Mtoto wa mgombea Urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jakaya Mrisho Kikwete, Ridhiwani Kikwete leo ameonja joto la jiwe katika ziara zake za kampeni ndani baada ya kutimuliwa mbio zaidi ya mara moja wakati akitaka kufanya kampeni za CCM katika taasisi za umma.

Ridhiwani ambaye ni mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya baraza kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) Taifa akiwa na viongozi akiwemo aliyekuwa mshindi wa kura za maoni jimbo la Iringa mjini Frederick Mwakalebela na washiriki wengine wa kura za maoni kama Jescar Msambatavangu, walifika katika shule ya msingi Ipogolo wakitaka kukutana na vijana wa eneo hilo ili mjumbe huyo aweze kumuunganisha mgombea ubunge wa jimbo hilo Monica Mbega na Mwakalebela japo mkakati huo uligonga ukuta.

Kabla ya msafara wa Ridhiwani kufika shuleni hapo kwa ajili ya kikao chake cha ndani ya vijana wa CCM kwa lengo la kuvunja makundi ndani ya chama hicho, aliyekuwa mmoja kati ya wana CCM 12 walioingia katika kinyang'anyiro cha ubunge jimbo hilo, Msambatavangu, alipita mitaani kujaribu kuwaomba vijana kwenda kumsikiliza mtoto huyo wa Raisi Kikwete japo waligoma kwa madai kuwa hawadanganyiki na ujio wake.

Hata baada ya vijana hao wa vijiweni kugoma kwenda katika shule hiyo kwa ajili ya kutana na mjumbe huyo kwenye chumba cha darasa la pili katika shule hiyo ya msingi Ipogolo, bado msafara huo ulifika katika eneo hilo kwa ajili ya mkutano japo idadi ya vijana waliokuwa wamefika ilikuwa ni kama vijana 10 pekee.

credit: Francis Godwin
Picture
Darasa la S/Msing Ipogolo lililokuwa limeandaliwa kwa ajiliya kikao cha UV-CCM
YOTOKANAYO...

Vyombo mbalimbali vya habari vimesharipoti na kulaani mkanganyo unaofanywa katika kampeni za Kisiasa, ambapo chama kilichoko madarakani kinatumia mwanya huo kushindwa kutofautisha shughuli za Kisiasa za Chama na shughuli za Kiserikali. Magazeti yamesharipoti kuhusu Wafungwa kutumiwa katika ujenzi wa majukwaa ya kisiasa na hivi jana imeripotiwa habari ya Wanyamapori kuwindwa ili kuwapatia kitoweo walioongozana katika shughuli za Kisiasa za Chama, na katika wananchi wakauziwa kitoweo (kuzuga?).

Wanaofanya hivi wanafanya kusudi ili kuonesha kuwa wao ni "mwamba" na hakuna wa kuwafanya lolote?
Wanafanya dharau, au ni kwamba hawafahamu kuwa wanalofanya ni kosa?

Kama si dharau  ya umuhimu wa elimu, ni kwa nini mikutano ya kisiasa iendeshwe mashuleni? Juzi tu hapa tumeshangazwa na kitendo cha wanafunzi kutokuingia madarasani, ati wanasubiri msafara wa mgombea uraisi upite? Ama, kwa utaratibu upi jama? Mbona hatuna heshima kwa mambo ya msingi kama elimu?

Mimi kinachonifurahisha ni kwamba, wananchi wameshaona huu sasa ushakuwa ujinga. Hizi ndizo chokochoko zinazoamsha hasira na kusababisha watu watwangane makonde... na zaidi ya hapo. Haya!
 


Comments

Kenny
29/09/2010 10:23

Mimi nilishasema huyo Ridhiwani Kikwete na hata mamaye Salma ni akina nani katika Taifa letu hata watoto wasiingie madarasani kwa ajili ya ziara zao.Si wangemwachia kampeni baba yao afanye? Ikulu pana biashara gani? Mwl Nyerere aliwahi kuuliza.

Reply
Advocate Jasha
29/09/2010 13:20

CCM wacheni kuwasumbua watoto wadogo katika kampeni zenu.Watoto ambao hawajafikia umri wa kupiga kura,nendeni vyuo vikuu huko kuna mizani ya kuupima upupu wenu.MUNGU IBARIKI TANZANIA

Reply
Mnoko
29/09/2010 13:38

siku zao zinahesabika

Reply
29/09/2010 13:43

Haya ndiyo maneno,kule Ngeza nako kumekucha. Tumechoka na dharau za waziwazi, heri kuingia msituni kuliko kutawaliwa na viongozi na watoto wao. Hii ni dharau kubwa kwa watanzania, Tanzania ni nchi huru wala siyo kampuni binafsi ya mafisadi na vigogo wa chama tawala.

Reply
29/09/2010 14:36

Sahihisho, Nzega badala ya ngeza.

Reply
kim
29/09/2010 16:23

no comment, Tanzania ni zaidi ya uijuavyo

Reply
Duh
29/09/2010 18:46

Hatutasubiri historia iwahukumu, Malipo ni hapa hapa tu. mimi hao chichiemu wananiboa sana. Kazi ni kuwalazimisha wanafunzi wa shule za msingi manake hao hawajui chochote, ili wajaze viwanja vya mikutano. Wanalazimika kufanya hivyo kwakuwa baadhi ya wananchi wanapokea hizo TSH 2,000/= wanazohongwa na hawatokei kwenye magari yanayowawaisha kwenye mikutano.

