wavuti
 
Picture
Hongera kwa wote waliopiga hatua kimasomo na kumaliza elimu ya kidato cha nne mwaka 2009.

Unaweza kutizama matokeo ya mtihani wa Taifa kuhitimu katika ngazi hiyo ya elimu kwa njia mbili. Moja ni kwa kutumia tovuti na nyingine ni kwa kutumia simu kwa wateja wa VodaCom pekee.

Bofya kujaribu kati ya linki zifuatazo:
  1. www.tetea.org/olevel.htm
  2. www.moe.go.tz/NectaResults/olevel.htm
  3. www.necta.go.tz/html_csee209/olevel.htm
  4. www.necta.go.tz/publishedresults/csee.php
AU
Tumia simu ya mteja wa VodaCom.
Tuma ujumbe mfupi wa maneno (sms) kwenda 15311 yenye message: MatokeoXcentreXcandno
Badili neno 'centre' na uandike jina la shule/kituo ulichofanyia mtihani
Badili neno 'candno' na uandike namba ya mtahiniwa
Kwa mfano: MatokeoXS0452X0203
Shukrani zimwendee Augsustine Maguta aliyetushirikisha njia mbadala.

ANGALIZO
Ikiwa namba ya kituo ulichofanyia mtihani namba zake zina tarakimu chini ya nne, unahitaji kubandika tu tarakimu hizo bila kutanguliza sifuri.
Kwa mfano: Namba ya shule/kituo ni S0012 na namba ya mtahiniwa ni 45 basi andika MatokeoXS12X45

Huduma zilizotajwa hapo juu kwa ajili ya matokeo haya hazitatozwa fedha yoyote ile.

ILANI
Tovuti ya matokeo inaweza kutokuwa hewani (off line due to bandwidth limit) kutokana na kuzidiwa na wingi wa watu wanaotaka kuona matokeo. Hilo ni suala la IT wanaohusika na wizara hiyo wanaweza kulirekebisha. Ufikwapo na hali hiyo, pole kwa usumbufu huo, ndivyo Wizara zetu za Serikali zilivyo na bandwidth ndogo il hali uhitaji ni mkubwa, hasa kwa tovuti hii ambayo imekuwa ikilalamikiwa kwa miaka mitatu mfululizo kwa tatizo hili hili, sifahamu mkakati wao wa kulitatua tatizo hili.

 


Comments

Hugo

Sun, 07 Feb 2010 04:13:31

safi sana na thanx kwa kuweka link hapo. nilikuwa natafuta haya matokeo kwenye site ya necta sijui ni kimeo, inaniambia record hazipo..

 

Sun, 07 Feb 2010 06:46:03

Hugo,
watu wengi wanakwenda kwenye tovuti ya NECTA ambako ndiko yanakotarajiwa kuweko matokeo lakini hayajabandikwa'mo yapo tu yale ya Ufundi, badala yake matokeo ya Form Four wameyaweka kwenye tovuti ya MOE tatizo, kwikwi ya bandwidth! Yaani matokeo yalipotoka tu niliweza kuyaona lakini saa chache baadaya ujumbe kusambaa watu walipoanza kutembelea tovuti kwa wingi ikazidiwa ikaenda doro.
Kaazi kweli kweli yani.

 

Sun, 07 Feb 2010 12:03:28

 

emmanuel samwel

Mon, 08 Feb 2010 11:24:38

Dah hiyo link yako imetulia kinyama na iko very faste ni kubofya tu na kupata tokeo dahh uko juu sana mzee

 

Mon, 08 Feb 2010 14:38:43

Pia yanapatikana hapa:

http://www.tetea.org/olevel.htm

Kama tovuti ya NECTA inakusumbua mno.

 

Mon, 08 Feb 2010 22:44:01

Brian Sterr,
Shukrani kwa linki uliyotoa, nimeiongeza kwenye orodha hapo juu.
BTW, tovuti nzuri ya TETEA, nashukuru kuifahamu.

 

ahamadi lalikila

Tue, 09 Feb 2010 01:33:26

 

TAMOTA

Tue, 09 Feb 2010 04:14:42

 

calvin nimrod oshorael some

Tue, 23 Feb 2010 02:14:05

 



Leave a Reply