Mheshimiwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, George Mkuchika ametoa tamko Bungeni lenye faraja kwa wanazuoni na wadau wa lugha ya Kiswahili akiungwa mkono na Mheshimiwa Spika wa Bunge. Kwa ujumla mheshimiwa Waziri na Spika wa Bunge kwa pamoja wameonyesha umuhimu wa Serikali na asasi zake kudumisha utamaduni wa kutumia lugha ya Kiswahili katika fomu na shughuli zote rasmi pamoja na mawasiliano yote ya Kiserikali. Wakati hayo yakiendelea, ni muhimu Wanazuoni na wadau wote wa lugha ya Kiswahili tuungane na Serikali katika kuondokana na dhana la kuwekeza kwenye maendeleo ya lugha za kigeni. Asasi za maendeleo ya lugha ya Kiswahili ziongeze uhamasishaji wa matumizi ya lugha ya Kiswahili katika maeneo yote muhimu yaliyotajwa na mheshimiwa waziri na media zote ziachane na kabisa na matumizi ya 'KISWANGEREZA' katika utendaji wao wa kila siku. Wenu kwa staha; Ray Ephraim Ndewingiya Njau Mdau na mtetezi wa Kiswahili Dar es Salaam, Tanzania. 2 Comments Maisha ya binadamu ya kuhama haka toka eneo moja hadi jingine ni ya tangu karne na vizazi hata vizazi. Angalabu watu wamekuwa wakihama ili kukidhi haja za kimaisha hasa pale walipo panapokosekana namna ya kutimiza mahitaji hayo ama kunapokuwa na usumbufu mkubwa, kama vile siasa chafu, uongozi mbovu, hali ya hewa isiyostahimilika, machafuko katika jamii, nk, yanayosababisha ugumu katika kukimu uhitaji na kufikia malengo mengineyo. Mipaka ya kijiografia, sheria za nchi na makubaliano baina ya mataifa juu ya rushusa na pasi na vibali vya kusafiria kuvuka mpaka mmoja kwenda kwingien imekuwa vimekuwa vizuizi vya safari nyingi ambazo zingeweza kufanyika kiholela. Najaribu kuifikiria dunia isiyo na vizuizi, taswira bado hainijii... Nimewaza hivi kufuatia kuziona picha zilizopigwa na mwandishi Francis Godwin na kubandikwa kwenye blogu yake zikionesha baadhi ya raia wanaosadikiwa kuwa wanatoka nchini Ethiopia na Somalia, punde walipokamatwa katika msako na askari polisi kwa kosa la kuwepo nchini Tanzania bila vibali maalum. MATUKIO KADHAA YA HABARI KATIKA PICHA 19/04/2010
Maelezo ya picha ya kwanza: Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika bwana Steven Wassira (aliyesimama akishikilia kijitabu) akichambua Mswada Sheria ya Madini wa mwaka 2010 ambao kwa mujibu wa ratiba ya mkutano wa 19 wa Bunge unatarajiwa kuwasilishwa bungeni. “Nchi inapata nini na wananchi watapata nini?... Je haiwezekani kuwawezesha watu maskini, wawekezaji wa ndani?” Aliuliza Waziri Wassira ambaye alisema kwamba ni kuwawezesha wawekezaji wa ndani ni muhimu huku akitoa mfano wa Sweden ambayo alisema uchumi wake unaotegemea madini kwa kuwezesha wachimbaji wake wadogo wazawa. Maelezo ya picha ya pili: Waziri Mkuu bwana Mizengo Pinda (aliyeketi kwenye kiti kilichotandikwa kitambaa cheupe) na Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa (kulia) wakisafiri katika behewa la daraja la tatu kutoka stesheni ya Mpwapwa hadi Godegode kwenye Reli Ya Kati wakati Waziri Mkuu alipokagua ukarabati wa reli hiyo tarehe 18 Aprili 2010. Mafuriko yaliharibu vibaya reli hiyo na ukarabati wake unaendelea huku ukitarajiwa kukamilika katikati ya mwezi Mei ili kuruhusu kuanza tena kwa safari za kawaida za treni ya njia hiyo. Photo credits: Beda Msimbe - Lukwangule Ent. UFISADI SIO KITU KIPYA - Godleader Shoo 19/04/2010
