Gavana wa Jimbo la Zhangdong nchini China bw. Sun Liang akizungumza na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Profesa David Mwakyusa kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo. Mgeni huyo pamoja na ujumbe wake walifika Wizarani hapo kwa mazungumzo mafupi juu ya mkakati wao wa kujitolea kujenga kituo cha kutibu magonjwa ya moyo na upasuaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Photo credit: Issa Michuzi blog

Jiwe la Msingi la Taasisi ya Tiba ya Moyo Muhimbili lasimikwa rasmi

Picture
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (wanne kushoto) na Balozi wa China nchini Bwana Liu Xinsheng (watatu kushoto) wakiweka udongo katika jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi kwa ujenzi wa Taasisi ya Tiba ya  Moyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili MNH tarehe 31 Machi 2010. Wengine katika picha ni Waziri wa Afya Profesa David Mwakyusa(watano kushoto) na kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Bwana Adolar Mapunda, wapili kushoto ni kiongozi wa ujumbe wa Jamhuri ya watu wa China bwana Sun Liang

Photo credit: Freddy Maro/Ikulu
 


Comments




Leave a Reply