Niliandika kuhusiana na ubaya wa kuwa na mipango mizuri ya mradi kwa ajili ya kuisaidia jamii, lakini kosa likatendeka katika kutokuwashirikisha walengwa, na matokeo yake ni wananchi kuona kama hawahusiki katika mradi huo, na hivyo kutokushiriki kikamilifu katika kuulinda, kuutunza na kuuendelea.
Picha inayoonekana hapa chini tena ni mojawapo ya mfano hai wa jinsi miradi isiyoshirikishi inavyoweza 'kususiwa' na kubaki kuwa kama urembo na magofu na kuishia kupewa majina ya kejeli.
Nimeishi pia Ilala, nakumbuka Jiji walijenga soko kwa ajlii ya Wafanyabiashara wadogo wadogo ili waweze kuhama Mchikichini na Boma waelekee soko jipya, wakalazimisha na daladala kufanya 'ruti' zake eneo hilo. Lakini siku baada ya siku soko lilizidi kuwa 'jeupe' huku baadhi ya Wafanyabiashara wachache waliohamisha makao na kufikisha bidhaa zao hapo wakilalamikia 'ukame' wa wateja, nao wateja wakilalamika 'umbali'.



RSS Feed