Majaribu vumilia, naona yashindikana, Hasira zinanijia, furaha yakosekana, Hebu sasa fikiria, hawa wana wa rabana, Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Waganga mwajitahidi, roho zetu kuziponya, Hata sikuu ya Iddi, waganga mwapatikana, Kumbe nanyi mna dhiki, mnashindia makana! (pumba za mahindi au mtama) Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Maisha haya magumu, nani asiyeyajua, Waganga mwawahukumu, vinono mnajilia, Wapeni hata chandimu, nadhani watachezea, (mpira wa makaratasi) Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Wadanganyika fukara, Temeke twategemea, Msifanye masihara, sisi tunaangamia, Amana zetu nyembamba, hazitoshi enda Indya, (mshiko) Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Waganga namalizia, kama kweli mna nia, Wekeni chini SILAHA, pasiwe wa kubakia, Gogoro mwalirefusha, kwa kuwa mnapingana, Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Haya kama hayafai, basi jaribuni hili, Wote rudini kazini, mpunguze makaburi, Mola wetu si bahiri, pepo mtaikabiri, Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? NA MGHANI WENU MZEE MTWANGAMBATE Dkt. Mtwangambate G.C; (M.D.) Add Comment Rais hakika naona aibu 04/02/2012
Nimepokea utenzi ufuatao kwenye email, simfahamu mtunzi, ila shukrani zote zimfikie. Rais hakika naona aibu, Sijui wewe una sababu, Umerudi uwe karibu, Huku madakitari wagoma. Rais umefika jana tu, Leo kutwa na viatu, Fungua benki ya watu, Huku madakitari wagoma. Rais nami umenchosha, Watu pia umewachosha, Sio siri hii inajionesha, Huku madakitari wagoma. Rais basi nenda Amana, Muhimbili napo umeona, Wagonjwa kila kona, Huku madakitari wagoma. Rais Bungeni Dodoma, Wanakula wao nyama, Muhimbili kumesimama, Huku madakitari wagoma. Rais hili tia makini, Sio za huku mijini, Hospitali za kijijini, Huku madakitari wagoma. Rais leo madakitari, Kesho pengine askari, Walimu nao wasubiri, Huku madakitari wagoma. Rais kemea hata hili, Achana na EPA na dili, Hayo sie tutasubili, Huku madakitari wagoma. Rais huko muhimbili, Wakudanganya ni shwali, Hakuna hata moja faili, Huku madakitari wagoma. Rais sema hata neno, Watanzania tuone upo, Kemea huyu we pepo, Huku madakitari wagoma. Naandika ushairi huu huku chozi linalengalenga, nilipita sehemu leo kuna mtu 1 alikuwa anaelezea ana mgonjwa Muhimbili mahututi anataabika toka mgomo uanza anakunywa pain killer. Rais amerudi ameishia enda kufungua FnB bank. Uwiiiii Mungu tusaidie sisi tusiojisaidia wenyewe pengine twaweza ona hata mwanga. Mungu ibariki Tanzania. Part of the following information was shared to me by a friend via the email. The world economy is going through major slowdown. Countries and currencies will be affected in many parts of the world, in Tanzania we have seen the Tanzanian Shilling moving from Tshs. 1,300 to the US Dollar to TShs. 1800 within six months. In Kenya, economic development has slowed down, so protect against risk, come together and support each other to grow together. Cut down unnecessary expenses in social fashion. It is not a time to live in an unreasonable spend thrift manner, invest in prudence, and plan for the future. We are still in recession, so be careful, don't use resources in an inappropriate way; you will need those resources to build your future. Don't spend more than you earn, buy only what is essential, save and conserve resources and don't live in a dissolute” KNOWLEDGE creating new technology is increasing. Right now there are gaps in knowledge in East Africa. This is creating opportunities in different industries. There are solid futures in emerging economies like Tanzania, new jobs using new technologies and knowledge will present us many opportunities. Investing in SELF is best investment but be selective in that so when you are done you are not outdated. In Tanzania we are faced with members who still do not understand the importance of insurances, be it for homes, businesses, or themselves. By that we mean life insurance and health insurance, we have members who insure their cars yet refuse to insure themselves. In both cases a loss or illness can mean great hardship to the whole family. Many families do not have wills written down. It causes so many issues after you are gone, for your families and businesses.
