wavuti
wavuti logo Facebook icon Facebook icon Twitter icon Subscribe RSS
 
Yule jamaa aliyenenepesha nyeti zake hadi kufikia zaidi ya kg10, Gasper Honza tayari amenza kupatiwa matibabu Nchini India, blogu ya Sufianimafoto inaandika.

Jopo la madaktari wa hospitali hiyo (jina kapuni mwa Sufianimafoto) tayari wameanza kufanya uchunguzi wa awali kwa kuchukua kipande cha nyama (biopsy) kutoka kwenye nyeti zake ili kubaini kemikali zilizokuwamo kwenye dawa aliyotumia.

Akizungumza na Sufianimafoto kwa njia ya simu jana kuhusiana na matibabu hayo, Gasper alisema tayari jopo hilo limempa dawa ya kupaka aina ya Hip absorb kwa ajili ya kupunguza uvimbe alionao kabla ya kumfanyia upasuaji katika nyeti yake.
“Kwa kweli tangu nimeanza kutumia dawa hii ninaona uvimbe unapungua japo napata haja ndogo chafu pamoja na maumivu makali, sina wasiwasi kwasababu nataka kupona hata hivyo daktaria wangu ameniambia nitapoteza nguvu za kiume jambo ambalo naona ni kawaida maadamu niutue mzigo huu,” alisema.

Kwa mujibu wa Dk. Hich Yagien wa India, Honza atapoteza uwezo wa nguvu za kiume baada ya upasuaji huo kutokana na uvimbe huo mkubwa kukaa kwa muda mrefu.
“Honza alifanya tofauti sana kwani dawa aliyotumia kwani dawa hiyo ni kwa ajili ya kukuza makalio ambayo zaidi hutumiwa na baadhi ya wanawake ingawa wengine waliotumia wameathirika na saratani na baadhi wamepoteza maisha baada ya upasuaji kutokana na kutokwa na damu nyingi. alisema daktari huyo.

Dawa hiyo ina nguvu sana na kwa mujibu wa maelezo ya dawa yenyewe mtu anatakiwa atumie mara mbili kwa wiki, lakini mtu anapoitumia bila kufuata masharti matokeo yake ni kama hayo ya kuvimba nyeti ama makalio bila mpngilio. ” alisema Dk. Yagien.
Alisema Honza atafanyiwa upasuaji mara baada ya vipimo kukamilika mwishoni mwa wiki hii.

Aidha alisema kuwa Honza si mgonjwa wa kwanza kukutana naye kwani ameshakutana na wagonjwa wa aina hiyo wengi tu ambao ameshawatibia kwa kuwafanyika upasuaji huku wengine wakifikishwa hospitalini hapo wakiwa wameoza.

Honza ambaye ni Mkazi wa Mbezi Beach Dar es Salaam, anatarajia kufanyiwa upasuaji huo wiki ijayo baada ya kutumia dawa ya kukuza makalio aina hypson akiwa na nia ya kukuza Nyeti ili kuinusuru ndoa yake Septemba mwaka jana.
 


Comments

Rama

Sun, 14 Mar 2010 11:36:51 am

Best wishes!

 

Sun, 14 Mar 2010 11:45:28 am

Hebu tufafanulie nini maana ya nyeti?

 

Adam, L

Sun, 14 Mar 2010 6:12:41 pm

KUINUSURU NDOA!!!!!!??????
Asalaleeeeeeeeeeee. Ee Mungu samee mutu sisi!! Ponya hii mutu

 

Ikera

Mon, 15 Mar 2010 11:02:56 am

Hakika haya ndio mambo ambayo sisi binadamu tunakosea sana. Tuombe Mungu atusamehe. Nia yake kunusuru ndoa sasa je itakuwaje maana jogoo hatapanda mtungi baada ya operesheni...pole zake.

 

Suzy

Mon, 15 Mar 2010 11:14:22 am

Maskini, alijua anaponya kumbe anaharibu. Turidhike na hali zetu wanadamu Uumbaji ni kazi ya Mungu. Mungu atusamehe.

 

Cheomi

Mon, 15 Mar 2010 4:05:01 pm

Daah!! hiyo kali eeh Mola tuepushie juu ya mambo hayo

 

ochima

Sat, 20 Mar 2010 4:09:37 pm

huyu mtu balaa lakini wasichana wengine wanapenda nyeti ziwe kubwa ili wasikie utamu,sasa naona demu wake alikuwa haridhiki akabidi afanye hivyo.tumsamehe

 

maroso

Sat, 20 Mar 2010 4:12:02 pm

kuna dada mmoja anapenda watu wenye nyeti kubwa kasababisha aachane na mkewe akaanza kuvamia wanaume wa watu eti kisa mume ana nyeti ndogo,balaa

 

Comments are closed.