Picha hii imenaswa na kamera ya McKepha akiwa ndani ya daladala, Tanzania.
|
|
Nadhani ilipaswa isomeke, "Abiria toa hela" lakin pengine maneno sahihi ni "Abiria lipa nauli", kwa maana ukimwambia abiria atoe hela bila makubaliano maalumu, anaweza kushindwa kuelewa atoe pesa ngapi. Picha hii imenaswa na kamera ya McKepha akiwa ndani ya daladala, Tanzania. CommentsFrank 19/10/2010 01:59
Hili ni tatizo la kielimu kubwa lililopo Tanzania kwa kuwa wachoraji(sign writers) wengi tulionao wameishia darasa la saba. 19/10/2010 13:11
Bwana Frank - inawezekana pia siyo tatizo la elimu bali ni athari ya lugha ya mama katika uzungumzaji wa Kiswahili Sanifu. Kwa mfano sisi Wasukuma tuna shida sana na kimadende [r]. Badala yake tunatumia kilainishi [l]. Wakurya ni kinyume chake (kura tumekura pa kurara je?). Eddo 19/10/2010 14:08
@Masangu Matondo Nzuzullima naomba uwatafute wataalamu wa lugha wakutofautishie kati ya maneno ya lugha ya kuandika na jinsi unavyotamka. 19/10/2010 14:21
Bwana Eddo; Muhd 19/10/2010 17:21
Tatizo ni kuwa hao waiokuwa hawajua matamshi mazuri ya Kiswahili wakiweza kuchoropoko kidogo na kufanya utafiti kwa kutumia lugha zao mama na wakapata PhD basi husema wao Kiswahili ni lugha yao mama. Nakumbuka kuna mama mmoja yuko US yeye utafiti wake kafanya kwenye Kichaga, na kapata PhD, naam. Lakini sasa anadai kuwa yeye Kiswahili ni lugha yake mama. Na anawaona waswahili kuwa hawajui lugha yao. Pia huthubutu kusema kuwa Kiswahili hakina mwenyewe.Lugha ya vitabuni ina tabu sana. Mnoko makini 20/10/2010 06:47
Bw Masangu Matongo, Leave a Reply |