Yafuatayo ni maoni aliyoyatoa katika kundi la WanaMabadiliko kufuatia majadiliano mbalimbali yaliyoelekea kuuaminisha umma wa Watanzania kwamba upo uadui binafsi baina ya Rais Kikwete na Dkt. Slaa. Mwalimu, Dkt. Lwaitama anasema: Kwa uchambuzi wa kina HAKUNA ugomvi wala uhasama kati ya Ndugu Kikwete na Ndugu Slaa; kama binadamu HAKUNA KABISA. Wapambe wachache wa Mh Kikwete kama Rais ambayo ni taasisi wanajaribu kutengeneza hii taswira ya eti ugomvi na uhasama ili waweze kuhalalisha kuweza kumdhuru Ndugu Slaa vile wanahofia sana umaarufu wake unaozidi kufunika hicho wanachodhani ni umaarufu wa Ndugu Kikwete... Ni siasa uchwara kama alivyoziita Ndugu Rostam Aziz... Ni siasa ambazo hapo nyuma nchini Kenya zilizaa siasa za kuuliwa kiongozi yeyote aliyeonekana kuwa kipenzi cha wananchi zaidi ya Rais...ni siasa zilizozaa mauwaji ya Tom Mboya, JMKariuki, na Robert Ouko. Dr. Slaa alisimamishwa na Chadema kugombea Urais 2010 na kama wizi wa kura ulizuia ushindi wa Dkt. Slaa kuwa Rais bado hiyo si kisa kati ya Dkt. Slaa na Dkt. Kikwete... Hapana... hilo ni tatizo kati ya CCM na Chadema; kati ya CCM na Watanzania waliochoka ukiritimba wa utawala wa chama kimoja kwa nusu karne.... HICHO NI KISA KATI YA CCM NA WATANZANIA KILICHOIMBUA KASI YA KUDAI KATIBA MPYA NA TUME YA UCHANGUZI ILIYO HURU... SI SWALA BINAFSI KATI YA Dkt. SLAA NA Dkt. KIKWETE LAKUMALIZWA NA ETI KWA KUNYWA CHAI PAMOJA IKULU... Rais Kikwete asijiruhusu kushawishiwa kukubali dhana potofu kuwa eti Dkt. Slaa ni adui yake... Hakuna kitu kama hicho. Adui wa Dkt. Kikwete ni kupanda kwa bei ya sukari na kuongezeka kwa bei ya umeme; ni kuzidi kudorora kwa uchumi kwa ujumla; na mawazo ya Rais yaelekezwe kwenye adui hao na wala hana haja ya kukutana na Dkt. Slaa eti kuyamaliza.. Kumaliza yepi? Bei ya sukari, mchele, mafuta ya taa na umeme au? Tuachane na dhana hizi za kijinga za wanasiasa na wanausalama uchwara wanaojikomba kwa Mh Rais ili awapatie ulaji kwa kumwambia eti adui yake mkuu ni Dkt. Slaa vile eti Dkt. Slaa anakinyongo kushindwa kuwa Rais shauri ya wizi wa kura... Huo ni ujinga utokanao na kukataa kukubali ukweli ulio wazi kuwa mwaka 2010 Dkt. Slaa katu hakujipanga kwa mtandao wa miaka kumi wa kuusaka Urais ulioundwa na ndugu na marafiki (ambao hawakuwa wale waliokutana barabarani) na uliogharamiwa na pesa za wizi kama ule wa EPA ...Si hulka ya Dkt. Slaa na hana sababu ya kuyatafisiri matokeo tata ya uchaguzi wa 2010 kama mambo binafsi kati yake na ndugu yake Mtanzania mwenzake Dkt, Kikwete. Hoja hii ya eti Rais Kikwete amwalike Dkt. Slaa Ikulu wayamalize inatia kinyaa na kudhalilisha dhana nzima ya taasisi ya Urais. Mwl. Lwaitama Somo: Umuhimu na masharti ya kuandika Wosia 16/01/2012
UMUHIMU WA KUANDIKA WOSIA
Afisa Mtendaji Mkuu/Kabidhi Wasii Mkuu Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Mtaa wa Kipalapala, Kiwanja Na.516 Upanga S.L.P 9183 Dar es Salaam. Simu Namba +255 - 22 – 2153069 Nukushi +255-22-2153075 ---- Ikiwa ulipitwa na masomo ya awali, bofya hapa na hapa kuyarejea. NAKUAGAJE REGIA? 16/01/2012
Siku zote ninaamini katika sera za vizazi kufundana na kukabidhiana majukumu. Katika maisha ya kijamii ninaumizwa sana na kupotea kwa utamaduni wa wazazi kurithisha watoto wao masuala kama ufundi na hata majukumu ya kitamaduni kwenye mila na desturi zetu. Ndio maana hivi sasa kwenye vijiji vingi hapa nchini imekuwa nadra kupata mafundi Seremala wa kurithi ama Waashi pia. Kwenye Siasa Kizazi kinaposhindwa kuandaa kizazi kingine kuchukua jukumu la kuongoza kuna hatari kubwa ya Taifa kukosa viongozi walioandaliwa vema na hivyo kuongoza inavyopasa. Taifa huumia sana linapopoteza viongozi wanaoandaliwa kubeba majukumu mazito ya kitaifa. Dada Regia Estelatus Mtema, Mbunge wa Viti Maalumu, Waziri Kivuli wa Kazi na Ajira na Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA ni mmoja wa wanasiasa vijana waliokuwa wanafundwa kuchukua majukumu