Tunayo kila sababu ya kutoa pongezi nyingi sana kwa Hasheem Thabeet kwa kutia juhudi na kufuata maelekezo na kufanikiwa kurejea kwenye ligi ya mpira wa kikapu ya Marekani (NBA). ![]() Hasheem Thabeet Hatimaye timu ya Memphis Grizzlies imemrejesha dimbani Hasheem Thabeet ambaye ni nyota wa Tanzania katika mchezo wa mpira wa kikapu, NBA, wa nchini Marekani. Hasheem anarejea baada ya kuichezea timu ya Dakota kwa takriban wiki mbili katika ligi ya kujinoa al maaruf D-League. Habari zaidi za kwa nini alikwenda D-League unaweza kuzirejea kwa kubofya hapa. "I was on the bench for a long time, I got to go out there and play big minutes, try to work on the stuff the coaches wanted me to do - rebound the ball, block shots, and be able to score when you get the ball. To stay active overall. I was successful doing that" - alisema Hasheem wakati akielezea sababu ya yeye kuweko benchi muda mrefu na kutokuichezea Grizzlies michezo mitatu kati ya mitano kabla ya kupelekwa Dakota. Hivyo basi, lengo kuu la Hasheem kupelekwa D-League ilikuwa ni kwa ajili ya kumpa changamoto, stamina na kujiamini zaidi ili aweze kukabiliana vilivyo katika michuano ya NBA. "They gave me a reason why I was going up there..., so it wasn't as tough as a lot of people were expecting. They explained to me why I was going there, and I was OK with it." Akiwa na Dakota WIzards, aliichezea mechi sita na kufanikiwa kufikisha pointi nyingi zaidi (19 ) siku ya Februari 28 na tarehe 5 Machi 2010 alifanikiwa kupata rebounds 18 na hivyo kuiwezesha Wizards kupata ushindi wa mechi 5-1 katika uwepo wake. "He went down and played well," Memphis coach Lionel Hollins said. "He was a huge factor for them. The one game he fouled out, they lost in the end. They're not 5-1, if he's not blocking shots and rebounding the way he was, and even scoring." Hii inadhihirisha kuwa kijana anaweza ikiwa anadhamiria. ![]() Timu ya Yanga (Obren amevalia fulana ya njano, kaptula nyeusi na soksi nyeupe) Mlinda mlango wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga, bwana Obren Circovic ameshaichezea Yanga kwa takriban miaka miwili sasa. Katika mazungumzo yake na kitengo cha michezo cha shirika la utangazaji habari la Uingereza (BBC Sports), kipa huyo mwenye asili ya Serbia anakubali kuwa vipo vitendo vya kishirikina katika soka ya Tanzania. Kwa mara kadhaa sasa tumekuwa tukisikia habari za hapa na pale kuhusiana na matumizi ya 'ndumba' na vitendo vya uchawi pamoja na ushirikina. Tumeyasikia haya katika nyumba za ibada mf. kanisa la TAG Mikocheni, pia tumesikia yanayotokea kwa watu wenye ulemavu wa ngozi, yaani albino, tumesikia pia kilichotokea katika hospitali ya Taifa Muhimbili pale kijana alipokutwa na kichwa cha mtoto mdogo na kuelezea mazingira alikokipatia na alikokuwa akielekea, tumesikia vile vile katika Bunge la Jamhuri ya Muungano pale baadhi ya watu walipokutwa wakinyunyiza unga fulani kwenye viti vya wabunge, tusisahau kile cha walokole vs mganga kilichotokea Tabata na hivi majuzi tumesikia tena kile kisa cha mfanyakazi wa ndani aliyerejeshwa kwao Morogoro na wiki iliyofuatia tukasikia habari za 'kutunga' za kisa cha mtu kutoa msaada kisha mikono kuota mnyoya, na visa kadha wa kadha ambavyo havijagonga vichwa vya habari lakini vinasimuliwa mitaani. Jambo hili