Watanzania wengi siku za karibuni tumeonekana tukishabikia sana swala la ufisadi, wengine wanafanyiana mzaha, wanasiasa wanatuhumiana, mashehe na wachungaji wanautumia kujenga hoja kwenye mawaidha na wanahubiri, mafisadi wanakimbiza mafisadi wenzao n.k. Binafsi nimejaribu kujiuliza huu ufisadi wa siku hizi umeanza lini? Una tofauti gani na ule wa zamani uliokuwa ukiitwa uhujumu uchumi, ulanguzi n.k. Ufisadi nina imani ni hulka au tabia ya mtu ambayo hakuzaliwa nayo, ila amejifunza akiwa anadhamiria au mfumo wa jamii iliyomlea umemlazimisha kujifunza ufisadi bila yeye mwenyewe kujua. Tabia hii wakati mwingine inamfanya yule anayetuhumiwa kutojiona yeye mwenyewe kuwa ni fisadi, bali anawaona wale wanaopambana nao ndio mafisadi. Hulka hii kwa namna moja au nyingine imelelewa na viongozi wetu, watendaji wa serikali, mifumo ya elimu, familia zetu ambao ni mafisadi bila kujijua au kwa kujijua. Ninasema bila kujijua kwani, shuleni wakati nasoma tulikuwa na miradi ya elimu ya kujitegemea mfano, bustani za mbogamboga, kilimo cha mahindi, n.k, waalimu waliokuwa walezi wa ufisadi waliweZa subiri mazao yakikomaa wanachuma mboga bila kulipa hela na kwenda kula na watoto wao, mwanafunzi aliyetoa jasho kwa kulima na kumwagilia mboga akibeba mbolea ya samadi toka nyumbani aambulii kitu, bali anayefaidi ni mwalimu wake aliyekuwa mnyapala. Kwa mantiki hiyo mwalimu huyu amefanikiwa kumfundisha mwanafunzi huyu kuwa hana haki na kile alichokifanyia kazi, kwa hiyo kesho atakuwa fisadi, Mungu asipoingilia kati. Katika familia, mama na watoto wanashiriki sana katika shughuli za kilimo na ufagaji, hadi mazao yanakomaa, siku ya siku baada ya kuvuna na kuweka stoo, baba anakuja chini ya kivuli cha mfumo dume(ufisadi) anachukua mazao yale na kuyapeleka sokoni na kuanza kuyatumia kwa anasa, ikiwezekana na vimada au hata kuoa mke wa pili, huku watoto waliozalisha anachokitumia wakibaki wanapiga miayo na mlo wa siku moja. Kwa upande wa wafugaji watoto wanashiriki kuchunga mifugo, wakina mama wakikata nyasi lakini mwisho wa siku baba anapeleka mifugo mnadani, na kwenda kutumbua maraha akiiacha familia ikiishi kwa mlo mmoja usohakika. Nakumbuka sana wakati wa msimu wa mavuno magonvi yaliongezeka sana katika familia, mama kapigwa, mara kapewa talaka n.k. Viongozi wa kiroho wanaposhindwa kusimamia kweli na kuwakumbatia watu wanaouasi uadilifu wazi wazi ni dalili kuwa hawa viongozi nao si waadilifu. Ni jambo la kawaida kusikia vurugu mbalimbali katikati ya waumini wa dini na madhehebu mbalimbali, ukichunguza kwa umakini sana sahemu kubwa ya mitafaruku hii inasababishwa na u-mimi au kujali maslahi binafsi zaidi kuliko kujali hali ya kondoo. Inapofika mahali pa kugunduana ndipo huunda makundi na hatimaye mitafaruku kutokea, kulinda maslahi au kupokonyana maslahi hayo. Hivi hawa viongozi wa kidini watajivua je lawama za kuwaandalia Watanzania waumini wasiowaadilifu? Nilitegemea siku moja tusikie waumini wa dini fulani chini ya uongozi wao wamemwita mwenzao anayetuhumiwa wakae naye wazungunze kuonesha namna gani anamfedhehesha Mwenyenzi Mungu na jamii ile wanayoshiriki pamoja kumwabudu Mungu. Kama taasisi hizi za kidini hazina zinachowezeza kufanya kuwaokoa watanzania toka kuwa na viongozi wasio waadilifu, basi wingi wa taasisi hizi zitakuwa zimejaa unafiki na ufisadi. Mwishoni mwa mwaka jana nilipokuwa ziarani Kanda ya Ziwa nilikutana na mzee mmoja maarufau wa chama, katika mazungunzo yetu nilimwuliza swali hili, “ ikiwa Rais wa kwanza