zaidi ya Taifa letu. Alikuwa anafundwa na Chama chake. Alikuwa anafundwa na Bunge (mafundo kutoka kwa vyama vyote na hasa Spika Anna Simamba Makinda). Alikuwa anafundwa na marafiki zake. Alikuwa anafundwa na Chama cha Walemavu Tanzania (CHAWATA). Alifundwa na Shirika la FES. Dada Regia alikuwa anafundika. Alikuwa ni Hazina kubwa kwa Taifa letu. Alikuwa na sifa za peke yake kabisa kulinganisha na wanasiasa wengine na hasa wanasiasa vijana. Nitaeleza. Sijui ni kwa nini mama yangu Bi Hajjat Shida Salum amekuwa sasa anapata habari kwanza kabla yangu (yeye ndiye aliyenipa habari za msiba wa Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga na Rafiki yangu kipenzi Shelembi). Nikiwa nimepumzika sebuleni, nyumbani kwetu Tabata Bi Shida ghafla ananiuliza, umeongea na dada yako? Ilikuwa kama saa sita mchana hivi, yeye kasimama upenoni mwa ukuta ananiangalia macho makali. Nikashtuka kidogo maana amekuwa mgonjwa mgonjwa toka amerejea toka Hijja miezi kadhaa iliyopita. Najua akiniuliza hivyo ana maanisha nani (Mhonga Said Ibrahim Ruhwanya), nikamjibu sijazungumza naye, kunani? Akaniambia piga simu makao makuu nasikia kuna Mbunge wetu wa Viti Maalumu amepata ajali. Mara moja nikashika simu kumpigia ndugu Msafiri Mtemelwa. Alichoniambia sikuamini. Eti kwamba Regia amepata ajali na amefariki muda mfupi uliopita. Nikamwita rafiki yangu Hatibu Mchange anayeishi jirani yetu kumwambia aje ili anisindikize makao makuu ya chama. Kisha nikamjulisha Bi Shida kuhusu msiba wa rafiki yake na mwanae Regia. Nikamwacha akilia sana. Sikumpa pole wala kumtaka asilie maana kwanza sikuamini kabisa kwamba ni kweli Regia ametutoka. Nikasema mpaka nikamwone mwenyewe kwa macho yangu. Siku nne kabla ya kifo chake Regia alikuja nyumbani kumsalimu mama yetu (Bi Shida siku zote alimwona Regia kama mwanaye na yeye Regia alimheshimu mama yangu kama mama yake mzazi kabisa). Wakati namsindikiza akaniambia, ‘naona umeshikia bango suala la ajira kwa vijana. Nakuunga mkono na unipe ‘data’ za kutosha ili kupitia Wizara yangu nilisukume suala hilo kwa nguvu zaidi’. Tukakubaliana. Tukakumbatiana na kuagana. Yeye alikuwa ameambatana na kulwa wake Remija. Kumbe ndio nilikuwa namuaga moja kwa moja dada yangu Regia Estelatus Mtema, mwanasiasa kijana asiye na woga na jasiri haswa. Hii ndio sifa yake kubwa kuliko wanasiasa wengi vijana. Ujasiri! Regia hakuwa mwanasiasa wa asili ama kurithi. Aliamua kuingia kwenye siasa kwa kwanza ushahiwishi wa ndugu David Kafulila ambaye walikutana huko kwenye Programu ya Mafunzo kwa vijana (YLTP) inayoendeshwa na Shirika la Friedrich Ebert Foundation (FES), mimi ni mwanzilishi wa Programu hii katika YLTP 1. David akiwa mwakilishi wa CHADEMA na Regia akiwa Mwakilishi wa CHAWATA katika YLTP 6. Regia alishawishika na kuingia CHADEMA, chama kikamweka kitengo cha Vijana kama Afisa. Wakati fulani kukatokea matatizo kati yake na Afisa mwenzake ndugu Ali Omar Chitanda kuhusu namna ya kufanya kazi. Regia akiwa na hoja kwamba chama kinajenga ushawishi kwa wasomi na hivyo vijana wasomi tu ndio waendeshe kitengo kile. Wakawa hawawezi kufanya kazi na mwenzake kabisa. Nikiwa Naibu Katibu Mkuu wa chama nikachukua maamuzi ya kumhamisha Regia na kumpeleka kuwa Afisa wa Mafunzo chini ya Kurugenzi ya Mafunzo na Oganaizesheni inayoongozwa na ndugu Benson Kigaila Masalamakali. Regia kwa ujasiri akaniandikia ujumbe mfupi wa simu ‘uamuzi wako sio sahihi’. Sikumjibu bali nikamwita Ofisini siku ya Pili yake. Nikamweleza namna ambavyo chama kinahitaji kada zote na kwamba wasomi wa vyuo vikuu waje kwenye chama wakijua pia kuna maafisa ambao si wasomi na wana mchango mkubwa katika harakati za kidemokrasia. Nikampa mifano ya namna mtu Kama Samora Machel alivyochaguliwa kiongozi wa FRELIMO ilhali kulikuwa na wasomi zaidi yake kama Joachim Chisano au hata mkewe Graca Machel. Regia alinielewa vizuri sana na mkutano ukaishia kutaniana kuhusu