Picture
Mkuu wa Mkowa wa Dar Es Salaam bwana William Lukuvi amesema kuwa Serikali ya Mkoa imewahamisha watumishi tisini na sita (96) wa hospitali ya Mwananyamala na kuwapeleka katika hospitali nyingine za ndani na nje ya Mkoa wa Dar Es Salaam.

Watumishi hamsini na saba (57) wamehamishiwa katika hospitali za Dar es Salaam na thelathini na tisa (39) wamepelekwa katika hospitali za nje ya mkoa. Hospitali hiyo imepokea wafanyakazi wapya hamsini na nane (58) kutoika katika hospitali nyingine.

Kwa kuwa uhamisho siyo suluhisho pekee la kuboresha huduma katika Hospitali hiyo, Serikali imepanga kuongezewa bajeti katika kipindi cha mwaka ujao wa fedha, ili kuimarisha miundombinu na vitendea kazi.

Itakumbukwa kuwa hospitali hii ya Wilaya ya Kinondoni imekuwa ikilalamikiwa kwa muda mrefu na wananchi kutokana na huduma mbovu, zisizoridhisha na kauli za kuudhi kutoka kwa baadhi ya watumishi. Malalamiko hayo yalisababisha kuundwa kwa Tume kadhaa ambazo takribani zote zilipendekeza kuhamishwa kwa baadhi ya watumishi ambao wamekuwapo eneo hilo kwa zaidi ya miaka thelathini (30) sasa.

 


Comments

msakanyoka
13/04/2010 06:16

Naomba haya yaliyofanyika mwananyamala yafanyike kwa hospitali nyingine pia,lakini napenda kuikumbusha serikali kuwa dawa si kuwabadilishia vituo vya kazi ikibidi hata wafukuzwe kazi kabisa ili kuwafanya wengine waliobaki wajifunze kitu kutoka kwa wenzao,hata hivyo tunaishukuru serikali kwa kusikiliza kilio cha muda mrefu!

Reply



Leave a Reply