Mimi Francis Godwin, mmiliki wa blog na mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, napenda kuelezea masikitiko yangu kwa wale wote ambao wameendelea kunipigia simu za vitisho kuhusiana na habari ya "RIDHIWAN KIKWETE AVAMIWA NA VIJANA WA CHADEMA ASHINDWA KUFANYA KAMPENI". Ijapokuwa sijapokea simu ya wahusika wenyewe, wapambe wa nje wameendelea kuwa na nguvu hata kutoa vitisho dhidi yangu kuwa iwapo nitaendelea kujifanya mkweli siku zangu zinahesabika.
Picture
Francis Godwin
Napenda kupingana na wote walionipigia simu nakutoa vitisho kama hivyo huku nikiamini kuwa kifo kwangu ni mipango ya Mungu na sitaogopa wala kuingia katika dhambi ya kusema uongo kwa jambo la ukweli, hivyo ni heri kuteswa hata kufa kwa kusema ukweli kuliko kuliangamiza Taifa langu kwa kuendekeza rushwa na kusema uongo kwa faida ya wachache.

Pia ninapenda utambue kuwa habari hii iliyopewa nafasi ya mbele katika gazeti la Tanzania Daima la Septemba 30, 2010 huu ndiyo ambayo imeonekana watu hata wale ambao ni rafiki zangu wakubwa na viongozi wangu ninao waheshimu zaidi kuninyoshea vidole na bila uchunguzi wakinituhumu kuwa mimi ni CHADEMA.

Japo si dhambi kuwa CHADEMA wala chama chochote cha siasa kwa Mtanzania, ni vema watambue kuwa mimi ni kada wa CCM na nimepata kugombea ubunge kupitia CCM na ni mjumbe wa halmashauri ya CCM wilaya ya Iringa Vijijini.

Taaluma yangu haina chama, dini wala kabila.
(Endelea kusoma zaidi katika blogu yake - bofya hapa)

Yatokanayo...

wavuti.com inakemea na kulaani vikali tishio lolote kwa raia yeyote wa nchi hasa kwa wanataaluma, hususan, wanataaluma ya habari ikiwa habari wanazoziandika ni za ukweli. Tumeshuhudia waandishi wengi wa habari toka Afrika, Asia, Ulaya na Urusi, wakitiwa katika misukosuko na wengine wao wakipoteza uhai, kwa kuwa tu wameripoti na kuchapisha habari zisizopendwa na baadhi ya watu.

Tunakemea jambo hili na kuwakumbusha wale wote wenye mawazo ya kuficha ukweli kwa vitisho kuwa kamwe haitawezekana kuuzuia ukweli. Kutisha au kuua mtu si suluhisho. Watanyanyuka wengine. Waliotishwa na hata kuuawa, haikuwa mwisho wa kuripoti habari. Watakapoondoka hao, watainuliwa wengine na kuchipua. Ni roho iliyo hai. Kamwe haifi, bali hunyanyuka kwa mwingine. Hilo mlifahamu.

Pole sana Francis Godwin kwa usumbufu unaoupata.
Inshaallah, twashukuru kuwa hukumu ya haki hutoka kwa Mwenyezi Mungu.

 


Comments

KULWA
30/09/2010 22:58

Pole sana FRANCIS GODWIN,
kama lilivyo jina lako GODWIN yaani Mungu ameshinda, NAAMINI MUNGU YUKO PAMOJA NA WEWE NA SHETANI YUKO PAMOJA NA HAO wanao kupigia simu za vitisho,

Watanzania wote tuko nyuma yako na hongera kwa uchambuzi wako mzuri pamoja na kuwa mkweli ingawa wewe ni wa CCM, nawaomba wana CCM wote wawe na moyo wa ujasiri kama wako wa kudhubutu ili tuiokoe Tanzania kutoka mikononi mwa MAFISADI

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA FRANCIS GODWIN, LAKINI UTUONDOLEE MAFISADI HAWA WA CCM.