wa Tanzania alikuwa mwalimu alishindwa je kuwafundisha wafuasi wake uaadilifu na hatimae wahitimu? Mbona wale wale waliokuwa vijana wa mwalimu na walioaminiwa na Mwalimu ndo wamekuwa mstari wa mbele kupingina na sera za mwalimu za uadilifu? Wanafunzi wake wa kisiasa walihitimu kweli? Yule baba alikaa kimya kwa muda kisha akaniambia “kuna tofauti kubwa kati ya wanafunzi wa darasani na wale wa kisiasa”. Kwa kuwa sikuridhika na majibu yake niliendelea kutafakari, Ufisadi umeanza enzi hizi za awamu ya pili, tatu na nne tu, awamu ya kwanza haikuwa na ufisadi? Nadhani nitakuwa sahihi nikisema ufisadi ulikuwepo, na ndiyo maana hayati Rashid M. Kawawa, Edward M. Sokoine, Mwl. Julius K. Nyerere na wengine wachache walionekana kuwa kioo, wakimaanisha kile walichokisema na wakisema kile walichokimaanisha. Hata kama leo tunasema walishindwa kuwaleta watanzania maisha bora, lakini yale waliyoyafanya yalikuwa na dhamira safi na yakiuadilifu. Kwa mantiki hiyo wakajichanganua miongoni mwa wengine wengi. Kwa mantiki hiyo ufisadi ulikuwepo ila kwa kujifichaficha na kwa unafiki mwingi. Ushahidi ni jinsi mashirika mengi ya umma yalivyofilisika kutokana na kukosekana kwa uadilifu kwa wale walithaminiwa na Watanzania kuyasimamia, hatma yake ikawa ni kufilisika kwa mashirika hayo. Waliokuwa watoto enzi hizo waliyaona hayo yote wakawa kimya kwani enzi hizo ilikuwa mwiko kuhoji, tofauti na hali ya sasa. Tatizo ninaloliona sasa ni mtu yeyote mwanye mali nyingi kudhaniwa kuwa fisadi bila hata kujiuliza kwanini? Mali hizi za halali au za kifisadi? Tumebaki kuhitana mafisadi mafisadi lakini bado hatuna suluhisho la tabia hii mbaya kwa Mwenyenzi Mungu na hata mwanadamu yeyote mwenye akili timamu na angalau chembe ndogo ya uadilifu. Hatari kubwa imekuja pale viongozi wa kiroho (mashehe na wachungaji) wameingizwa katika mkumbo huu wa tuhuma. Upande mmoja nilikubaliana na tuhuma juu ya upande huu wa viongozi wa dini, kwani binafsi niliamani ndio waliobaki pekee kusafisha mioyo miovu ya waumini wao, ili wawe waadilifu na wawatumikie watanzania kwa uadilifu, ila dalili inaonekana kama wameshindwa. Nisiendelee kuwa miongoni mwa watoa tuhuma, lakini tuangalie nini cha kufanya sasa. Pakuazia ni malezi ya watoto wetu kiroho na kiakili. Ni lazima tuangalie utaratibu mzima wa malezi ya watoto wetu ili wasiwe mafisadi, Kwa waalimu wao kiroho na kiakili kuishi uadilifu ili wanapowaelekeza watoto kuwa waadilifu wauone mfano kutoka walezi hawa. Ni lazima wauishi uadilifu, wauseme wazi wazi mbele ya watoto hawa n.k. Leo tukiwa na watoto waadilifu, kesho tutakuwa na vijana waadilifu, na keshokutwa tutakuwa na watu wa umri wa kati ambao ni waadilfu. Swali kubwa ni hili, tutatoa wapi waalimu wa kiroho na kiakili wenye kufundisha uadilifu kwa vitendo? Kama serikali ikishindwa tuanze nyumbani kwetu na kudhamiria wanetu wawe waadilifu, hata kama akikutana na mwalimu asiye mwadilifu, ajitahidi kumtambua na akwepe ushawishi wake wa kutokuwa fisadi. Nina amini kuwa wewe nawe unasuluhisho mbadala tushirikishane, ili kuona kama tunaweza kupambana na sumu hii ya kukosa uadilifu badala ya kupambana na watu walio matokeo ya tabia hizi. Tutafute mizizi ya ufisadi tuing’oe na tuiteketeze kasha tufute kumbukumbu ya historia yeke. Nawasilisha Godleader Shoo (anwani pepe imehifadhiwa) ![]() Tanzania leads the list of East African states that have lost billions of dollars to money