wavuti
wavuti logo Facebook icon Facebook icon Twitter icon Subscribe RSS
 
Picture
 
 
Nyumba inapangishwa iko maeneo ya Kijitonyama ina vyumba viwili kimoja ni self contained. Ina sebule, jiko car parking na choo cha nje. Bei ni Sh. 250,000/- Kama unahitaji wasiliana na Amani 0715154070
 
 
Picture
 
 
Kampuni ya RJ inatafuta wasanii wa Kike na wa Kiume wenye umri wa kuanzia miaka 14 hadi 18.

Yeyote mwenye nia anatakiwakufika katika ofisi za RJ Company zilizopo Sinza Mori, Dar Es Salaam
Siku ni Jumatatu, 30 Agosti 2010 kuanzia saa 6 mchana hadi saa 10:30 jioni.
 
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUJITOKEZA KWA UKIUKWAJI MKUBWA WA MAADILI YA TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI KATIKA HABARI ZA UCHAGUZI MKUU
Kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu 2010 kimefika na vyombo vya habari vinalo jukumu kubwa la kuwapa Watanzania taarifa sahihi kuhusu mchakato huu muhimu wa kidemokrasia.

Baraza la Habari Tanzania (MCT) linapenda kuvipongeza vyombo vya habari kwa kazi nzuri ambayo vimekuwa vikifanya hata kabla ya kuanza rasmi kwa kampeni kwa kuchapisha na kutangaza habari ambazo zililenga kuwasaidia wananchi kushiriki katika uchaguzi huku wakiwa na uelewa wa wagombea na sera za vyama vyao.
Picture
Kajubi Mukajanga - Katibu Mtendaji/MCT
Pamoja na pongezi hizi, Baraza lingependa kutoa tahadhari kuhusu hali ya uvunjwaji wa maadili ambayo imeanza kujitokeza na kuelekea kuenea kwa kasi. Baraza `linatambua kuwa matatizo haya yanachangiwa na uelewa mdogo wa maadili, ushabiki wa kisiasa, lakini pia vitendo vya makusudi vya wagombea na vyama vyao vinavyolenga kuwarubuni waandishi na wahariri kukiuka kanuni za taaluma yao kwa makusudi.

Baraza linapenda kuwakumbusha wahariri na waandishi kwamba ushabiki wa vyama unaoingilia maadili ya taaluma haukubaliki kamwe. Wakati Baraza linafahamu na kuheshimu ukweli kuwa chombo cha habari kina uhuru wa kuunga mkono msimamo fulani wa kiitikadi au kisiasa, linapenda kukumbusha kuwa hiki si kisingizio cha kukiuka maadili ya kusema ukweli, kutoa haki ya mshutumiwa au mtuhumiwa kujibu, na kuzingatia uungwana katika uwasilishaji wa habari.

Baraza limefurahishwa na matamko ya vyama vya siasa kuwa vitaendesha kampeni za kistaarabu, zisizokuwa za kutukanana na kupakana matope. Hadi sasa, Baraza linaona kuwa vyama vilivyoingia kilingeni, kwa kiasi kikubwa vinajitahidi kutimiza ahadi hii.

Hata hivyo, kama msimamizi wa maadili ya wanataaluma ya habari, Baraza limeshtushwa na mwelekeo unaojitokeza unaoonyesha kwamba wakati wanasiasa wakionyesha kuendesha kampeni za kistaarabu majukwaani, baadhi ya vyombo vya habari vinaonekana kuendesha kampeni za maji taka kwa niaba ya wanasiasa.

Jambo hili halikubaliki, na ni aibu kubwa kwa taaluma hii adhimu. Katika kampeni hizi, waandishi na wahariri waepuke kujaribu kuwa Wakatoliki kuliko Papa mwenyewe, yaani kuwa na ukereketwa na ushabiki kuliko ule unaoonyeshwa na wagombea na vyama vyenyewe! Vyombo vya habari viepuke kufanya kazi chafu kwa niaba ya baadhi ya wanasiasa.

