Picture
mwanariadha Mtanzania Marko Joseph
Tangu ampokonye ubingwa Mbarzili Franck Caldeira (mwaka 2008), huu ni mwaka wa pili mfululizo kijana Marko Joseph (miaka 20) anaibuka kidedea katika mashindano ya kilomita kumi nchini Brazili.  Marko ameweza kumaliza mbio za mwaka huu katika muda wa dakika 29 na sekunde 58, rekodi ambayo ni bora zaidi kwa kutangulia sekunde tano kulinganisha na rekodi aliyoiweka mwaka jana, ishara kwamba kiwango cha Marko kimeimarika.

Kwa upande wa wanawake, mkimbiaji wa Kenya, Chepkorir Kipkoechi aliibuka mshindi kwa kumaliza mbio hizo katika muda wa dakika 34 na sekunde 24, hivyo kuwazidi washindani wake wa karibu Mwethiopia Zeineba Hasso Hayato na Mbarazili Maria Zeferina Baldaia

Mashindano hayo yalifanyika nchini Brazili siku ya Jumapili na yanajulikana kwa jina la King's Run. 

Hongera sana Marko kwa ushindi huu na tunakuombea mafanikio tele kwa mwaka huu katika mashindano zaidi yajayo.

 


Comments




Leave a Reply