Reply
29/09/2010 23:45

Wananchi wameshachoshwa na mambo yao ndio maana wanatimuliwa, Baba, Mama na mtoto wote kampenini na ndege za kukodi, CHICHIEM HAMNA SERA, Mm! Ambada umelewaaa!!!tehe tehe!! wasingekimbia wangeambulia ngeu, tumechoshwa na UFISADI,

Reply
Prince Can
30/09/2010 03:35

Saaaaaaaafi Sana! Timuo wote hao

Reply
JUNIOR
30/09/2010 07:24

CCM kubalin kwamba Watanzania wamewachoka hat aktitumia mpaka wajukuu zake kumfanyia kampen kama hawamtaki ndo hivo

Reply
30/09/2010 07:35

Ninyi nyote mliotoa maoni yenu hapo juu, nina hakika sio Watanzania

Ni Warundi, Wanyarwanda, Waganda, Wakenya au wale watu wanaotoka kwenye nchi za shida, watu wanoona kuuana ni jambo la kawaida kwao.

Kama kweli ninyi ni Wabongo ni VIHIYO wakubwa. Nendeni hospitali kupima akili zenu, kwani inaonyesha mnaumwa bila ninyi kuelewa.

Itakuwaje kweli Mtanzania mwenye akili timamu awaze kuingia porini ili arudi kumwua Mtanzania mwenzake? Kwa vile tu yeye (mwuuaji) ana itikadi za chama kingine?

Wote walioandika hapo juu wanaishi nchi za nje kama ninavyowafahamu mimi hao Watanzania wawili, japo sina hakika kama ni kweli ni Watanzania ni "Malkiory" na "Kenny".

Tanzania ikipata balaa la kuvunjika kwa amani, Watanzania hao wawili, wao watakuwa wakila kuku kwa mirija huko waliko. Kuweni makini nao.

Toeni maoni yenye kushawishi wapiga kura kutokakana na sera ya chama unachokipenda, sio kuropoka eti huyu mtoto wa Rais, tumechoka kuongozwa na CCM. Hakuna anayewalazimisha Watanzania kuichagua CCM, ni watu wazima na akili zao ndiyo wanaoipigia kura CCM, ikiwa ni pamoja na wazazi wa hao wanaotoa maoni yao hayo juu, yanayofanana na watu wanaokunywa supu za utumbo kilabuni na maoni yao ikiwa ni utumbo mtupu kama tunavyoona hapo juu.

It's Great To Be Black=Blackmannen

Reply
Mtanzania
30/09/2010 08:14

Blackmannen:::::::: samahani ila napenda nikuambie huna sera na watu kama wewe ndo wanaopotosha jamii. hebu angalia hapo juu watu wameongea mambo ya msingi kama kutositisha vipindi mashuleni na kuthamini elimu wewe unakuja hapa na kusema walioandika hapo siyo watanzania. mi nafikiri wewe ndo siyo mtanzania maana hujui kinachoendelea. kama huwezi changia kitu na kutathmini mambo basi kaa pembeni maana huyu Dada yetu Subi mwenye hii site anatumia muda wake mwingi na analipia hela japo toka mfukoni kwake, kwa vile ni mtanzania.

Tafakari na upembue usiwe mshabiki tu!!! na ukiwa mshabiki uwe na ushabiki wenye manufaa ya watanzania siyo yako! Umeniudhi kwa kweli nasema toka moyoni.

Reply
Hashim
30/09/2010 11:14

Huyo Ridhiwani ni shQga tu na aondoke zake,Tanzania si nchi ya kifalme itawaliwe na Baba ,Mama na mtoto.Pumbavu zake

Reply
Lulu
30/09/2010 14:23

Blackmannen!

Jina lako lenyewe linakutambulisha kama wewe ni punguani au umetumwa.

Mtanzania halisi tangu lini akajiita hilo jina. Watu wanaposema watakwenda porini cha ajabu ni kipi? Mbona unaiheshimu Zimbambwe kama wewe CCM ambayo inaua watu kila siku? Mbona unaifagiria Sudan nakuiiunga mkono wakati Janjawidi wanaua watu kila kukicha? CCm ndo inaenda mpaka UNO kumtetea Rais wao pamoja na Mgabe. Je hapo CCM si inachangia kumwaga damu?

Tumia akili na utafakari uyasemayo. Au unaona Bora TZ iendelee kuwasaidia wauaji ili mradi mTZ abakie maskini na wachache wawe wafalme? Wewe unayeongea yawezekana ndo umepewa shati la kijani au tshirt ya njano na unaogopa usije ukaaibishwa na hao mafisadi wako.

Walikuwepo akina MOi wako wapi? Akina Chiluba si walishindwa? Wako wapi akina Blair je damu ilimwagika? Bush?

Acha ujinga. Omba Chadema au CUF ziingie ndo upate elimu ya bure tuliyoipata wakati wa Mchonga.

Reply
kulwa
30/09/2010 22:46

We Blackmannen ni shoga tu, nadhani huyo kikwete na familia yake wamekuoa
Wanaochangia ukurasa huu wanatoa hoja zao za msingi kuhusu tanzania, kwa nini uwaite si watanzania?

Una macho lakini huoni, ni wapi uliona Familia inafanya kampeni za baba yao?

Una masikio lakini husikii kwamba watanzania tumechoka na danganya toto ya huyo kiwete wako?

Una akili lakini hazifanyi kazi kwa vile wewe in shoga wa RIDHIWANI

Kumbuka sisi watanzania tuna uchungu na mali za nchi yetu, hatutakubali hata second moja kukaa kimya wakati familia ya kiwete na CCM wanaiba na kula matunda ya tanzania, tuko tayari kumwaga damu hasa ya watu kama BLACKMANNEN NA WENZAKO.
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA UTUONDOLEE KIWETE NA CCM YAO

Reply



Leave a Reply