Habari zinasema kuwa siku ya Jumamosi, maafisa katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha mjini Philadelphia nchini Marekani wamefaulu kukamata paundi mbili za madawa ya kulevya aina ya hashish na ounce moja na nusu ya marijuana zilizokuwa zimefichwa katika kifaa cha mchezo wa chess.

Maafisa hao waligundua siri ya urembo baada ya kustukia kibao cha chess kuwa na uzito usio wa kawaida.

Msemaji wa kampuni inayohusika na kitengo hicho cha vifurushi, Steve Sapp alisema kuwa bangi hiyo ilisafirishwa toka Tanzania lakini hakusema ilitakiwa kumfikia nani.

Polisi wanatathmini kuwa madawa hayo ya kulevya yatakuwa na thamani ya dola za Kimarekani $ 30,000.

Madawa hayo yatateketezwa.
Hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
 


Comments

28/10/2009 02:07

Nakutakia kila la kheri kati "NYUMBA" mpya uliyoamia.

Nimeona kuna mapinduzi mengi mazuri.

Daima bado tupo pamoja.

Tutafika tu

Reply
Wavuti
28/10/2009 07:06

Shukran Edo!
Nimehama tu mtaa lakini tupo kijiji kimoja bado.
Karibu tena!

Reply



Leave a Reply