wavuti
wavuti logo Facebook icon Facebook icon Twitter icon Subscribe RSS
 
Hiki ni kipande tu cha aliyoyasema Dk. Harrison Mwakyembe alipozungumza na waandishi wa habari 28 Oktoba 2009 na kuwapa changamoto kuhusu uandishi tafiti na kufichua habari mbalimbali.

Namshukuru sana Dr. Kiva kwa kukubali usumbufu wangu wa kumwoba kurekodi na kunitumia audio hii nami niiweke mtandaoni walao watu wengi waweze kusikia ya hapa na pale yanayosemwa na wabunge, wawakilishi na viongozi wa wananchi Tanzania.

Unaweza kusikiliza audio clip katika ukurasa wa 'Redio' sehemu ya 'TBC1 Redio Tanzania'.
 


Comments

Thu, 29 Oct 2009 3:15:28 am

Nimeikubali wavuti, Hebu niambie Da'Subi hizi wavuti unaziunda mwenyewe nini? kama ni hivyo sikuwezi.

Bless you.

 

Wavuti

Thu, 29 Oct 2009 3:18:51 am

Da' Mija,
Karibu kwenye wavuti.
Ni kweli wavuti zote tangu nukta77.com hadi blogu ya nukta77.blogspot.com na sasa wavuti.com ni kazi ya mikono yangu... huwa nachokonoa sana vitu visivyonihusu lakini vinavyonivutia teh teh teh, wenyewe wenye fani yao huwa wananikosoa nami nawaambia, mi najifunza jama, samahani kwa kuwachafulia lakini napenda kujifunza! mwe!

 

Thu, 29 Oct 2009 11:50:36 am

Usinambie, I'm speechless. Yaani nahangaika kutafuta wanawake wa shoka mbaaaali na kumbe wewe uko hapa hapo. Nitakutafuta.

Naomba niishie hapa. Hongera Mwanamke.

 

Fri, 30 Oct 2009 6:34:48 pm

Hivi hamna mtu wa kuwambia hao wasomaji wa habari kuwa wanasoma hizo taarifa zao kwanza kama wanaimba na pili wanasoma bila kufuata vituo?? Habari wanazosoma ni nzuri lakini usomaji haulingani na habari zenyewe wanazozisoma. Kuna umuhinmu wa kufanya mazoezi ya kusoma vizuri hizo taarifa za habari.

 

Comments are closed.