Picture
Abdon Kidege (miwani myeusi) | Rainfred John Masako (kofia
Mtangazaji na mwandaaji wa vipindi vya ITV na Radio One bwana Rainfred John Masako ametangaza nia yake ya kugombea ubunge katika jimbo la Ulanga Magharibi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Mbunge wa sasa wa jimbo hilo ni  mheshimiwa Juma Ngasongwa aliyewahi kuwa Waziri Serikalini katika vipindi tofauti.

Rainfred Masako aliyezaliwa mwaka 1952 katika Wilaya ya Ulanga amesema muda alioitumikia jamii katika masuala mbalimbali unatosha sasa na anataka awasaidie wananchi wa Jimbo la Ulanga kupitia Siasa, akaongeza kuwa yeye ni dhahabu iliyokuwa ikitembea na sasa ili wakazi wa jimbo la Ulanga waichimbe na kuipata ni kumpa ubunge yeye ili wasaidiane katika kuinua uchumi wa wakazi wa jimbo hilo. 

Pichani, aliyeketi  kulia mwa Rainfred Masako ni mshauri wake wa masuala ya Siasa bwana Abdon Kidege.

Photo credit:
John Bukuku - FullShangwe

 


Comments

S.MTUWA
15/04/2010 17:08

Kweli siasa ni dira ya mafanikio , kila lakheri Ndgu A.J. Masako , ....... wenye vijiko hayaaaa... wenye madumu hayaaaaaaaa.... wenye ndoo hayaaaa.. ili kila mtu apate japo kidogooooo




Reply
15/04/2010 23:17

Wewe Masako ni kipenzi cha wengi wanaopenda kujua ukweli kuhusu nchi hii. Ikiwa nia yako ni ya dhati na siyo kubipu , basi ninakutakia mafanikio na naamini wananchi wa Ulanga wanahitaji mabadiliko sasa.

Reply



Leave a Reply