Viongozi hao wa dini walisema kuwa kukataa matokeo ni chanzo kikubwa cha uvunjifu wa amani na husababisha nchi kuingia kwenye matatizo makubwa kisiasa.
Wakawaomba viongozi wa vyama vya siasa kuacha tabia ya kushambuliana majukwaani, badala yake wanadi sera na Ilani za vyama vyao.
Dk. Slaa akizungumzia maombi ya viongozi hao wa dini kuwa wakubali matokeo yatakayotangazwa na Tume, alisema “tuliwaambia vurugu baada ya uchaguzi zinatokana na matokeo, nasi tumesema wao wasitwambie tu tupokee matokeo, ila wahakikishe taratibu za haki zinafuatwa katika kupata matokeo”.
Tume hiyo imekuwa ikuzungumza na viongozi wakuu wa vyama vya siasa katika kipindi hiki cha kampeni za Uchaguzi Mkuu na tayari wameshakutana na Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad na uongozi wa juu wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Willibrod Slaa na John Mnyika.




RSS Feed