namna ya mitindo ya uongozi. Regia hakuficha kama hakupenda jambo na wala hakuwa anaangalia cheo cha mtu. Alisema anachokiamini na mengine yatabaki mjadala wa baadaye. Ujasiri wake wakati mwingine ulimletea shida kwa wakubwa zake lakini hakuna hata mmoja aliyetilia shaka mapenzi yake kwa chama chetu. Hakujali kuudhiwa na alikuwa tayari kukilinda chama muda wote. Huu ni mfano wa pili wa Ujasiri wake kisiasa. Wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi mwaka 2010 Regia alikwenda kugombea Ubunge katika Wilaya ya nyumbani kwao Kilombero. Watu wengi hawakumpa nafasi kubwa ya kushinda. Aliliandaa jimbo lake kwa mikutano ya mara kwa mara. Alishinda kura za maoni katika mchakato wa ndani ya chama. Katika kikao cha Kamati Kuu mmoja wa Wakurugenzi wa Chama akasema tunaye mgombea mwingine mzuri sana, Mwanasheria. Regia akaombwa kukaa pembeni. Akakubali. Kamati Kuu ikampitisha mtu ambaye hakwenda kwenye kura za maoni na wala hatukuwa tunamjua maana tuliambiwa na mtu tunayemwamini kwamba ni mgombea mzuri. Regia hakufurahishwa na uamuzi ule lakini kwa heshima na utiifu wa hali ya juu akakubali kutogombea. Siku za kurejesha fomu za kugombea zilipokuwa zinakwisha yule mgombea akatoa nje. Hakuonekana, kwa sababu mbalimbali ambazo sisi tuliokuwa mbali na Dar es Salaam na Morogoro hatuzijui. Chama hakikuwa na namna isipokuwa kurudi kwa Regia kumwomba aokoe jahazi. Regia hakusita. Akaendesha kampeni za uhakika akiwa hana mali wala jina kisiasa. Akaaminiwa na watu wa Kilombero. Akapata kura nyingi sana ambazo hata zilileta utata wa uhalali wa matokeo ya uchaguzi katika Jimbo lile. Ujasiri na nidhamu ya namna hii ni nadra sana kwa wanasiasa sio tu vijana hata waliobobea kwenye siasa. Huyu ndio Regia. Ndiye tunamsindikiza kwenye nyumba yake ya milele. Regia mwenye upendo wa dhati kwa watu aliowapenda. Regia aliyekuwa tayari kusaidia kwa hali na mali wenzake wanapohitaji msaada. Hii ni sifa yake ya nyingine ya kipekee. Mara baada ya Uchaguzi Mkuu na yeye kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Viti Maalumu, Spika alitugawa kwenye Kamati Wabunge wote. Kazi ya kwanza ya Kamati hizi ilikuwa ni kuchagua wenyeviti na makamu wao. Regia alijua mimi napenda kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma (uwekezaji umma). Hata hivyo alijua nina wakati mgumu sana kutokana na mazingira ya kisiasa yaliyokuwapo wakati ule kati ya Wabunge wa CCM na CHADEMA. Regia ni Mbunge pekee (ukiachana na wajumbe wa kamati ya POAC kutoka CHADEMA) aliyezunguka nami usiku kucha na kupiga simu kwa kila Mbunge mjumbe wa Kamati yangu kuniombea kura. Mbunge mwenzangu na Rafiki yangu wa karibu kutoka Ludewa Deo Filikunjombe atamkumbuka Regia kwa aina ya kampeni aliyopiga. Deo aliniambia kwamba alipokea simu ya mwanamke anaongea Kipangwa (moja ya Lugha ya watu wa Ludewa). Mwanamke yule mwenye sauti nyembamba na ya kutulia alikuwa anamwombea kura Zitto kuwa mwneyekiti wa POAC. Deo alifurahishwa na namna Regia alivyoweza kutumia lugha ya nyumbani kwao kuniombea kura. Hata tulipopata taarifa kwamba Kamati ya Wabunge wa CCM imeamua kwamba atakayepewa kura sio mimi, Regia alinitia moyo na kuendelea na kampeni. Asubuhi ya siku ya kura alimpitia kila mjumbe wa Kamati POAC aliyemwona na kumkumbusha kunipa kura hata kama CCM imewakataza. Nilimcheka sana Regia kwa kumwambia wewe sio mzoefu hapa. Hao wakishakaa ndio maamuzi hayo. Akaniambia hapana watabadilika. Ghafla Waziri Mkuu akatangaza kikao kingine cha Wabunge wa CCM na huko wakaelezwa kwamba kamchagueni Zitto. Ningekata tamaa bila kuendelea na juhudi usiku kucha kama nilivyoshauriwa na regia kwa kweli nisingeshinda nafasi ile. Regia alikuwa mtu wa kwanza kumjulisha matokeo ya uchaguzi nilipopata kura 13 kati ya 15 zilizopigwa. Huyu ndiye Regia ambaye alikuwa na uwezo wa kufanya kila mbinu ili mwenzake apate msaada. Ni lazima watu watoe machozi. Ni lazima Wabunge watoe machozi. Ni