Reply
Kenny
01/10/2010 11:05

Kudadadeki, pole sana ndugu yangu Francis Godwin.Sasa ndio utambue kuwa Ridhiwani Kikwete anaandaliwa na babake kurithi taifa letu la Tanzania. Hizo simu za vitisho kwa ajili ya kuandika taarifa za kuzuiliwa kwake kufanya mkutano zinatoka wapi? Mimi nlisema Ridhiwani ni nani Tanzania, na hiyo UVCCM ina nafasi gani ya kikatiba katika Taifa letu? Sijui kama unajua kuwa sasa hivi ukienda pale Ikulu hutamkuta Mama, Baba na wala watoto, wote wako kwenye kampeni mikoani wakitumia fedha za walipa kodi.Maisha sasa hivi bongo ni magumu, hela yote iko kwenye kapmeni ya CCM. Kwani wewe ukiwa CHADEMA ni nongwa? Huko CCM walikubatiza UBATIZO mtakatifu na ukiamua kutoka ni dhambi? lo!

Reply
lusumanguo
01/10/2010 12:54

Mzee wa Matukio Francis Godwin, nakupa pole sana kwa vitisho hivi. Ninaandika kutoka Rome, Italy kulaani vitisho hivyo. Nikiwa mtanzania ninasema kuwa siyo haki kwa waandishi kutishiwa kutokana na ukweli mnaouandika. Hawa mashabiki au wakereketwa wa CCM kama waliona kuwa ulichooandika ni uwongo, basi wangekuja na hoja za kupinga ulichoandika, siyo kutisha. Halafu huyo Ridhiwani Kikwete ni nani kwa taifa hilo mpaka afanye wanafunzi wakose masomo kwa ajili ya ujio wake? Hivi baba yake haoni uozo huo na kumkemea?? Nasema kuwa tuko watanzania wengi ambao tunaihate CCM kutokana na vitendo vyake na kauli yake... Hii ni aibu kwa CCM Iringa na RIdhiwani Kikwete. Pole sana.. tuko nawe katika ukombozi wa Tanzania kutoka kwa makucha ya hawa wasiojua mchezo wa siasa na uongozi.... wameumbuka mwaka huu!!! wajifunze alama za nyakati!!!
Lusumanguo... Roma, Italia

Reply
PMN, Bukoba
01/10/2010 23:07

Pole sana ndugu yangu Godwin kwa yaliyokusibu.

Mengi yatatokea, lakini hatima yake ni ukweli kuonekana na hila kujitenga. Mambo kama hayo hayatakiwi kabisa katika taifa letu tunalojidai nalo kuwa ni la amani na kidemokrasia. Demokrasia iko wapi? Kuna mtu nilimtumia sms ya kupigia debe CHADEMA, akasema rafiki, hizi sms zitakusanywa na CCM baada ya uchaguzi na kisha wahusika wote kutiwa mbaroni, nilimjibu kwa ufupi kwamba - To hell!!

Lakini ni lazima watu wachache waleta vuguvugu la mabadiliko wengine watafuata, hata ukombozi wa Afrika haukuja hivihivi, kuna watu wachache - mnakumbuka history!

Basi, Godwin, be strong enough usihofu, hizo simu ni za kupima msimamo wako, hawatakufanya lolote maana Mungu wako ndiye anayekulinda daima. Keep it up, na usiogope kwa ajili ya hayo - Bible says.

Kama niko sahihi kesho tarehe 4/10/2010 Bi Salma Kikwete atakuwa Bukoba kutafuta kura za mumewe, kwa fedha za nani? kama siyo zangu, wewe na yule mlipa kodi - mlalaoi anayetozwa ushuru kwa kuuza nyanya gulioni???????

Enough is enough, I call upon you readers to act, we need change before things contunue falling apart!!

Reply



Leave a Reply