
Tatizo la fistula inatibika ikiwa mhusika atafika hospitali.
Kutokana na asili ya tatizo hili, akina mama wengi hupatwa na soni na kushindwa kutafuta matibabu, hivyo ninaungana na Brenda, Dina na wengine wote katika kuwahimiza ndugu, jamaa na rafiki kuwashauri na kuwasaidia akina mama wenye fistula kwenda hospitali kwa ajili ya matibabu.
CCBRT inajitolea kugharimia usafiri, malazi, chakula na matibabu bure kabisa.
Ikiwa unalo tatizo, au unamfahamu yeyote mwenye tatizo hili, basi piga simu namba 0752 678263 POPOTE ULIPO na utaelekezwa jinsi ya kupata usafiri wa kufika hospitali ya CCBRT, Msasani, Dar es Salaam.
credit: Dina Marios blog


RSS Feed