Baraza pia limezingatia kwa masikitiko mtindo unaochipuka wa wanahabari kuwa wakala wa vyama vya siasa wakati wakiwa kazini. Baraza linapenda kuwakumbusha wanahabari kuwa hawapashwi kushabikia rangi za vyama wawapo kazini, kuvaa mavazi yenye nembo, kauli mbiu au majina ya vyama na wagombea wa nafasi mbali mbali za uchaguzi.

Jambo hili linawadharaulisha wanataaluma, linajenga mashaka juu ya uadilifu wao. Jambo hili sio tu ni kinyume cha maadili, bali pia ni jambo la hatari, kwani linamweka mwandishi katika nafasi ya kuonekana wakala wa chama au mgombea, na hivyo kuweza kudhuriwa na wapinzani wa mgombea huyo.

Lakini pia, mwandishi akishajitambulisha kuwa anafanya kazi ya mgombea fulani, wagombea wengine na vyama vyao watawezaje kumwamini atakapokwenda kuandika habari zao?
Baraza linapenda kuchukua nafasi hii kuviambia vyama vya siasa bayana kuwa ni makosa kuwapa waandishi fulana, skafu, makoti, kanga, kofia, au vazi jingine lolote lililoandaliwa kwa minajili ya kampeni.

Baraza linawataka wahariri kuwaonya waandishi wao kuacha mara moja tabia hiyo. Kila mhariri makini ajiulize ikiwa kweli ana sababu ya kutumia habari inayoandikwa na mwandishi anayevaa nembo za chama katika kuandika habari za uchaguzi.

Kumeanza pia kujitokeza mtindo wa baadhi ya vyombo vya habari kutoripoti kabisa habari za baadhi ya vyama na wagombea. Baraza linapenda kuwakumbusha wenye vyombo vya habari na wahariri wao kuwa kibali cha kuendesha gazeti au kituo cha radio au runinga ni mali ya umma.

Leseni za vyombo vya habari hutolewa ili umma upewe taarifa; hili ndilo lengo la kwanza. Faida ya kifedha au mapenzi ya kisiasa sio sababu kuu inayofanya leseni ya chombo cha habari itolewe. Kwa hiyo wahariri wajitahidi kufanya kazi yao kwa uadilifu, na wamiliki wa vyombo wasiwashinikize kuacha kutangaza au kuandika habari muhimu katika kipindi hiki.

Baraza la Habari Tanzania litaendelea kufuatilia utendaji kazi wa vyombo vya habari katika kipindi hiki na kushauriana na wahariri, ili Watanzania watendewe haki. Wakati huo huo, Baraza lingependa kuwahimiza wale wote waliopatiwa raslimali kwa ajili ya shughuli ya ufuatiliaji vyombo vya habari katika kipindi hiki, kufanya hivyo na kuwapatia wahariri na wadau wengine ripoti za ufuatiliaji huo, ili wahariri waweze kufanya marekebisho ya udhaifu wowote unapotokea.

Tanzania yenye vyombo vya habari makini na vinavyowajibika kwa umma inawezekana.

Kajubi D. Mukajanga
Katibu Mtendaji
Agosti 27, 2010

 
 
Watu wawili wamethibitika kufa na wengine zaidi 60 kulazwa katika hospitali mbalimbali mjini Tarime mkoani Mara, baada ya kuugua ugonjwa wa kipindupindu. Habari ambazo hazijathibitishwa na wataalamu wa afya zinadai kwamba idadi ya watu waliokufa kutokana na ugonjwa huo mjini Tarime katika kipindi cha wiki moja iliyopita ni zaidi ya watano.
 
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Dk. Samson Charles, amewataja wakazi wa mjini Tarime waliokufa juzi baada ya kuugua ugonjwa huo kuwa ni Mzee Msabi (zaidi ya miaka 50) na Magesa Rozana aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Nkende.
 