angalabu si jipya katika nyanja za michezo kwani mara nyingi sana tumesikia habari za wachezaji wa timu kubwa kubwa na maarufu kama Simba au Yanga wakihusishwa na matumizi ya 'ndumba' katika kutaka kupata ushindi hasa pale wanapokutana. Mara timu imetia kambi Bagamoyo kwa 'mafunzo maalumu' au kwenda Zanzibara kwa ajili ya 'kujiandaa' kupambana na watani wao. Akizungumza na BBC, pamoja na mazuri mengi ya kusikia soka la Tanzania hasa akilinganisha na lile la Serbia, kipa Obren anasema, "That witchcraft wasn't mine, it was for some of the other players from Tanzania,"... "I have heard of that [witchcraft] but I don't believe in it, I've had contact with it, but I don't believe in that." Anaongeza kusema kuwa, amejitahidi kuzungumza na wachezaji hao kuhusiana na 'ndumba' lakini wao humsikiliza, wakaitika kwa midomo yao lakini vitendo vyao haviendani na kauli zao, "I've spoken to them but all of them are saying one thing and doing another,"... "They say 'we don't believe in that' but tomorrow I see them putting some bottles or something like that [in my goal]." Angalizo aliloliona Obren kwa soka la Tanzania na maoni yake ikiwa tunataka kufikia kiwango cha Ulaya ni kuwa, "The problem here is behaviour, behaviour here are not at a high level; they must change how they play on the pitch, how they play in training,"... "Behaviour, lifestyle they must change, because your performance depends on behaviour, you must improve yourself." Kwa habari kamili, bofya linki ifuatayo: news.bbc.co.uk/sport2/hi/football/africa/8534075.stm Simba 3 JKT 1 03/06/2010
Ilikuwa ni dakika mbili za mwisho za kipindi cha pili zilizoipa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania, Simba SC ushindi wa magoli 3 - 1 dhidi ya timu ya JKT Ruvu. Simba inahitaji pointi mbili tu ili iweze kutangaza ubingwa wa kabumbu Tanzania Bara katika msimu wa Vodavom Premier League 2010/2011. Ikiwa Simba itafanikisha hilo, hii itakuwa historia mpya kwani tangu kuanza kwa ligi hiyo, Simba haijawahi kupoteza mchezo hata mmoja isipokuwa kutoshana nguvu katika michezo miwili tu ilipocheza na timu ya Kagera Sugar ya na African Lyon. Magoli ya Simba yalifungwa na Mussa Hassan Mgosi 2 (moja kila kipindi) na Uhuru Selemani. Goli la JTK Ruvu lilipatikana kipindi cha kwanza kwa njia ya penati. Photo credit: PwaniRaha.com, IssaMichuzi blog na Full Shangwe blog. ![]() Hasheem Thabeet Habari zilizoandikwa hivi karibuni mtandaoni kumhusu Mtanzania mwenzetu, kijana Hasheem Thabiti ambaye ni Mtanzania wa kwanza kucheza mchezo wa kulipwa wa mpira wa mikono katika ligi ya nchini Marekani maafuru kama NBA, si za kufurahisha. Hasheem alinyakuliwa katika naasi ya pili 'Pick Number 2' na timu ya Memphis Grizzlies kwa ajili ya msimu wa NBA 2010. Habari zilizoripotiwa na kuandikwa katika mtandao wa Yahoo! na mitandao mingine zinasema kuwa Hasheem ameshushwa kutoka NBA na kupelekwa katika ligi ya D (Developmental League) ambapo mchezaji anayeshindwa kufikia viwango na malengo katika NBA hutakiwa kwenda kwa muda ili kujinoa zaidi. Kitakwimu, katika michezo yote 50 aliyocheza Thabeet msimu huu, ameweza kupata wastani wa pointi 2.5 tu ndani ya kila dakika dakika 10.3 za mchezo. Tayari amepoteza nafasi yake katika timu ya Grizzlies kwa Hamed Haddadi, kiungo wa kati