laundering, tax evasion, government graft and other illegal operations, according to a report by a US-based financial watchdog group. The report “Illicit Financial Flows from Africa: Hidden Resources for Development,” by Global Financial Integrity, states that the country has lost $8.9 billion over the past four decades through the illicit means. Kenya lost $7.3 billion while Uganda lost $6.4 billion over the same period. The three East African countries thus lost a total of $22.6 billion, money that would be sufficient to wipe out their combined outstanding external debt while leaving several billion dollars available for fighting poverty and spurring economic growth. The study points out that the impact of these losses is felt most acutely by the poorest Africans. The illicit outflow of money also “drains hard currency reserves, heightens inflation, reduces tax collection, cancels investment and undermines free trade,” the study says. Tanzania is ranked 13th among the top 15 countries with cumulative illicit outflows after Angola, Republic of Congo, Cameroon, Côte d’Ivoire, Ethiopia, Gabon, Ghana, Madagascar, Mozambique, Nigeria, South Africa and Sudan. Zambia and Zimbabwe take the 14th and 15th positions respectively. Already, Global Financial Integrity has started collecting signatures to petition the G20 Transparency at the G20 summit this June. The organisation is looking for 100,000 signatures from all over the world to forward to Canadian Prime Minister Stephen Harper, the current president of the G20. “Our goal is to show him the names of 100,000 people from all over the world who support ending banking secrecy, increasing financial transparency, and finally attacking the root causes of poverty.” Read the rest of this (Tanzania to be ASHAMED of) report at TheEastAfrican... (click here) BLOGU YA IKULU MAWASILIANO Keero kero! 18/04/2010
Blogu ya Ikulu ya Tanzania vipi jamani? Kuna mtu anaweza kunifahamisha umbumbu wangu wa TEKNOHAMA?. Hivi blogu ya Ikulu ya Tanzania inaendeshajwe? Haina habari za kila siku?Hivi yote yanayotokea Tanzania, ziara za waziri mkuu hivi karibuni, mama Salma Kikwete, Rais Kikwete safari zake zote za mwezi mzima uliopita, risala zake, hotuba zake, angalau hayo tu yanashindikana kuwekwa kila siku? mawasilianoikulu.blogspot.com Hivi idara ya mawasiliano ya Ikulu hawalioni hili? Leo Jumapili 18.04.2010. Habari za mwisho kwenye blogu hiyo ni za Machi 18. Mwezi mzima umepita. Matukio mengi yamepita katika kipindi hicho, lakini hakuna hata picha wala nini. Tunaona picha kwenye blogu ya Michuzi, Mjengwa, Hakingowi, Mrocky, Wavuti na nyinginezo za watu binafsi. Ikulu ka! Basi wacha blogu, tovuti ya taifa la Tanzania, ndo´kichekesho! Manaake habari haziko katika mpangalio. Ziko shaghalabaghala! Angalieni wenyewe hapo: www.tanzania.go.tz Mbona tovuti za wizara mbali mbali habari zake ziko katika mpangilio? Hii ndio sura ya Tanzania nje ya nchi, lakini mwee?sisemi mengi. Hata tovuti ya Waziri Mkuu www.pmo.go.tz inapendeza iko katika mpangalio mzuri. Wenu Tausi Usi Ame Makame, Oslo (anwani pepe imehifadhiwa) YATOKANAYO wavuti.com inaunga mkono kilio cha Tausi na Watanzania wengine ambao tumekuwa tukipiga kelele kila leo, hasa Dk. Faustine ambaye ameandika mara kwa mara kuhusiana na kero hii lakini inaonekana kelele hizi ni sawa na za kupigia mbuzi gitaa. Watanzania tunapenda turinge kuwa nasi tupo