Swali: Tusaidianeni katika kunyosha utata huu katika sentensi ifuatayo JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA na JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA.
Ipi ni sentensi sahihi kati ya hizo sentensi mbili?
Paul
|
|
Ni swali alilouliza Paul Misalaba siku chache zilizopita kwenye kisanduku cha maoni na bado halijapata jibu. Swali: Tusaidianeni katika kunyosha utata huu katika sentensi ifuatayo JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA na JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA. Ipi ni sentensi sahihi kati ya hizo sentensi mbili? Paul Commentsmashaka 31/03/2010 04:46
Sahihi tunasema muungano huu ni wa aina gani na si ya aina gani ni wa kimajimbo au nchi mbili huru ,kwahiyo sahihi ni jamhuri ya muungano wa tanzania.mf ndoa ni muungano wa watu wawili. ya inaonyesha umiliki wa jamhuri ya muungano ninani?na haionyeshi ninani walioungana. David Fred 31/03/2010 09:41
Halo bwana Paulo. Kuna tofauti ya matumizi ya neno /kiunganishi 'ya' na neno/kiunganishi 'wa'.Neno 'wa' linaonesha muunganiko wa vitu viwili na wakati mwingine hata umiliki wa kitu.mf. umoja wa wanafunzi,kuku wa Abdala .Neno 'ya' linatumika kuelezea kitu(kuelezea maana ya kitu)mf.Siku ya uhuru(hii inaelezea hiyo siku ni siku maalumu ya kuadhimisha uhuru) . Subi KNY Monsignor (comment via GBuzz) 31/03/2010 11:49
Inaitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania..rejea Katiba ya mwaka 1977 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2000. Soma kichwa cha habari cha katiba yenyewe pia anza kuingia ndani uk 9 tunapotangaza jina la Tanzania kwenye sheria ya 1984 Na.15 ibara ndogo ya 3utaikuta......Mazoea yana tabu, sijui kwa sababu ya urahisi wa kutamka ya badala ya wa.. Paul 31/03/2010 21:51
Nashukru sana kwa michango yenu mizuri juu ya hili swali. Mbwambo 11/04/2010 09:00
Hii iko wazi. Sentensi sahihi ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ukitumia "ya" badala ya "Wa" lazima usitaje neno "Jamhuri" ila utaje neno kama "Nchi". Leave a Reply |