aliyeichezea timu hiyo kwa miaka miwili sasa. Wakala wake, Bill Duffy, alifanya juhudi za kumhamishia kwenye timu ya Dakota Wizards ambayo ni washirika wa Grizzlies katika D-Legue na kusema, "I think he needs to play". Kwa kucheza D-League, Hasheem anakuwa mchezaji wa kwanza kabisa kushuka toka NBA hadi D-Legue kati ya wote waliowahi kunyakuliwa katika nafasi za juu za NBA draft. Hasheem anatarajiwa kuingia kiwanjani wakati Dakota itakapopambana na Erie siku ya Ijumaa. YATOKANAYO Waswahili tuna usemi wetu kuwa, 'kuteleza si kuanguka'. Kwamba kijana Hasheem bado anayo nafasi ya kufanya vizuri na kuwa mchezaji bora kabisa ikiwa atapata ushauri na maelekezo mazuri. Safari ya Hasheem alikotoka na alikofikia si ya lele mama hasa pale utakapoilinganisha na mamilioni ya watu, si tu wanaotoka nje ya Marekani, bali hata waliopo nchini Marekani kwenyewe. Historia ya Hasheem ya nyumbani Tanzania ambako mchezo wa mpira wa kikapu si nzuri kama ilivyo mchezo wa soka, anayo kila sababu ya kuangalia hatua na mafanikio aliyoyafikia. Kwa kuzingatia umri wake (16 Februari 1987), Hasheem bado anayo fursa ya kujinoa, kukata tamaa ni mwiko. Mara zote tunapoanguka au kupatwa na shida, yatupasa kuangalia chanzo cha tatizo, kisha tutafute mbinu sahihi za kulitatua na tena liwe somo ili tupate kujifunza kutokulirudia tena kosa. Binafsi nimejitahadharisha, 'usifurahie kujikwaa kwa mwenzio' ama 'usicheke ukunga na uzazi ungalipo'. Nimepitia magumu mengi, matatizo makubwa, na machungu tele, na bado mapambano yanaendelea, hivyo ninaelewa ilivyo mtu unapopatwa na hisia za uchungu na pengine aibu. Lakini huu si wakati wa kufikiria hayo, huu ni wakati wa kujua kuwa kadiri ya ukubwa wa jina lako, ndivyo utakavyokuwa ukubwa wa mlio wa mguno wako. Kijana jipe moyo mkuu, nyanyuka, simama imara, piga kifua mbele, safari na iendelee. Nasemaje, 'make it your STEPPING stone and not a STOPPING stone' - Subi, 25.02.2010. Yapo matumaini baada ya kujiuliza mara kadhaa ikiwa kweli sekta ya utalii inayapa kipaumbele mashindano ya kombe la mpira wa miguu litakalofanyika Afrika Kusini hapo mwezi Juni mwaka huu. Video iliyotengenezwa na Akon iligusa zaidi nyoyo zetu katika suala la utalii kama tulivyouliza kwenye posti iliyopita (bofya kuisoma). ![]() Hatimaye mwandishi Apolinari Tairo anairipotia eTN kuwa: ...in kicking off the campaign, the Tanzania Tourist Board (TTB) has organized and invited 28 travel and tourism executives from leading South African tourist companies to visit Tanzania’s key sites to assess the available tourist attractions and services being offered to the foreign visitors. During their stay in Tanzania, the South Africans took an educational tour in northern Tanzania’s tourist circuit including the Ngorongoro Crater, Serengeti, and Lake Manyara wildlife parks... Other than the wildlife parks, the delegation viewed Mount Kilimanjaro and visited Mazimbu and Dakawa areas in Morogoro region... ![]() Tanzanian and South African governments are negotiating the best options to make these two places tourist sites. ...the South African tourist executives vowed to promote tour packages to Tanzania during the World Cup event by encouraging sports fans and other stakeholders to visit Tanzania and experience its unique attractions including