Hii ni picha iliyonigusa moyo wangu, ijapokuwa sifahamiani na yeyote katika picha hii, nafsi yangu imepatwa na huzuni kubwa. Nimetamani nijizuie lakini hisia nzito zilizojaa simanzi zimeshinda ujasiri wa nafsi. Ninajua Mungu ataweka njia kwa ajili ya malaika huyu aliyeachwa mikononi mwa mzazi mmoja. Yeye aliyeruhusu Mama kutangulia wakati huu alipohitajika zaidi kwa mwenza wake na mtoto wake, atafanya njia. Mipango yake si mipango yetu, mawazo yake si yetu, tukimtumaini na kumtegemea, atatuonesha njia. Yeye aliyeruhusu yote kutokea kwa kuwa Yeye ni Yeye, tukikubali ama kupinga, bado anabakia kuwa Yeye.
Ni kwa picha hii naguswa kuwaombea faraja wale wote waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki kifoni.
Mwenyezi, Yeye aliye mwingi wa rehema na neema, akupeni nguvu ya kutosha katika kipindi hiki kigumu.
Wimbo aliouimba Reuben Kigame na rafikize, 'Nitayainua Macho Yangu', uwe faraja kwenu nyote muaminio.



RSS Feed