"Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu imesikia kilio cha wananchi wengi. Imeongeza muda wa usajili wa simu za viganjani hadi Julai 15, mwaka huu baada ya hapo simu zote ambazo hazijasajiliwa zitafungwa,” alisema Profesa Msolla.
Baada ya muda uliotengwa awali kuonesha kuwa watu wengi hawakuwa wamesajili laini zao, mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania, TCRA, iliongeza muda wa miezi sita, yaani Januari - Juni 30, 2010 kwa wananchi wote wenye simu kuwa wamesajili laini zao za simu kwa makampuni husika.
credit: Margareth Kinabo na Benjamin Sawe/Maelezo-Dodoma via: GPL


RSS Feed