Zanzibar Island, Selous Game Reserve, Kilwa Ruins, and Kondoa Irangi, apart from northern wildlife parks. In order for this campaign to succeed, the Tanzania Tourist Board has teamed up with South African Airways (SAA), looking for more seats or added daily flights between Johannesburg and Tanzanian airports so as to ensure that every tourist from South Africa can fly to Tanzania. Habari kamili: www.eturbonews.com/14583/tanzania-campaigns-woo-world-cup-2010-tourists Ukitizama video ya wimbo wa mwanamuziki Akon wa Oh Africa alioutunga mahsusi kwa ajili ya kombe la Dunia la mpira wa miguu Afrika Kusini 2010, utaziona rangi za bendera ya Taifa la Tanzania. Zifuatazo hapa ni picha nilizokamata toka kwenye video hiyo ambayo unaweza kuisikiliza kwenye ukurasa wa videos (bofya hapa) au kusikiliza audio kwenye ukurasa wa audios (bofya hapa). Ni katika kutizama wimbo huo nimejiuliza ikiwa wahusika wa Utalii Tanzania wanaweza kuipa kipaumbele (promotion) video hii ili kujipatia sifa ya kuitangaza nchi kwa bendera inayoonekana humo. Isije ikawa tuna'omba Mungu' siku tu Akon ashukiwe na Malaika akurupuke atutungie tangazo atuletee aseme hili hapa kwa ajili yenu kuboresha utalii. Loh! kwa kupenda vya bwerere? huenda twashindwa bure. Nadhani ni fursa nzuri ya kutumia video hiyo yenye mahadhi ya Kiafrika kujipatia-ujiko (sifa) bure. Nataka kujiaminisha kuwa wapo wabunifu wa sekta ya utalii wanaoweza kuifanyia kazi hii na sidhani kama Akon atakataa ikiwa atatakwa ruhusa na ridhaa ya kutumia video hiyo. Tusiiwekee ukomo kwa kudhania kuwa haiwezekani, tujaribu kwa juhudi kwanza na tuache kupenda vya mreremko. Association of South African Travel Agents Recently SARS have randomly selected passengers and requested proof of purchase of the foreign exchange they are carrying. This refers more particularly to travellers cheques and forex and is not a new rule, rather one being enforced more rigidly now in terms of the Financial Intelligence Centre Act 2001. This proof would be a receipt of the transaction of the purchases. If the traveller has lost the proof of purchase or cannot find it, they must go back to where the forex was purchased and obtain a duplicate receipt. In the event that the traveller cannot prove that the forex in hand was purchased correctly, it will be confiscated and they will have 90 days in which to submit a claim. Some banks have included a declaration at the end of their invoice for the customer to sign, stating that they will retain all invoices for a period of 2 years and that they declare that they will travel within 60 days of the purchase date of the invoice. It also states that they will not purchase in excess of the travel allowance and that all unused forex will be returned within 30 days of return or if the trip is cancelled. South African Exchange Control requirements:
CEO – ASATA ENDS Prepared for TNW – ASATA Column P O Box 3062 Parklands 2121 Tel + 27 11 327 7803 Fax + 27 11 327 7827 Email general@asata.co.za Website www.asata.co.za Head Office Block C, Ground Floor, Rosebank Office Park 181 Jan Smuts Avenue Parktown North, Johannesburg, 2193 ASATA is a Non-Profit Organisation established in 1956 Member of the World Travel Agents Association Alliance Member of the Tourism Business Council of South Africa
