
Naye mwanaharakati Kainerugaba Msemakweli amesema hujuma dhidi ya harakati za kupambana na ‘ufisadi wa elimu nchini’, unaodaiwa kufanywa na baadhi ya vigogo nchini, zimepamba moto, baada ya mpango wake wa kuanika zaidi kashfa hiyo kupitia mabango kukwamishwa. “Nimehujumiwa. Maana tarehe 18 (mwezi huu) watu wanne walikwenda kampuni ya mabango na kuwatisha kuwa wakikubali niweke mabango watachunguzwa kodi zao na mabango na wamejenga kwenye hifadhi za barabara. Naandaa kuwafungulia kesi kwa kuvunja mkataba na mimi”.
Mabango hayo ilikuwa yawekwe katika baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na kwenye majimbo yanayowakilishwa na wanasiasa hao, ikiwa ni hatua ya tatu ya mapambano aliyoyaanzisha dhidi ya ufisadi wa elimu nchini. Jijini Dar es Salaam yangewekwa katika daraja la Salender, Jangwani, makutano ya barabara za Nyerere na Kawawa na Barabara ya Kilwa karibu na bandarini.
Kabla ya hujuma dhidi ya mabango hayo, Msemakweli alilalamikia kufanyiwa hujuma vitabu alivyochapisha vinavyoelezea kashfa ya vigogo hao jijini Dar es Salaam na mkoani Mwanza, ambapo mtu mmoja alionekana akinunua nakala zaidi ya 600 kwa mkupuo mmoja bila kujulikana anakozipeleka.
Kwa habari kamili, jisomee gazeti tando la NIPASHE kwa kubofya hapa




RSS Feed