lazima wana CHADEMA wamlilie. Mimi sitawafuta machozi na nimekataa kulia. Kikao cha mwisho cha chama ambacho nilishiriki na Regia nilihudhuria kwa muda mfupi sana. Wenzangu watakumbuka mengine katika kila kikao kile. Mimi ninakumbuka moja tu ambalo ni moja ya sifa pekee aliyokuw anayo na wanayo wanasiasa wachache sana na hasa wanasiasa vijana (ambao hupenda zaidi siasa za kuridhisha kwa kusema watu wapendacho). Regia alikuwa na uwezo mkubwa wa kusema usichopenda kusikia. Alisema tu. Katika kikao kile wajumbe na Wabunge walikuwa katika ‘emotion’ sana kuhusiana na muswada wa mchakato wa kuandika Katiba. Mjadala ulikuwa mkali sana. Mwenyekiti wetu akampa nafasi Regia aseme. ‘mimi nashauri tuombe kuonana na Rais Kikwete’ yalikuwa ni maneno yake makali kupenya kwenye ngome za masikio ya wengi na yalipokelewa kwa mguno mkubwa. Mwenyekiti akaamrisha wajumbe na Wabunge watulie kwani Regia ana haki ya kutoa maoni yake. Mimi niliondoka baada ya muda mfupi maana nilikuwa ndio nimetoka nchini India kwa matibabu na nilikuwa na masharti ya kupumzika muda mrefu. Ushauri wa Regia (pamoja na wajumbe na viongozi wengine wa chama walioshauri ama waziwazi au kwa chinichini) ndio uliofuatwa na sasa kumekuwa na mazungumzo ya mara kwa mara ya viongozi kuhusu sheria ile ya mchakato wa kuandika Katiba. Huyu ndio dada Regia. Maisha mafupi lakini mafunzo makubwa katuachia vijana wenzake kwenye medani ya siasa. Nakuagaje Regia? Nilikataa kuamini kuwa umekufa. Nikasema mpaka nikuone. Nilipofika Tumbi, nikasema hujafa na wala siingii ‘motury’ kukuona. Sasa eti nakuandikia Tanzia . Kwa nini nikuage? Halafu nakuagaje REGIA? Ukikutana na Shelembi Magadula, mwambie kile kiti chake cha udiwani tulikitunza, akija atakikuta. Ukikutana na Chacha Wangwe Mwambie bado tunaendelea na harakati Nyamongo. Ukikutana na Amina mwambie asilie tena vijana wengi wameingia Bungeni na sasa wanaelekea Ikulu. Ukikutana na Bibi Titi mwambie sasa wanawake hata wanawake walemavu wanaweza bila hata kuwezeshwa, wanajiwezesha. Nakuagaje dada yangu mpenzi? Haya. Mungu atupe subira. Kabwe Zuberi Zitto, Mb DSM, 16 Januari 2012. Kamanda Umechanua na kunyauka. Pumzika kwa amani! “Tuache masihara, hakikisha unaninunulia ukiwa unarudi vitabu hivi; Balance Scorecard na Iron Lady cha Margeth Thatcher maana nimesikia upo nje ya bongo” aliniambia Regia, name nikamjibu “sawa. usijali nitakununulia”! Sikufahamu kuwa ndiyo yalikuwa mawasiliano yetu ya mwisho kati yangu na rafiki yangu Regia tuliyofanya tarehe 12.01.2012 na hata wala hatutoonana name kupata fursa ya kumpatia vitabu kama ombi lake. Kwangu ni kama ndoto. Ukishtuka isiwe kweli. Lakini si njozi. Tayari Regia amefunga kitabu cha maisha yake duniani angali katika umri moto wa ujana. Angali akiwa bado na mipango na mikakati mwingi kutelekeleza. Alikuwa rafiki yangu ambaye tulishazoea sana kiasi cha kutaniana na kuongea upuuzi upuuzi mwingi sana……maana hata binadamu wa namna gani kuna watu wake ambao anataniana nao na hata kuongea upuuzi upuuzi. Niandikapo tanzia hii kwa laptop nayo ni sehemu yenye kuongeza machungu na simanzi. Kwani nakumbuka aliniomba nimsaidie kupata laptop kwa kazi zake, nami nilikuwa nataka kubadili kompyuta. Hivyo nikamwakikishia nitaenda kumchagulia kompyuta nzuri ambayo ataipenda maana alishachoka kuzunguka madukani bila mafanikio hadi akafikiria kuagiza nje. Nilikwenda naye, na kumwonyesha kompyuta ambayo alipenda hivyo tukanunua pamoja aina moja ya kompyuta. Alikuwa mtu ambaye nilikuwa nimeshibana sana na nilifurahishwa sana nae mara kwa mara tulipokuwa tukikutana. Tulisoma pamoja kozi ya mwaka mzima ya uongozi ambayo ilizidi kutuweka karibu zaidi na zaidi. Mengi tukifundishana na kuelekezana. Kozi tuliyoifanya mwaka 2006/2007. Nakumbuka ni kipindi hicho na kuendelea ndipo alikuwa mstari wa mbele katika kazi za kisiasa kupitia chama cha Chadema. Mara kwa mara nilikuwa namwambia kuwa