Simba yageuza wembe upande wa pili 02/09/2010
Baada ya kuwekewa kauzibe huko nyanda za kanda ya ziwa Nyanza, hatimaye leo timu ya Simba Sports Club wamegeuza makali ya kiwembe upande wa pili na kuwanyoa Manyema Rangers FC mara mbili. Ilikuwa ni dakika ya 63 mchezaji wa simba Ulimboka Mwakingwe alipoiandikia Simba bao lake la kwanza. Bao la pili liliwekwa kimyani kwa njia ya penati kunako dakika ya 71 baada ya wachezaji wa Manyema kumfanyia 'ndivyo sivyo' mchezaji wa Simba Mussa Hassan 'Mgosi' katika eneo la hatari na hivyo kuzaa penati hiyo aliyoifunga mwenyewe 'Mgosi'. Mechi ilichezwa katika uwanja wa Uhuru. Hadi mwisho wa mechi ni Simba SC 2 Manyema Rangers FC 0. Simba yawafunza mpira Toto Afrika; nayo Misri yatwaa ubingwa Afrika; wakati ManU wainyoa Arsenal 01/31/2010
![]() Timu ya Simba Sports Club leo imefanikiwa kuendeleza dozi zake kwa kuifunga Toto Afrika katika uwanja wao wa nyumbani goli 2 kwa nunge. Hadi kipindi cha kwanza kinakwisha, timu zote zilikwenda mapumziko kwa suluhu ya kutokufungana. Kipindi cha pili dakika ya tano, Mussa Hassan 'Mgosi' alifungua darasa la magoli akifuatiwa na Ramadhani Chombo 'Redondo' aliyefunga kitabu cha magoli dakika nne baadaye. Hadi mwisho wa mtanange huo, Simba 2 Toto Afrika 0. Hongera Simba kwa kuondoa aibu ya mwaka jana kwa kufanya malipizi ya aina yake kwa mwaka huu! Na katika mechi zilizochezwa kwingineko duniani, Mshindi wa kombe la mpira wa miguu kwa Mataifa ya Afrika amekuwa Misri baada ya kuitandika Ghana bao moja ambalo lilifungwa dakika ya 85. Hivyo hadi mwisho wa mechi, Misri 1 Ghana 0. Nchi ya Misri inaweka rekodi ya kuwa nchi iliyonyakua kombe hilo mara nyingi zaidi kuliko nchi nyingine yoyote. Na kisha huko Uingereza matokeo ni Manchester United 3 Arsenal 1. Patrick Lusato of Tanzania won the Nagpur International Marathon, which was held on Sunday to mark the death anniversary of Mahatma Gandhi. Patrick crossed the finish line with a timing of 2:13:06 to win the title plus a prize money of Rupees 1.25 lakh in the Full Marathon. Oswald Kahanuzi of Tanzania, came in second with a timing of 2:13:07, winning a prize of Rupees 2.25 lakh. Benson Yator of Kenya clocked 2:13:54 to win the third spot and a prize money of Rupees 2 lakh. Helen Musyoka of Kenya won the Half Marathon for women, clocking 1:11:27 and winning Rupees 1.50 lakh in prize money. Restituta Kemi of Tanzania came in second (1:12:39, Rupees 1.25 lakh) and Dehninet Jara of Ethiopia third (1:13:00, Rupees 1 lakh). Nearly one lakh runners took part in the marathon in various events, which included the full marathon, half marathon, 12 kilometres for boys, 10 kilometres for girls, 5 kilometres for boys under 18, 3 kilometres for girls under 18, besides an event for wheelchairs. The 'Ahimsa Daud' (The Run for Non-Violence) attracted thousands of entries and saw enthusiastic participation from the residents of the second capital from all walks of life. The events were flagged off by former India cricketer Mohammed Azharuddin, Maharashtra ministers R R Patil, Anil Deshmukh and Suresh Shetty, besides Mayor Archana Dehankar. Bollywood stars Arshad Warsi and Vidya Balan were among the guests for the concluding and prize distribution ceremonies. Source: news.webindia123.com | |||