wavuti
 
Picha ya Mlima Kilimanjaro iliyopigwa tarehe 4 Mei 2008 kama inavyoonekana katika tovuti ya Boston - BigPicture katika kusanyo lenye kichwa cha habari "Scenes from Kenya" (bofya hapa kutizama picha zote 40).
Picture
Fresh snow covered Mount Kilimanjaro seen at sunrise from Ambuseli game reserve in Kenya, May 04, 2008. (MLADEN ANTONOV/AFP/Getty Images)
 
 
Mgeni Rasmi na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UV-CCM Taifa, Ridhiwani Kikwete, amewasimika Makamanda mbalimbali wa UVCCM ikiwa ni pamoja na kamanda wa Vijana CCM kata ya Kijitonyama kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika shule ya msingi Kijitonyama jioni ya tarehe 10 Machi 2010.
 
 
Picture
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Makamu na Kaimu Rais wa Nigeria, Dk. Goodluck Jonathan kwenye hoteli ya Transcorp Hilton jijini Abuja anakohudhuria Mkutano wa Viongozi wakuu kuhusu maendeleo ya biashara na viwanda vya kilimo barani Afrika. Alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano huo.
Picha kwa hisani ya Mroki Mroki
 
 
Honda CRV. Model 2000. Automatic. 4 cylinder. Color: Metalic Golden. Imetembea mileage 47000 tu.
Bei ni maelewano kupitia +255784524148 na/au +255715524148
Bofya picha zifuatazo kuzikuza kwa muonekano mzuri zaidi
 
 
Picha kwa hisani ya blogu ya Jide aka Lady Jay Dee. Bofya picha kuzikuza kwa muonekano mzuri kidogo.
 
 
Picha kwa hisani ya PwaniRaha.com
 
 
Picture
Mroki Mroki aka Father Kidevu anaomba 'caption' ya picha hii...
 
 
Kwa wale ambao hawakuiona video hii na wanatamani kujua yaliyojiri, basi video inapatikana katika ukurasa wa video, au bofya hapa. Pia, DVD zinapatikana kwa kuwasiliana na wahusika kwa namba zifuatazo (+44) {07957632385} au (+44) {07595485727} au kwa njia ya email: ebrahim628@hotmail.com
Picture
 
 
Picture
mmoja wa walioathirika baada ya kutumia maji yaliyotiririka toka migodi
Picha zinazoonekana hapa ni mali ya blogu ya Kijijini Kwetu ya Chacha o'Wambura (Ng'wanambiti) na zimewekwa hapa ili kusambaza habari hii kwa watu kwa matumaini kuwa yupo mwenye roho ya ubinadamu walao mmoja atakayesikia na mwenye uwezo wa kufanya jambo la haki au kufikisha suala hili kwa anayeweza kulishughulikia. Masuala kama haya yatatufababisha siku moja tudaiane haki na amani kwa ncha ya upanga, na hiyo si kauli yangu binafsi bali nukuu ya wenye hekima waliotutangulia, mwenye akili na afahamu.

Ng'wanambiti anasema:
Cha kushangaza ni kuwa kuchukuwa hatua kwa swala hili kumekuwa kukichukua muda mrefu sana. Tunachosikia ni majibu ambayo ni ya kiutawala ambayo Barrick, DC wa Tarime, RC Mara, NEMC, Wizara ya Mazingira, Wizara ya Afya na Wizara ya Madini wanayatoa ni sawa kuwa 'wenyeji wameiba lining za mabwawa ya kuhifadhia maji machafu'. Je na hawa ambao wako katika vijiji vilivyo mbali na mgodi ambao ndo wamedhurika kwa kiasi kikubwa ni wezi?

Ndo kusema kuwa wataalamu wetu wa afya kuanzia Mkemia Mkuu wamewaasi wananchi walowasomesha kwa jasho la kodi zao na kuungana na wawekezaji kwa kisingizio cha 'attracting foreign direct investment? FDI kwa gharama za wananchi wetu? Je kuna mkono wa mtu (kisiasa na kampuni)ama ni kutojali kwa viongozi wetu?

 
Simba 3 JKT 1 03/06/2010
 
Ilikuwa  ni dakika mbili za mwisho za kipindi cha pili zilizoipa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania, Simba SC ushindi wa magoli 3 - 1 dhidi ya timu ya JKT Ruvu.

Simba inahitaji pointi mbili tu ili iweze kutangaza ubingwa wa kabumbu Tanzania Bara katika msimu wa Vodavom Premier League 2010/2011. Ikiwa Simba itafanikisha hilo, hii itakuwa historia mpya kwani tangu kuanza kwa ligi hiyo, Simba haijawahi kupoteza mchezo hata mmoja isipokuwa kutoshana nguvu katika michezo miwili tu ilipocheza na timu ya Kagera Sugar ya na African Lyon.
 
Magoli ya Simba yalifungwa na Mussa Hassan Mgosi 2 (moja kila kipindi) na Uhuru Selemani. Goli la JTK Ruvu lilipatikana kipindi cha kwanza kwa njia ya penati.

Photo credit: PwaniRaha.comIssaMichuzi blog na Full Shangwe blog.