Akiendelea na mikutano ya kampeni katika mikoa mbalimbali, akiwa mkoani Tabora katika Jimbo la Urambo Magharibi, Jakaya Kikwete amewataka Watanzania wamkumbuke kwa mambo 8 atakapoaga Ikulu 2015.

"Nimesema kuna mengi nayafanya, lakini nikimaliza kipindi changu nataka watu wanikumbuke kwa mambo nane... waseme Mungu amrehemu, yule bwana acha tu, amefanya kitu."
Picture
Jakaya Mrisho Kikwete
Mambo hayo aliyataja kuwa ni:

  1. Kuimarisha kilimo cha umwagiliaji kupitia mpango wa Kilimo Kwanza,
  2. Matumizi bora ya mbolea,
  3. Dawa za kilimo,
  4. Kutoa wataalamu na maofisa wengi wa kilimo.
  5. Kusaidia upatikanaji wa masoko kwa mazao ya wakulima,
  6. Kusimamia uwepo wa bei bora za mazao,
  7. Kuimarisha barabara ili wakulima waweze kusafirisha mazao kutoka vijijini
  8. Kuachana na jembe la mkono kutumia matrekta makubwa na madogo

Akasema, mengi yanahitaji misaada ya wahisani, yamo ujenzi wa barabara na miundombinu ya kisasa ya maji. Ndipo akapata na fursa ya kugusia malalamiko ya safari zake nyingi za nje ya nchi.

Alisema: "Wapo wanaosema nasafiri sana,  sasa ningekaa pale nyumbani kwangu nikamwangalia mke wangu Salma halafu nimwambie aisee ulivyopendeza, Watanzania wangekufa njaa na Wajapani wanaotaka kusaidia, leo hii wasingeijua Kaliua... "Sasa kuyapata yote haya, lazima nisafiri. Nilikuwa Marekani, nikakutana na wahisani mbalimbali; wenyewe wananiuliza wanataka wanisaidie wapi, mimi nasema hapa na hapa na pale... kuna watu wanapesa nyingi tu."

Soma habari nzima katika gazeti la Mwananchi

 


Comments

mayi
30/09/2010 23:38

unaacha kuangalia na kusimamia watendaji wako unaenda omba misaada nje?? kuomba kula nje ni kwa sababu ya EPA,richmond, migodi etc iliyo na usimamizi mbovu!Tz tuna uwezo wa kujitosheleza sana.Na pia katika yote aliyoahidi 2005,hayo 8 tuu ndo yalitotekelezwa kulingana na yy!.maji,elimu,afya,maisha bora yako wapi?? na still unaendelea kuahidi. am doubting of your promises my dear president!

Reply
GreatMAN
01/10/2010 01:26

JK Umetoa Jambo moja tu lenye vipengere nane, ambavyo navyo hakuna umeweza tekeleza hadi sasa. ustubabaishe

Reply
Kenny
01/10/2010 11:11

Nyie mtaona, akichaguliwa tu, safari yake ya kwanza Marekani kwa Obamma, ya pili Uturuki, ya tatu Jamaica kwenye muziki. Ya nne...!

Reply



Leave a Reply