angalikuwa mbunge baada ya uchaguzi wa mwaka 2010. Jambo ambalo mara nyingi alikuwa akikwepa kulijadili kwa kina na kuyeyusha kwa mizaha na pale nikimsisitiza kuwa sikuwa katika mizaha aliishia kuniambia siasa ni safari ndefu lolote linaweza kutokea hivyo tudumu katika kuombeana na utashi wangu mwema utimie. Ifahamike, wakati namwambia hayo juu ya uwezekano wake kuwa mbunge hakuwahi kuniambia juu ya kufikiria kusimama kugombea, na wala hakuwa ameniambia juu ya jimbo la Kilombero. Nilishawishika na uwezo, dhamira, jitihada alizokuwa nazo na hakika kwa yeye kuwa katika siasa na kufanya kazi za chama kwa kujitolea na kujituma niliona ni miongoni mwa vigezo muhimu sana ambavyo vilimpatia zaidi na zaidi uwezo na ufahamu wa kisiasa hivyo nilitaraji yeye kugombea na kushinda mwaka 2010. Maneno yangu kwake daima yalikuwa msukumu kumuonyesha kuwa anaweza na kama alikuwa akisita kuthubutu apate ujasiri wa kusonga mbele. Na mwaka 2010, ndipo aliniambia dhamira yake ya kuingia moja kwa moja katika siasa. Kusimama katika jimbo na kushindana. Taarifa hiyo kwangu ilikuwa furaha kuu. Nilimwamini, na kuwa na uhakika angalifanya vizuri na kuibuka kidedea. Ukiwa mwaka wa mikiki mikiki mingi kisiasa, licha ya majukumu mengi, alidumu kuwasiliana nami na kubadilishana mawazo hapa na pale. Na hatimaye hata dakika za mwisho za kusubiri matokeo nilikuwa na furaha sana kuona amemudu kufanya vyema. Licha ya kutotangazwa mshindi. Hakika Regia alikuwa mwakilishi imara wa wanakilombero. Nilifurahi zaidi nilipoona orodha ya wabunge rasmi wa Chadema kupitia viti maalumu jina lake likiwamo, nakumbuka nilikutana nae na kwa furaha niliishia kumwambia; “unakumbuka lakini nilikwambia utakuwa mbunge?!” yeye hakujibu neno bali kicheko tu na kunirushia matani ya hapa na pale. Uwakilishi wa kibunge aliutumikia vyema pasi kuchoka, akijituma licha ya changamoto nyingi zilizopo katika uendeshaji wa siasa zetu nchini. Hakukata tamaa na kurudi nyuma. Hakuacha kujifunza, hakuacha kuwa msikivu! Ni mapambano haya ya kuleta mabadiliko katika jimbo la Kilombero ndiyo pia yalimsukuma Regia kuja na wazo la kuwa na vuguvugu “movement” ya maendeleo ndani ya Kilombero. Katika mwaka wa kiuchaguzi alikuwa tayari akitumia kauli ya; “Kilombero for Change” (Kilombero kwa Mabadiliko). Nakumbuka tulikutana na kujadiliana juu ya umuhimu wa kupiga hatua ya kutoka kuwa “movement” na chombo rasmi, kuwa taasisi kwa jina la Kilombero for Change. Jambo ambalo baada ya siku kadhaa aliniomba nilisimamie mwanzo mpaka mwisho kuhakikisha chombo kinasajiliwa na kuanza kujiendesha. Kazi ambayo niliipokea na kuitenda kwa uaminifu mkubwa nikijua nasaidia mabadiliko kwa wanakilombero na zaidi namsaidia rafiki yangu katika kutekeleza ndoto aliyonayo. Ingawa bado shirika halikufikia hatua ya kusajiliwa, lakini tulimudu kukamilisha taratibu zote zilizostahili katika usajili kama Katiba, nembo, jina na vingine vingi tuliweza kuvikamilisha nikisaidiwa na marafiki wa karibu katika harakati. Tukiwa tunasubiri jambo moja tu, orodha ya majina ya watu ambao aliwaamini walikuwa imara kuanza kutenda kazi katika ngazi ya wajumbe wa bodi. Mara kwa mara nikiwa namkumbusha juu ya kukamilisha mchakato wa kuanzisha taasisi, alikuwa msikivu na kunikumbusha pia umuhimu wa kuhakikisha anapata watu wazuri katika bodi na si bora watu tu kutimiza hitaji la uanzishwaji wa taasisi. Licha ya majukumu mazito ya kibunge, daima alikuwa mwepesi katika mawasiliano kupitia mitandao ya kijamii na hata simu yake. Alikuwa mshirika imara na mwepesi kushughulikia jambo hasa upatikanaji wa taarifa au nyaraka kwa wakati. Nilimtegemea sana kwa hili na yeye hakuniangusha daima. Kwangu daima aliendelea kuwa rafiki wa karibu zaidi hata ya nyadhifa yake! Najaribu kutafakari maneno ya Jim Reeves katika wimbo wake wa; “This world is not my home”! Siamini maneno haya sasa yanarindima kwa rafiki yangu Regia. Licha ya majonzi