Amesema baadhi ya wagonjwa wameshatibiwa na kuruhusiwa na kwamba waliokuwa wanaendelea kulazwa katika wodi maalumu hospitaini hapo kufikia jana ni 23 wakiwemo wanawake 18 na watoto wawili.
 
Mkuu wa shule ya Sekondari ya Nkende, Mwalimu Michael Ng’wanang’walu, amesema hadi jana wataalamu wa afya walikuwa hawajafika shuleni hapo kuweka dawa ya kutibu maji ya visima kama walivyofanya katika maeneo mengine.
 
Kwa upande wake, Mkuu wa shule ya sekondari ya Tarime, Mwalimu Mutta Jeremiah, amesema shule hiyo ilifungwa Agosti 21, mwaka huu, baada ya wanafunzi tisa kuugua ugonjwa huo na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya kabla ya kuruhusiwa siku tatu baadaye.
 
Naye Mkuu wa Chuo cha Ualimu Tarime, Mkufunzi Lucas Samuel, amesema wakufunzi na wafanyakazi wengine wameanza kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo baada ya wanachuo wawili kuugua na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya.
 
Changamoto kubwa inayokabili wataalamu wa afya na wakazi wa mji wa Tarime kwa sasa ni namna ya kudhibiti vitendo vya kufua nguo za wagonjwa wa kipindupindu katika mito ya Bomani na Msati, hali inayoweza kueneza zaidi ugonjwa huo.
 
Wakati huo huo, baadhi ya ndugu na jamaa wa wagonjwa wa kipindupindu wamelalamikia vitendo vya kunyimwa na kuuziwa dripu za maji kwa ajili ya wagonjwa wao waliolazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime, ambapo Dk. Charles ameahidi kufutilia tuhuma hizo ili wahusika wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria.  Hata hivyo, Dk. Charles amesema ofisi yake imenunua maji ya kutosha tofauti na mwanzoni ambapo kulikuwa na upungufu wa dripu za maji hospitalini hapo na hivyo kushindwa kumudu mahitaji ya dripu 24 za maji kwa kila mgonjwa wa kipundupindu.

credit:
Christopher Gamaina/Radio Free Africa
 
 
Call for music film / Wito kwa filamu za muziki / Appel aux Films

Sauti za Busara is East Africa’s No 1 music festival. Every year during February, Stone Town Zanzibar comes alive in celebration of African music.

New for the 2011 festival is the African Music Film programme. Throughout five nights the Old Fort’s amphitheatre becomes a cinema space under the stars where music films will be screened, complementing more than forty live music shows on the main stage next door.

We are looking for a variety of stimulating and entertaining music films from the African Continent and diaspora. These may be full length features, recorded concerts, documentaries, music clips and videos or more experimental films. We’re looking primarily for:
  • Films telling a story of music and musicians from the African Continent and diaspora
  • Music films that are of exceptional interest to the festival audience (regional and international)
  • Music films that represent the wealth and diversity of music from East Africa and beyond
  • Films with great visuals, quality sound and music that is firmly rooted in Africa
  • Films that tell of new and unheard of sounds as well as established artists
  • Foreign language films should ideally be subtitled in Kiswahili and/or English
Deadline for applications: 31st October 2010

More info and application form at www.busaramusic.org/callforfilm

Busara Promotions, PO Box 3635, Zanzibar, Tanzania

Tel: +255 773 822 294

www.busaramusic.org

Looking forwards >>> 8th Sauti za Busara music festival, 9 - 13 February 2011
 
 
Picture
 
 
Picture
 
 
Binti Sarah anapenda kufahamisha wapenzi wote wa iliyokuwa blogu ya angaliabongo.co.tz kuwa amehama na sasa ina ujio wa mwonekano mpya na jina jipya la angalia-bongo www.angalia-bongo.com

Wote mwakaribishwa kumtembelea na kuchangia taarifa, habari na maoni katika anwani hiyo mpya!
Picture