Picha na maelezo kutoka kwenye blogu ya blogu ya Nyakasagani Add Comment Wafungwa nchini Kyrgzstan wajishona midomo 27/01/2012
Wafungwa wapatao 1300 nchini Kyrgyzstan wameshona midomo yao, huku wengine 700 wakiendelea na mgomo wa chakula ikiwa ni hatua ya kupinga hali mbaya na dhuluma wanazofanyiwa wakiwa gerezani. Maofisa wa Kyrgyz wanasema kuwa wafungwa hao waliamua kushona midomo yao baada ya wakuu wa magereza kuwalazimisha kula ili kuvunja mgomo wa kutokula waliouanza tangu Januari 17, 2012. Kitendo cha kuwalazimisha kula kilisababisha ghasia baina ya wafungwa na askari ambapo inaripotiwa mfungwa mmoja alifariki dunia na wengine kujeruhiwa kiasi cha kupelekwa hospitali kwa matibabu. Kyrgyzstan ilijipatia uhuru wake mwaka 1991 kutoka kwa Muungano wa nchi za Kisovieti uliovunjika. Inaripotiwa pia kuwa hali katika magereza ya nchi hiyo ya Bara la Asia ya Kati ni mbaya. Wafanyabiashara wawili mtu na mkewe, wamepigwa risasi na kumwagiwa tindikali huko Zanzibar kwa kuuza pombe. Katika uvamizi huo uliofanyika Jumatano iliyopita mwanamke Bimal Alvind (36) alinusurika kupoteza ujauzito wake wa miezi minne baada ya kupigwa risasi ya tumbo na kumwagiwa tindikali. Risasi hiyo ilitolewa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili bila kuathiri ujauzito huo lakini tindikali hiyo ilimjeruhi mwilini kuanzia usoni, kifuani kwenye matiti, mikono yote miwili na tumboni. Mumewe, Alvind Asawla (42) alipigwa risasi kichwani kwenye paji la uso katikati ya macho iliyotokea nyuma chini ya shingo na sasa amepooza upande mmoja. Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwa ndugu yake Upanga wiki hii, Asawla alisema walivamiwa Jumatano iliyopita saa 10:30 jioni katika Mtaa wa Hurumzi Mji Mkongwe. Alisema wakati wakivamiwa, yeye na mkewe aliyeishi naye kwa miaka 17 sasa na kujaliwa watoto wawili; Priyanka (14) na Nidh (12), walikuwa wakitoka katika biashara yao wakirudi nyumbani eneo la Kiponda. Alisema ghafla watu wawili walimvamia mkewe na kummwagia tindikali na yeye alipokuwa akijaribu kumsaidia, watu hao walimmwagia tindikali usoni. Kwa mujibu wa Asawla, wakati wakitaharuki kwa hali hiyo, ghafla alitokea mtu mwingine na kumpiga risasi katika paji la uso akadondoka chini huku damu zikimtoka. Alisema alijaribu kujikongoja kwa nia ya kuendelea kumsaidia mkewe lakini mtu huyo wa tatu alimpiga risasi ya pili mgongoni na mkewe akapigwa risasi ya tumbo. Asawla alisema baada ya hapo hakujua kinachoendelea mpaka alipozinduka Kituo cha Polisi cha Malindi walipopatiwa PF3 na kupelekwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja walipopigwa picha za x-ray na kugundulika wana risasi mwilini. Baada ya kipimo hicho, Asawla alisema hospitali hiyo haikuwa na vifaa vya kutoa risasi hizo, ndipo ndugu zake waliwasaidia usiku huo na kuwasafirisha kwa ndege hadi Dar es Salaam ambapo walikimbizwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Alisema mkewe alilazwa katika wadi ya Kibasila namba tatu na yeye akahamishiwa katika Hospitali ya TMJ kwa ajili ya kipimo cha CT-Scan ambacho hakikupatikana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Kwa mujibu wa Asawla, mke wake alitolewa risasi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na yeye kufanyiwa upasuaji wa kumtoa risasi ulifanyika katika Hospitali ya TMJ. Alisema anamshukuru Mungu kwa kuwa ni mzima hadi sasa kwani alipigwa risasi sehemu mbaya na kukaa nayo kwa saa zaidi ya 12 ndipo ilipotolewa kichwani jambo lililowashangaza hata