katika karne ya Sayansi na Teknolojia katika TEKNOHAMA lakini tunashindwa kujivunia hata kuthubutu kuhadithia ati tuna mkondo wa mawasiliano ya uliofunguliwa rasmi na Raisi mwaka jana na sasa kuna ujio wa EASSy cable. Tafadhalini wahusika wa IT Serikalini tuondoleeni hili kwani sisi tupo tayari kuitangaza e-Tanzania. Kundi la majambazi yapatayo kumi na yasiyojulikana ambayo yaliivamia nyumba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF), Ramadhan Dau, na kupora kasha la fedha zenye thamani ya mamilioni lilifanikisha azma yao kwa kutoboa ukuta wa uzio wa nyumba hiyo. Tukio hilo lililothibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga, lilitokea kwenye nyumba hiyo iliyopo Kinondoni eneo la Ada Estate. Habari ambazo gazeti la MTANZANIA Jumapili imezipata kutoka eneo la tukio, zinasema lilitokea usiku wa manane ambapo majambazi hao waliingia baada ya kutoboa ukuta wa uzio na kisha kuwateka walinzi. Baada ya kufanikiwa kufanya hivyo, waliwalazimisha walinzi kutoa funguo za geti, wakalifungua na kuingiza gari lao ndani. Inadaiwa baada ya hapo walifungua milango ya nyumba na kuanza kupekua vyumbani hadi katika chumba cha Dau walikolikuta kasha hilo, waliloondoka nalo pamoja na nyaraka kadhaa zilizokuwamo. Wakati tukio hilo linatokea, Dau na familia yake hawakuwamo nyumbani humo. Majirani wanasema ndani ya nyumba kulikuwamo na kijana mmoja, ambaye alifungwa kamba na kuzibwa mdomo kwa plasta huku akilazimishwa kuonyesha zilipo fedha na nyaraka walizokuwa wakihitaji majambazi hao. Taarifa ya Kamanda Kalinga kuhusiana na tukio hilo inasema Polisi inawashikilia walinzi wawili kwa ajili ya upelelezi kamili. “Katika hali ya kawaida haiwezekani wawe na silaha halafu watu watoboe ukuta waingie ndani bila ya kudhibitiwa,” alisema Kamanda Kalinga. Aliwataja wanaoshikiliwa kuwa ni Deus Mtatilo (52) mkazi wa Kinondoni na Yusuph Bakari (56) mkazi wa Ubungo. Walinzi hao ni waajiriwa na NSSF. “Dau na familia yake hawakuwapo, walinzi walikutwa wamefungwa kamba…katika matukio ya uhalifu kama huu zinaweza kufanyika hadaa vilevile,” alisema. Picha kwa hisani ya blogu ya Sufiani Mafoto Habari hii imetoka katika gazeti la HabariLeo Kitendo cha Kenya kuongoza kampeni ya kupinga Tanzania isiuze meno ya tembo katika mkutano huko mjini Doha, Qatar kimewachefua wabunge wa Tanzania na wameionya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuwa makini na nchi hiyo na itambue kwamba Kenya si rafiki wa Tanzania. Wabunge hao pia wamesema adhabu pekee ya kuipa Kenya ni kwa Bunge kukataa kuridhia itifaki ya soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki ambalo linashabikiwa na Kenya ambayo inaamini kuwa itafaidika zaidi kuliko nchi zingine mwanachama wa jumuiya hiyo. Walitoa msimamo huo kwenye semina baada ya Waziri Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala kuwasilisha mada yake iliyolenga kueleza maudhui ya itifaki ya soko la pamoja la Afrika Mashariki. Itifaki hiyo itawasilishwa bungeni kesho. Katika mada yake, Dk. Kamala aliwaeleza Wabunge jinsi hatua za utekelezaji zitakavyoanza kutekelezwa mara Bunge litakaporidhia itafaki hiyo kesho. Lakini wabunge wengi waliochangia walisema soko la pamoja, Tanzania bado haijawa tayari na iwapo Bunge litaridhia watakaonufaika zaidi ni Kenya. Mbunge wa Masasi, Raynald Mrope (CCM) alisema suala la soko la pamoja linaonekana linaharakishwa, wakati Kenya ndio wanaoonekana