nafarijika sana kwa Regia kumudu kufanya mengi katika umri wake mbichi wa ujana. Amemudu hata kuthubutu kuingia katika siasa tena kupitia upinzani na zaidi kugombea kiti cha ubunge kupitia jimbo! Wengi sana wamekuwa wakiahirisha uamuzi na kusubiri miaka ipite kwanza. Wengi kwa kuwa wanawake wamekuwa wakirudi nyuma na kuacha kugombea kupitia majimboni. Amemudu kuishi na kuitumikia nchi, si tu katika harakati kupitia mashirikia ya watu wenye ulemavu bali katika kutunga sheria na kuisimamia serikali. Amejitahidi kurejesha matumaini na fikra mbadala kwa wanakilombero, kwa vijana, kwa wanawake na zaidi kwa watu wenye ulemavu. Amedhihirisha inawezekana! Licha ya nafsi zetu binadamu kutokumudu kuhimili majonzi na simanzi zito na kuishia kuanguka katika kilio, naamini Regia huhitaji machozi yetu sana sasa kama unavyohitaji sala zetu. Daima nitakuweka katika sala zangu. Daima tumuweke katika sala zetu! Pole sana kwa Remija natambua uchungu ulio nao kwa kupoteza pacha mwenzako. Pole sana baba na mama, najua mpo katika simanzi na majonzi makuu ya kumpoteza kijana wenu. Ni uchungu gani kumlaza kijana mbichi kama Regia!Mungu awape faraja na moyo wa saburi. Pole kwa familia nzima ya Regia, ndugu, jamaa na marafiki. Naamini ni kipindi kigumu sana, tuweka tumaini letu kwa MUNGU. Makamanda wote wa CHADEMA poleni sana. Kwa namna ya kipekee John Mnyika (MB) ambaye amekuwa chachu, taa na muongozo mkubwa kisiasa kwa Regia,pole sana. Mwenyekiti Mbowe na Katibu Mkuu Dr.Slaa, Makamu Katibu Mkuu Zitto na viongozi wengine wote pamoja na maafisa na watendaji wa chama Makao Makuu poleni sana. Kamanda alisimama kidete, alipambana, hivyo daima tunu kubwa itakuwa kuendeleza mapambano; Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke! Poleni sana wananchi wa jimbo la Kilombero! Poleni sana wabunge na bunge zima kwa ujumla! Zaidi poleni sana wananchi wote wa Tanzania. “Even though crying is a human act that helps in healing our pains in our souls…now Regia needs much our prayers than tears”!! (Hata kama kulia nikitendo cha kibinadamu kinachosaidia kutuliza maumivu katika roho…sasa Regia anahitaji zaidi sala zetu zaidi ya machozi!) Kwa kheri Kamanda! Ulale mahala pema peponi. © Michael Dalali, 14.01.2012 Somo hili ni murua sana na lina maneno yenye mifano ya hekima na busara ambayo mtu yeyote anayejiuliza ni kwa jinsi gani anaweza kupunguza au kuepuka kabisa mikwaruzano na wanajamii, anaweza kujifunza na kujitahidi kuitekeleza. Somo limehaririwa kidogo nami, lakini msingi wake ni maandiko ya Lucy Nkya katika gazeti la Tanzania Daima. Leo tutaangalia ni jinsi gani mtu unaweza kujiepusha na migongano isiyokuwa ya lazima. Mahali popote palipo na mkusanyiko wa watu iwe majumbani, kazini, shuleni, vyuoni na sehemu nyingine upo uwezekano mkubwa wa kutokea migongano isiyokuwa ya lazima, kama mtu hatajitathmini na kuamua kujiepusha na hali hiyo. Hivyo basi kutokana na hali hiyo ni vizuri kila mmoja akajua na kujifunza mbinu mbalimbali za kuishi na kila mtu, kwani anaweza akafanya jambo ambalo anaona kwake ni zuri na wakati huo huo likawa chukizo kwa watu wengine. Hii hutokana zaidi na maeneo ya mtu aliyokulia, mazingira ya familia iliyomzunguka, shule aliyosoma na malezi kutoka kwa wazazi au walezi wake. Mtu hupendwa na watu kutokana na kufuata tabia na kanuni za watu wanaomzunguka, pia mtu huchukiwa kutokana na kwenda kinyume cha kanuni za kuishi na watu vizuri wanaomzunguka. Tabia za kujifunza:
Tabia za kuepuka:
Mtoa maoni Kahabi ameandika hivi katika ukurasa wa facebook, "Wavuti.com ni kisima cha fursa kwa watanzania kuanzia habari, kazi, Scholarships na kadhalika. Nilipata kazi katika shirika la kimataifa kutokana na Tangazo kwenye tovuti hii. Pia nilipata Scholarship ya kusoma nje ya nchi kutokana na Tangazo katika tovuti hii. Kwa Mtanzania mwenye nia ya kufanikiwa katika maisha yake hatamaliza siku bila kusoma habari mpya na Matangazo katika tovuti hii. Ukijisajiri kila siku wanakutumia e mail yenye habari na fursa mpya. Ni kama vile unaletewa kazi na fursa nyingine katika mlango wa nyumba yako." Ndugu Kahabi, shukrani kwa kutoa ushuhuda huo kuhusu wavuti.com na kwa jinsi ulivyofaidi na kuwahimiza wengine kuitumia vilivyo tovuti hii ili kupata mengi kwa faida zao na taifa lao. Ni matumaini yangu kuwa wengi zaidi watazidi kuiperuzi wavuti.com katika kurasa zake mbalimbali na kupata yatakayowafaa. Nami nakupa pongezi kwa kufaidika na wavuti.com, ambalo ndilo lengo kuu la uwepo wake, yaani kushirikishana. 5 tips on How to Date a Friend 10/01/2012
Intro: "How to Date a Friend" is a guest post from Meggin Sanez of Black Online Dating Sites --- If you are friends with someone and realize that you possess feelings for them that are more than just friendly, you might be feeling overwhelmed. Although many of the greatest relationships begin with a foundation of friendship first, it can still be difficult to share or act on such feelings for fear of losing your friend if things don’t work out. However, if you keep your emotions bottled up inside, you run the risk of forever asking the question “what if?” To avoid such a fate, check out the following tips for taking a friendship to the next level: Assess your friend’s feelings. Before you tell your friend that you want to explore your relationship further with them, try to determine if they feel the same way. Set aside some alone time (not a date) for the two of you to casually hang out—whether it’s by watching TV or having lunch, this time spent without anyone else around should be able to give you a feel if there is a mutually romantic vibe between the two of you. Tell your friend. Gathering the nerve to tell someone how you feel about them is likely the most difficult step in the process of dating a friend. If you decide that you are ready to express to your friend your interest in dating them, put the butterflies aside and find a convenient time to sit down face-to-face somewhere it will be comfortable to discuss the subject. Gently and honestly communicate your feelings without being too emotional. Give your friend space to think. Whether the feelings are mutual or not, it might be shocking for your friend to hear that you are interested in them so they deserve some time to think and respond. If the feelings are mutual, plan to set up a date. If not and you still wish you to maintain a friendship, try to be understanding and be careful not to push the issue. Plan a casual date. If your friend wants to embark upon a dating relationship as well, that is great news! Now it’s time to plan the perfect first date. You may think an elaborate set-up will impress them, but because the two of you are likely to be nervous and self-conscious, it’s best to keep things simple and low-key. If you keep the first few dates casual, much of the pressure is taken off and you will find it will be easier to transition from friends into more than friends. Be yourself. This is a classic rule of dating that holds especially true to dating a friend. Your friend likely knows you very well so if you are putting on an act or letting nerves get the best of you, they are sure to see right through it. Remember that you are still the same people so just relax and be yourself—it’s why your friend liked you in the first place! The guest post author Meggin Sanez, enjoys writing about dating and relationships. In addition to her hobby of guest posting, Meggin also owns Black Online Dating Sites where she educates singles about safe black dating sites on the net. --- Thank you Meggin for this informative post. I have visited your site too. bestblackdatingsites.org | Vitabu vya WatanzaniaBofya picha ya kitabu unachokitaka ili ujinunulie nakala
Yaliyomo/CategoriesAll Hifadhi/ArchivesFebruary 2012 |






RSS Feed