baadhi ya wauguzi. “Nimepooza upande mmoja wa kichwa changu, sihisi jambo lolote lakini madaktari wameniambia nitarudi katika hali yangu ya kawaida polepole baada ya kufanya mazoezi,” alisema. Alisema aliambiwa kuwa risasi hizo hazikupita katika mishipa mikubwa ndiyo maana yuko hai hadi sasa na mshipa mdogo uliomwaga damu, umefanya jicho la upande uliopooza kuwa jekundu licha ya kuona vizuri. Mfanyabiashara huyo alisema kuwa watu hao wamempa ulemavu wa kudumu bila kutegemea huku akiamini siyo majambazi ingawa walichukua pochi ya mkewe iliyokuwa na fedha kidogo. Alisema hospitalini wameambiwa tindikali waliyomwagiwa ni aina ya asidi sulfuriki (sulphuric acid) inayotumika katika magari. “Unajua mwizi anataka fedha na siyo kumwagia tindikali au kukupiga risasi na sisi hatukuwa na silaha yoyote; nia ya watu hawa ni kutuua kwani tumekuwa tukipata vitisho vya mara kwa mara kutokana na biashara yetu ya kuuza pombe Zanzibar,” alidai. Alidai mara kwa mara wamekuwa wakipata vitisho ikiwemo kukuta karatasi inayomtaka kuacha biashara hiyo vinginevyo utauawa; na wamekuwa wakitoa taarifa katika vituo vya Polisi vilivyopo karibu na biashara zao. Alilalamika kuwa licha ya wafanyabiashara wengi wa pombe kufanyiwa vitendo vya kumwagiwa tindikali, kupiwa risasi na hata kuchomwa moto, hakuna aliyewahi kukamatwa na kuchukuliwa hatua. “Sisi tunafanya biashara na mahoteli makubwa ya kitalii na tunalipa kodi zote stahiki, Serikali iseme wazi kama haitaki biashara hii Zanzibar au wawadhibiti watu hawa,” alisema. Alidai kuwa matukio kama hayo ni ya muda mrefu na mwaka 2007 wakati wa Jumatatu ya Pasaka, baba yake mzazi, Ahandillal Asawla aliyekuwa akifanya biashara hiyo alimwagiwa tindikali usoni akafariki dunia. “Hata baba yangu aliuawa lakini hakuna hata mtu aliyekamatwa na Serikali haikufanya jambo lolote, sasa umefika wakati Serikali itulinde tunaofanya biashara hii au itangaze kusitisha kwa manufaa yetu,” alisema Asawla. Alisema cha kushangaza tangu ukoloni babu zake waliuza pombe kwa amani lakini sasa wanatumia pombe kama sababu za kisiasa ili kuangusha uchumi wa Zanzibar. Gazeti hili liliwasiliana na uongozi wa Polisi katika Mkoa wa Mjini Magharibi bila mafanikio. Kwanza Kamanda wa Polisi Mjini Magharibi, ACP Azizi Mohamed simu yake iliita bila majibu na simu ya Kamisha wa Polisi Zanzibar, CP Musa Musa haikupatikana pia. Baadaye gazeti hili lilifanikiwa kumpata Ofisa Uhusiano Polisi Zanzibar, Asha Mzule lakini alisema kuwa ni mgonjwa kwa muda kidogo hivyo hajui kinachoendelea na kutoa namba ya simu ya OCD wa Wilaya ya Mji Mpya. Hata hivyo OCD huyo alikataa kuzungumzia uvamizi huo wala kutaja jina lake lakini akashauri atafutwe ACP Azizi ambaye alidai yuko Uwanja wa Ndege akimsubiri Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein anayetokea nje ya nchi. Namba ya ACP Azizi ilipopigwa kwa mara ya pili, haikupatikana kabisa. -- Picha via blogu ya Lukwangule, habari via HabariLeo Viongozi hawa wenye nyadhifa tafauti nchini Tanzania wamekuwa wakitamkwa katika vyombo mbalimbali vya habari kwa namna tofauti kiasi cha kuuaminisha umma wa Watanzania kuwa wana tofauti zilizozaa makundi ndani na nje ya chama. Naam, picha hii kama wasemavyo wahenga, ni moja ila yaweza kuwa na maneno elfu! Aabiria aliyefahamika kwa jina moja la Amina mkazi wa wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya alikufa papo hapo katika ajali iliyotokea juzi usiku katika Kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani kutokea Mbeya baada ya basi la New Force kuparamia ukuta wa mgahawa uliopo mkabala na Ofisi za Mabasi ya Kampuni hilo. Tukio hilo limetokea majira ya saa 5:00 usiku wa Ijumaa ya Januari 20 mwaka huu katika Kituo hicho cha Mabasi yakitokea mikoa mingine. Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kondakta wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Januari Kapinga aliingia ndani ya basi hilo lenye namba za usajili T 853 AVQ aina ya Yutong lililokuwa likitokea Dar es Salaam baada ya abiria wote kushuka ndipo alipolikurupua kwa nguvu na kumshinda hatimaye kuparamia ukuta. Abiria aliyefariki alikuwa safarini kuelekea masomoni mkoani Tabora na wakati gari likiparamia ukuta wa mgahawa huo alikuwa akipata chakula cha jioni. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, mtu mmoja alifariki na watu watano kujeruhiwa. Aidha kondakta wa basi hilo alitoroka na kwenda kusikojulikana na juhudi za Jeshi la Polisi kumtafuta zinaendelea. Dereva wa basi hilo anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi. Noah Mwakatumbula, Mwenyekiti wa Kituo cha Mabasi mkoani Mbeya yaendayo mikoani amewataka madereva waliopewa dhamana ya kuendesha vyombo hivyo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waache mara moja tabia ya kuacha funguo za vyombo vyao vya usafi. -- taarifa via blogu ya Mbeya Yetu Kumbukumbu za Martin Luther King Jr 22/01/2012
Juu ni gari lililohifadhiwa katika jumba la makumbusho ya Mchungaji mpigania haki, usawa na uhuru nchini Marekani, Martin Luther King Jr. Gari hilo la kukokotwa na farasi ndilo lililoubeba mwili wa marehemu Martin Luther King Jr. kwa ajili ya maziko kufuatia kupigwa risasi na kuuawa. Picha ya chini ilipigwa siku ya maziko ya Mch. Martin Luther King Jr. Picha zote zimepigwa na "Dewo" alipozuru jumba hilo lililopo Atlanta, Georgia, Marekani (Januari 2012). Kwa mengi zaidi kuhusu Martin Luther King Jr, fungua tovuti iliyotengenezwa mahsusi kwa ajili yake: thekingcenter.org Jioni yaleo, Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa pamoja na viongozi na wajumbe wengine wa CHADEMA wamekutana Ikulu kwa mwendelezo wa mazungumzo ya mchakato wa muundo wa kupatikana kwa Katiba Mpya ya Tanzania. Baadhi ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Freeman Mbowe, Tundu Lissu, John Mnyika, Said Arfi, John Mrema, Profesa Mwesiga Baregu na Profesa Abdallah Safari. Katika mkutano wa awali ambapo Rais alikutana na baadhi ya viongozi wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa hakuhudhuria. Zifuatazo ni picha za Ikulu za mkutano wa leo. (Picha za mkutano uliotanguli aunaweza kuziona kwa kubofya hapa). Mkutano huo ulihitimishwa saa tano na robo usiku! Huko Ikulu leo, Rais Jakaya Kikwete amekutana na uongozi wa chama cha NCCR-Mageuzi kufuatia ombi la kutaka kuonana naye ili kuwasilisha mapendekezo ya chama hicho kuhusu mchakato wa jinsi ya kuipata Katiba Mpya ya Tanzania. Zifuatazo ni picha toka Ikulu za mkutano huo. Rais Kiwete leo Jumamosi, Januari 21, 2012 ameongoza mamia ya viongozi na wakazi wa Dar es Salaam waliofika katika viwanja vya Karimjee kwenye hafla ya kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mbunge wa Arumeru, marehemu Jeremiah Sumari. Zifuatazo ni chache ya picha za zilizopichwa na Mpiga picha wa Ikulu (na nyingine toka blogu ya Richard Mwaikenda.) | Vitabu vya WatanzaniaBofya picha ya kitabu unachokitaka ili ujinunulie nakala
Yaliyomo/CategoriesAll Hifadhi/ArchivesFebruary 2012 |











RSS Feed