Picture
Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Juma Kapuya (aliyeketi kulia) akitangaza viwango vipya vya mishahara kwa kima cha chini kwa wafanyakazi wa sekta binafsi tarehe 30 Aprili 2010 wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam.
Waziri wa Wizara husika ametangaza viwango vya kima cha chini cha mshahara na kutaja kima cha chini cha mishahara hiyo kwa sekta mbalimbali binafsi kama ifuatavyo, wafanyakazi wa:
  1. Huduma za Afya - Tshs 80,000/=
  2. Sekta ya Kilimo - Tshs 70,000/=
  3. Viwanda na Biashara - Tsh. 80,000/=
  4. Maji (Bahari na Uvuvi) - Tsh. 165,000/=
  5. Ulinzi Binafsi - Makampuni makubwa na makampuni ya kigeni - 105,000/=; Makampuni menginey o- 80,000/=
  6. Madini - [Migodini 350,000/=; Wachimbaji wadogo -150,000/=; Wauzaji wadogo na watoa leseni 250,000/=; Brokers Licenses 150,000/=
  7. Mahotelini - Hoteli kubwa za kitalii - 150,000/=; Hoteli za kati - 100,000/=; Hoteli ndogondogo,mabaa, nyumba za wageni na migahawa- 80,000/=
  8. Usafirishaji na Mawasiliano - Huduma za anga 350,000/=; Clearing and Fowarding 230,000/= Mawasiliano ya Simu 300,000/=; Usafiri wa nchi kavu 150,000/=
  9. Majumbani (mabalozi na wafanyabiashara wakubwa) - isiwe chini ya Tsh 90,000/=; Maafisa wenye sitahili ya kulipiwa huduma hii -isiwe chini ya Tsh.80,000/=; Wengineo - Tshs 65,000/=
  10. Sekta nyingine ambazo hazikutajwa - 80,000/=
Habari kwa mujibu wa taarifa East Africa Radio na blogu za Issa Michuzi na John Bukuku - Full Shangwe.
Picha na Aron Msigwa wa Maelezo.
 


Comments

JJ
30/04/2010 14:53

Hivi mbona mnakurupuka? Tatizo sio mishahara pekee bali mafao ya uzeeni, sasa mmeona uchaguzi unakuja mnakurupuka.

Reply



Leave a Reply