Ile kidali poo inayochezwa baina ya nchi za Kenya na Tanzania na yule bwana Al-Faisal bado ipo pale pale. Ukitaka kusoma ilivyokuwa, rejea posti ya awali kwa kubofya hapa. Huyu bwana, alikatiza alikokatiza kwa njia anazozijua yeye, hadi alipokwamia nchini Kenya. Huko nao wakafanya mipango na hatimaye wakatutangazia kuwa wamekubaliana kumsafirisha hadi Naijeria kwa malengo ya kumfikisha nchini Gambia, nchi pekee iliyokuwa na uwezekano wa kukubali kumpatia usafiri wa ndege wa moja kwa moja hadi kwao Jamaika. Iliripotiwa na wasemaji wa polisi wa Kenya kuwa, haikuwezekana kumsafirisha  bwana Al-Faisal hadi Marekani ili akamalizie safari ya kwao kutokana na Marekani kumpiga marufuku ya kusafiri katika anga yake.

Shirika la Associated Press linairipotia New York Times kwamba, bwana Al-Faisal wala hakukanyaga Gambia bali alirejeshwa tena nchini Kenya kutoka katika kiwanja kimojawapo cha ndege cha nchini Naijeria ili akaanze upya safari yake ya kurudi kwao Jamaika.

Tuhuma zinazosababisha azuiliwe kusafiri katika nchi kadhaa ni hivi:
Mr. Faisal was convicted in Britain in 2003 of inciting racial hatred for urging his followers to kill Hindus, Christians, Jews and Americans, and he was accused of influencing one of the bombers who struck the London transit system in July 2005. Britain deported him to Jamaica in 2007, and it is not clear how he ended up in Africa.

Soma habari kamili kupitia linki hii: http://www.nytimes.com/2010/01/11/world/africa/11kenya.html
 


Comments




Leave a Reply