Wahenga walisema, "ukiona mwenzio ananyolewa, nawe katie zako maji".
Habari kwa mujibu wa tovuti ya BBC Swahili zinasema ifuatavyo kuhusu majirani zetu:

Nchi ya Marekani imesitisha ufadhili wa dola millioni saba za mpango wa Elimu Ya Bure kwa Shule za Msingi nchini Kenya.  Balozi wa Marekani nchini Kenya bwana Michael Ranneberger amesema ufadhili huo utasitishwa hadi pale madai ya ufisadi katika Wizara ya Elimu yatakapochunguzwa.  Hatua Marekani kusimamisha ufadhili huo imechukuliwa mwezi mmoja baada ya Serikali ya Uingereza kuondoa ufadhili wake kwa sekta hiyo ya Elimu. Balozi Ranneberger amesisitiza kuwa ni lazima mpango mzima wa Elimu ya bure nchini Kenya ufanyiwe uchunguzi. Marekani imekuwa ikishinikiza serikali ya Kenya kutekeleza mabadiliko mbalimbali nchini humo.
 


Comments

Mallaba Jr
27/01/2010 02:25

This is just the begining, Utawala wa Obama umeshatangaza kupunguza misaada Africa ,kwa hiyo sishangai kuona hivyo na bado kwa nchi yetu Tz ndo hao mafisadi watakapo pata adabu. Wanabadilisha mfumo wa kutoa pesa yaani mpaka ziwe zimehakikishwa kwamba zitafanya nini au kutakuwa nafaida gani kwa wananchi husika chini ya Balozi wao..Saasa kama unakumbuka JK amewapiga mkwara mabalozi kuingilia serikari yake ..je unategemea wafanye nini?Wanalalamika sana wafadhili kuwa pesa haziwafikii walengwa.
Hata kama ningekuwa ni mimi lazima nifuatilie matumizi ya pesa zangu.....
So dont be worry and not much far this gonna happen even in our country.

Reply
27/01/2010 02:34

Hizi habari za misaada na kukata misaada huwa hazieleweki kinagaubaga, ninachoamini ni kuwa pande mbili - mtoa msaada na mpokea msaada - hufaidika kutokana na makubaliano maalumu, shida inakuja pale mpokea msaada anapofanya marororso yanayomchukiza mtoa msaada, yaani kula na kipofu kisha umguse kabisa na uanze kumringishia kuwa wewe una gari nzuri zaidi yake na nyumba bora sana wakati hela kakupa yeye kwa makubaliano ya kufanya jambo tofauti na uliyoyafanya.
Pengine katika kunyimwa misaada kutachangamsha akili - tutafute kwa taabu na tutumie kwa makini - ila tusifikie waliko Zimbambwe jama.

Reply



Leave a Reply