Blogu ya Ikulu ya Tanzania vipi jamani?

Kuna mtu anaweza kunifahamisha umbumbu wangu wa TEKNOHAMA?.

Hivi blogu ya Ikulu ya Tanzania inaendeshajwe? Haina habari za kila siku?Hivi yote yanayotokea Tanzania, ziara za waziri mkuu hivi karibuni, mama Salma Kikwete, Rais Kikwete safari zake zote za mwezi mzima uliopita, risala zake, hotuba zake, angalau hayo tu yanashindikana kuwekwa kila siku?
mawasilianoikulu.blogspot.com

Hivi idara ya mawasiliano ya Ikulu hawalioni hili?

Leo Jumapili 18.04.2010. Habari za mwisho kwenye blogu hiyo ni za Machi 18. Mwezi mzima umepita. Matukio mengi yamepita katika kipindi hicho, lakini hakuna hata picha wala nini. Tunaona picha kwenye blogu ya Michuzi, Mjengwa, Hakingowi, Mrocky, Wavuti na nyinginezo za watu binafsi.

Ikulu ka!

Basi wacha blogu, tovuti ya taifa la Tanzania, ndo´kichekesho! Manaake habari haziko katika mpangalio. Ziko shaghalabaghala! Angalieni wenyewe hapo: www.tanzania.go.tz

Mbona tovuti za wizara mbali mbali habari zake ziko katika mpangilio? Hii ndio sura ya Tanzania nje ya nchi, lakini mwee?sisemi mengi.

Hata tovuti ya Waziri Mkuu www.pmo.go.tz inapendeza iko katika mpangalio mzuri.

Wenu Tausi Usi Ame Makame,
Oslo
(anwani pepe imehifadhiwa)

YATOKANAYO
wavuti.com inaunga mkono kilio cha Tausi na Watanzania wengine ambao tumekuwa tukipiga kelele kila leo, hasa Dk. Faustine ambaye ameandika mara kwa mara kuhusiana na kero hii lakini inaonekana kelele hizi ni sawa na za kupigia mbuzi gitaa. Watanzania tunapenda turinge kuwa nasi tupo katika karne ya Sayansi na Teknolojia katika TEKNOHAMA lakini tunashindwa kujivunia hata kuthubutu kuhadithia ati tuna mkondo wa mawasiliano ya uliofunguliwa rasmi na Raisi mwaka jana na sasa kuna ujio wa EASSy cable.
Tafadhalini wahusika wa IT Serikalini tuondoleeni hili kwani sisi tupo tayari kuitangaza e-Tanzania.
 


Comments

kaizio
18/04/2010 13:37

blogo inatia aibu. ikulu inakuwa na blog kama ile. Ulizia gharama zilizotumika kucreate hiyo blogu.

Reply
18/04/2010 16:24

Mie nilishasikia kilio cha Dr Faustine nami nikaimba weeeeeee lakini "where"?
Yaani hawa wanatia kinyaa Dadangu.
Nadhani schedule yako haikukuwezesha kuisoma post yangu niliyouliza kama TAARIFA NI HAKI YA MWANANCHI AMA..? (http://changamotoyetu.blogspot.com/2010/02/taarifahaki-ya-wananchi-ama.html)
Na huko umeenda mbali Dadangu. Si wakumbuka KICHEKESHO cha tovuti ya ubalozi wa Tanzania hapa Marekani na uongo wao???
Mie wakati mwingine nishachoka Dada

Februari 15, Edo Ndaki aliweka post juu ya Air Tanzania kutokuwa na tovuti (http://edondaki.blogspot.com/2010/02/air-tanzania-haina-websitekituko.html) na niliweka maoni nikisema

Pole kwa kushangaa kaka. Yaani kama hili tatizo la kutokuwa na website zinazofanya kazi, basi wenzako "tumeshashiba njaa" kwa tatizo hili.
Tusiwaonee AIR TANZANIA. Tuanze na wakubwa wao.
Ingia TOVUTI YA IKULU (http://ikulu.go.tz/)uone utakachokutana nacho. Anyway, hao wako busy, basi twende kwenye SHIRIKA LA UTANGAZAI TANZANIA (http://www.tbc.go.tz/)ambayo ilikuwa hewani kwa wiki moja baada ya hapo iko matengenezoni kwa miezi sasa. Who cares.
Lakini zinazofanya kazi nazo umeona updates zake? Angalia hii ya Idara ya Mawasiliano Ikulu (http://mawasilianoikulu.blogspot.com/)ambayo licha ya Rais ambaye ni msafiri kuliko uhitaji, bado updates zao ni za kusikitisha.
Anyway, labda hilo si tatizo. Kuna ambao wanaweka HABARI ZA UONGO. Kama nilivyoandika kwenye post yangu ya leo kuhusu tovuti ya UBALOZI WA TANZANIA HAPA MAREKANI. Nimeiona web yao baada ya kukutana na maelezo haya ya Uncle John Kitime aliyesema "Umekosa website za vichekesho? Basi google Tanzanian Embassy USA, kisha fungua ukurasa wa Embassy of Tanzania, fungua About Tanza...nia, halafu fungua People and culture hapo ndo utajua kumbe Ze Comedy wako wengi. Je ulijua kuwa Zouk na ndombolo ni tradional music wa Tanzania? Je ulijua kuwa Pilau kizungu ni wild rice? Je... ulijua chapati ni bread? Halafu kuna michapo mingine kuhusu mtunzi wa wimbo wa Taifa nk"
Isome hapa (http://www.tanzaniaembassy-us.org/tzepeo.html)
Labda nikwambie kaka kuwa ukitaka kujua yanakoanzia haya, basi angalia tovuti hizi za vyuo kama zilivyoelezwa na mdau hapa (http://issamichuzi.blogspot.com/2010/02/yaaawnnext-please.html)

NI MWENDO WA KINYONGA, LAKINI TUTAFIKA TUUUUU!!

Reply



Leave a Reply