watafaidika zaidi na akasisitiza kuwa Watanzania hawajawa tayari kwa sababu mbalimbali. “Hawa majirani zetu lazima waelewe kuwa ni lazima wawe jirani mwema, hivi karibuni ametukamata vibaya kule Doha wamekataa tusiuze pembe za ndovu zilizojaa kwetu. Huyu sio ndugu yetu, huyu tukimruhusu aje kufanya kazi kwetu haya mambo yatazidi... walichokifanya ni lazima wapate adhabu na ni kutokubali itifaki hii kama wanavyotaka wao,” alisema Mrope. Mbunge wa Shinyanga Mjini, Dk. Charles Mlingwa (CCM) alipendekeza Tanzania iwe ya mwisho kuridhia itifaki ya soko la pamoja. Alitoa pendekezo hilo kwa kile alichodai kuwa tabia ya nchi hiyo katika mikutano ya kimataifa imekuwa mstari wa mbele kupinga maombi ya Tanzania. Alisema kitendo cha Kenya kuamua kujenga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Taveta, lengo lao hasa ni kutaka kuua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Mbunge wa Njombe Magharibi, Yono Kevela (CCM) aliomba wabunge wakatae kuridhia itifaki hiyo kwa maelezo: “Tuachane na soko hili kwa sababu wananchi wetu bado hawajapewa elimu ya kutosha kwa nini tuhangaike nalo. Hii ni kuwatengenezea ulaji watu wa Kenya, hivyo sisi wawakilishi wa wananchi tusiingie kichwakichwa katika kusaini itifaki hii.” Mbunge wa Lulindi, Suleiman Kumchaya (CCM) alisema Tanzania haiwezi kuwa mgongo wa nchi nyingine kupandia kwenda kwingine. Alisema nchini Doha nchi za Afrika mashariki zingekuwa na kauli moja na hata kuna kitu Tanzania ilikosea Kenya isingesimama kwenye mkutano huo kulisema. Naye Mbunge wa Kahama, James Lembeli (CCM) alisema yeye alikuwapo Doha alishuhudia kwa macho yake namna jirani yetu Kenya analivyoiua Tanzania kwa sumu na akaonya kuwa Bunge linaweza kuridhia leo; lakini vijana hao wakawalaani hadi wanakwenda kaburini. Mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango (CCM) alitaka Tanzania iende pole pole na liletwe bungeni baada miaka mingine 10.“Iandikeni hii tarehe ya leo maana tutakuja kujutia, angalieni ya Doha namna Kenya walivyotufanyia.” Alitaka Tanzania ifanye sensa kujua Wakenya wanaofanya kazi nchini kwani wamejazana kwenye mahoteli ya kitalii ndipo itifaki hiyo iridhiwe. “Nina ushahidi kule kwenye mbuga za wanyama wamejaa wao, warudi kwao kabla ya sisi kufikiria kuridhia.” Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikiri kuwa ni kweli Wakenya wamejaa hapa nchini na akahoji “Kwa nini Watanzania hawaendi huko kwao? Alihoji na kuwataka Wabunge wawe wazi ili Kenya wapate ujumbe huo kwamba Tanzania imekasirika. Habari hii imeandikwa katika gazeti tando la HabariLeo Mmomonyoko wa maadili unaelekea kuiathiri jamii ambapo sasa baadhi ya viongozi wa dini wanazidi kuingia matatani kutokana na kushiriki katika vitendo vya ngono. Mchungaji wa kanisa la African Inland - (AIC) ambaye pia ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Chona, wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Pasia Dickson (36), ametuhumiwa kufumaniwa Jumatano akifanya mapenzi na mwanafunzi wa darasa la saba. Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Daudi Siasi amethibitisha tukio hilo akisema kwamba, mtuhumiwa ameshatiwa mbaroni na amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kubaka na kushambulia. Siku ya tukio mwalimu huyo alikwenda nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kufanya naye tendo la ndoa chumbani kwa mama wa mwanafunzi, ambaye wakati wa tukio hilo alikuwa amekwenda gulioni kununua mahitaji ya nyumbani. Naye Diwani wa Kata ya Chona iliyopo umbali wa kilomita zaidi ya 50 kutoka Kahama Mjini, Mabala Mlolwa amesimulia tukio akisema kwamba, alishiriki kwa kiasi kikubwa katika kuyaokoa maisha ya mchungaji huyo. “Ni tukio la kweli, na mimi nimeshiriki katika kumnusuru kwa sababu baada ya fumanizi alijiokoa kwa kumng’ata kaka wa binti na baadaye alitimua mbio akiwa mtupu hadi kwenye ghala la kuhifadhia nafaka katika nyumba ya jirani. “Wananchi wenye hasira walitaka kummaliza huko huko ghalani, nikawasihi wasubiri polisi na kweli baadaye polisi walikuja kumchukua, mimi ndiye niliyemchukulia nguo, na sasa wanamshikilia …” Mashuhuda wa tukio hilo wanaeleza kwamba, Mchungaji huyo alikuwa na uhusiano wa muda mrefu na mwanafunzi huyo. “Hata siku ya tukio, jamaa alikwenda akijua kabisa ratiba ya mama wa mwanafunzi, bila woga alikwenda na pikipiki akaiegesha nje naye kuzama ndani na hawara yake… Kaka mtu ndiye aliyeshitukia mchezo mchafu wa mchungaji, kwani alipofika nyumbani alishangaa kuona pikipiki nje, baada ya kuingia ndani alimkuta mchungaji huyo katika kitanda cha mama yao akiwa utupu wakifanya mapenzi na mdogo wake mwenye umri wa miaka 16... ndipo katika kukurupushana huku mchungaji akitaka kutoka akiwa utupu na kaka mtu akijitahidi kumzuia kutoka huku akipiga kelele, mchungaji aliamua kumng’ata kaka mtu na kukimbia, lakini hakufika mbali kwa sababu hakuwa na nguo,” alisema Mlolwa. Kesi ya Mchungaji Dickson inatarajiwa kuendelea Aprili 30, mwaka huu. MAZUNGUMZO BAADA YA HABARI Pumbaf kabisa! Jeshi la polisi Kamanda Dar es salaam kwa kushirikiana na kampuni ya simu za mkononi Tigo wameunda kikosi kazi kwa madhumuni ya kudhibiti wizi wa miundo mbinu kama vile betri za minara ya simu, vipuri vya majenereta na mafuta. ![]() Suleiman Kova - Kamanda wa Polisi Dar Kamanda wa Polisi kanda maalum ya polisi Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema wizi wa miundo mbinu wa mara kwa mara sasa umekithiri. Wezi wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za wizi kwa kujifanya wao ni watumishi wa kampuni hiyo na hatimaye kufanikiwa kuiba. Wizi huo umegharimu mamilioni ya fedha dhidi ya kampuni ya Tigo hivyo kuathiri mapato ya kampuni ya Tigo na nchi yetu. Ili kupata ufanisi wa operesheni hiyo, wananchi wameombwa kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kutuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) kwa namba 0715 123888, mtu yeyote atakayekuwa na taarifa atume ujumbe, ujumbe utakuwa ni bure hautakuwa na tozo lolote. Aidha, kampuni ya ulinzi ya Kiwango inayoshughulikia ulinzi wa minara itakuwa inatumia namba 0715 123444 kwa kupitia namba hizo utoaji taarifa utakaombatana na mafanikio utamfanya mtoaji taarifa kufanikiwa kupata donge nono lisilopungua shilingi milioni moja na kuendelea, hii ni kwa kutokana na uzito wa taarifa yenyewe. Pia wananchi wameonywa kutonunua betri za aina hiyo kwa matumizi yasiyokusudiwa kwani ni kinyume cha sheria na watakaofanya hivyo watashitakiwa mahakamani. Tayari kikosi kazi hicho kimefanikiwa kukamata betri 48 na watuhumiwa wawili wamekamatwa majina yao yamehifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi. story credit : Mroki Mroki | Vitabu vya WatanzaniaBofya picha ya kitabu unachokitaka ili ujinunulie nakala
Yaliyomo/CategoriesAll Hifadhi/ArchivesFebruary 2012 |

















RSS Feed