wazee walionitangulia hakuwahi hata mmoja kusumbuliwa kwa magonjwa yoyote ya figo au kibofu cha mkojo. Wao walifariki tu kwa uzee au ajali au kisukari nk, na kamwe si matatizo ya figo na kibofu cha mkojo. Mimi nimechunguza afya yangu na sina tatizo lolote la figo au kibofu. Ikiwa malaria inaua mtu mmoja kila baada ya nusu dakika, je si sawa tutumie DDT ambayo itaua watu wachache kwa matatizo wanayoyaita ya figo na kibofu cha mkojo (pengine kutokuua kabisa)? Ndiyo DDT itaua, lakini Malaria inaua zaidi. Tuna wasomi, na akili zetu zinafanya kazi kama wasomi kweli wenye uchungu na wananchi wenzao? Kweli wasomi hawawezi kutumia kiasi kinachokubalika na Shirika la Afya duniani (WHO) kwa uangalifu hadi tusimamiwe na Wamagharibi katika kufanikisha jambo lolote linaloihusu nchi yetu, hasa hili la malaria? Ukowapi ujasiri wetu? Kwani ni lazima watu wote wakubaliane ili jambo litendeke? mbona inahitaji watu wachache tu wenye ujasiri ili kuweza kubadili mwelekeo mzima? Yailai toba, tupoje? Kama ni kufa mbona watu wanakufa tu? sasa tuogope nini kutengwa? Watutenge lakini hatuna malaria! Hiyo siyo bora? Madhara ya malaria ni makubwa. Kwa uchache, ukiumwa malaria huhudhurii kazini, kwa maana hiyo ufanisi unapungua na kipato kinashuka. Mwanafunzi akikosa masomo shauri ya malaria, anahitaji nguvu mara mbili kuweza kuwafikia wenzie kufidia siku alizokosa vipindi, matokeo yake si kufaulu kwa kiwango cha juu. Mkulima akiugua malaria anakosa kwenda shambani na hivyo mazao yanakosa uangalizi unaotakiwa, matokeo yake ni mazao duni au kidogo. Fundi seremala, ushoni, viatu, makenika, msanii, mchezaji, mwanahabari nk wakiugua, maeneo yao ya kazi yanazorota na hivyo kuzorotesha wengine waliomtegemea. Wachilia mbali watu wanaofariki kwa malaria na hivyo kubidi kuwazika, ni muda na gharama vimekwenda na maji zaidi sana, tumezika nguvu kazi. Tufike mahali tuyaone haya kwa ukubwa na jinsi inavyoathiri Taifa. I am sick and tired of all this. Tunahitaji Kim, Mugabe na Ahmedinejad wetu katika hili. Basi mimi ningekuwa Waziri, walahi ningeutoa rehani uhai wangu na ningefurahi kufa au kuachishwa kazi kwa matumizi ya DDT. Hawatanielewa sasa lakini watakuja nielewa baadaye au vizazi vyao vitajanielewa na watanishukuru kwa hilo, that's how great people go down in history - doing the greater good for the majority, giving their lives for others - that's a definition of a hero on my perspective. Huo ndiyo msimamo wangu kama ningekuwa Waziri wa Afya - kama Ninge - Nami si Waziri wa Afya. Laiti ningekuwa. Laiti ningekuwa. Ninge, ninge, ninge... Subi. PS: Nimesema ninajua wapo watakaonipinga, ni sawa, ni uhuru wao, kadiri ile ile niliyotumia uhuru wangu kuyaandika haya. Huu msimamo wangu, sijaubadili tangu mwaka 2007 na wala sina nia ya kufanya hivyo. 10 hand signs that you need to be aware of 05/11/2010
Click on a picture and read at the bottom, a description of the corresponding hand gesture. List made possible courtesy of www.intac.net I Wish My Dad Was Alive 05/10/2010
I woke up one day, I was very young, I heard my dad speaking “today I had a dream that in this country people are going to live together as a single society sharing their wealth as either farmer’s in the villages or business in the cities, sharing their income reducing the gap of haves and have not”. Moreover that day he called our family, it was an extended family plus other’s relatives and said it is time for those who have, to tell us where they got and share with us all, and for those who don’t have at all, there is enough land to cultivate thus will be given enough support. Furthermore my father was capable of correcting the wrong, he was not scared, he can just pop in and say I know there is a problem he will intervene and solve it without complains. He didn’t entertain rumors. Whenever he discovers there are some treasures within the family compound, he says preserve it, it might be of good use later and benefit the grand children, he was thinking of the future and he knew who will be the best to succeed him when his time passes or when he passes away, I mean who will lead the family. My father had his own approach, where he listened everybody and weighed how to help and support without discouraging. Thus the family lived a unified life happily together although we had only a radio but it was ok. As time went on, he grew very old, he had to pass the head of the house to my elder brother, who was wise, quiet and had his own approach of solving problems, he was not that strict but improved the family, the business group prospered more than the farmers and he managed to add the TV in the house. At that time one family member wanted to live alone on his own and thought it would be a good idea, he was serious, and this forced Dad to intervene things shacked but his presence made a change and things went back to normal. His time also elapsed and passed it to my other brother, he came back to be strict and changed the rules, he decided to invest and use treasures, soon after the death of Dad, it proved some success in terms of employment but cant talk much about it, he allowed some neighbors to do business with the family members, even the family bank was given for the far neighbors to run, but he did his best and his approach improved the family wellbeing, and improved its income, causing the other families to appreciate. Sincerely during dad’s time people were sincere and obedient with a lot of respect to him. The time came for my last but one brother was, during his milestone every family member was expecting much from him, they loved him, he was their chosen one, I can’t say much, but he began his journey of heading the family well, he promoted farmers and decided to give them support. The challenges come when he has problems with the family members, especially on the issue which is very sensitive to the family; I can say he is aggressive, short tempered and doesn’t forgive. Surprisingly this brother of mine he has his own interest were even if there is a family member is allocated to solve it, he will intervene, but in those sensitive issues he will be quiet and considerate but when the responsible family member fails to intervene or solve, depending on how the information goes, he will react sincerely with aggression and even me his young brother could feel the heat is on, but the problem of my brother the opposite of my father, he doesn’t go into details of the report which is given either due tiredness he doesn’t like to read much but he will receive the briefing from the responsible family member so if this person slips or changes the theme, I mean mislead, it isn’t easy to extinguish the fire, That’s why I wish my dad was alive, he knew him well, he could have assisted him, and he was not troubled with family problems at all, he was more willing to assist even if u don’t ask him to. The problem’s comes after dad passed away some few potential people in my family for butter bread to the neighbors, will they think of coming back to my family? And for those who are still in the family are we happy? WRITTEN AND COMPOSED BY THE MASCOT – Dr.Henry |