Dondoo:
Matokeo ya utafiti huu pia yametamkwa katika taarifa ya habari ya TBC, ya saa mbili usiku leo, "tafiti huo ulifanywa katika mikoa 15 ya Tanzania bara, uliwahusisha watu 3047 na lengo la utafiti halikuwa kuonesha taswira halisi ya matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 31, bali kuwasaidia wagombea kujua maeneo zaidi ya kujikita katika kampeni kwa muda uliobaki kabla ya uchaguzi" - imesema sehemu ya Taarifa hiyo ya TBC.
Picture
L-R: Dk. Vicent Leyaro na Deus Steven Msechu katika hoteli ya Courtyard, Dar
Shirika lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na kutoa utafiti wa taarifa mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha wananchi maamuzi kwa uelewa la Tanzania Citizens Information Bureau (TCIB) limetoa taarifa ya matokeo ya utafiti wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais 2010.

Akizungumza na waadishi wa habari Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam idara ya Uchumi Dk. Vicent Leyaro amesema malengo ya TCIB ni kutoa msukumo kwa wananchi kushiriki katika harakati za kulinda na kendeleza misingi ya Demokrasia, Kutoa fursa kwa wananchi katika kutoa maoni yao juu ya mambo mbalimbali katika maisha na kujenga uwezo wa wananchi kwa njia ya tafiti na elimu katika nyanja za Serikali, siasa, Mambo ya Kimataifa, ulinzi, elimu na maadili.

Aidha Dk. Vicent Leyaro amesema washiriki katika kura hii ya maoni ni 3047 wenye wasifu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto chini ya darasa la saba, elimu ya Sekondari na elimu zaidi ya Sekondari ambapo katika utafiti huo asilimia kubwa ya vijana wamemuunga mkono mgombea urais wa CHADEMA Wlibrod Slaa na asilimia kubwa ya wazee wameonesha kumuunga mkono mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete.

Amesema Dk.Willbod Slaa ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa ya Kilimanjaro 71%, Arusha 60.4%, Manyara79.8%,  Iringa 58.2%  na Dar es salaam 42%

Ambapo raisi wa sasa wa Tanzania, Jakaya Kikwete ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa ya Dodoma 59.3%, Morogoro 56%, Mbeya50%, Rukwa54.3% na Ruvuma 55%.

Akihitimisha wakati akijibu maswali kwa waandishi wa habari Dk. Vicent Leyaro amesema utafiti haukuangalia wala kupendelea sehemu ambazo mtu anapendwa sana kuliko sehemu nyingine na uchambuzi wa matokea kimkoa yanaonyesha kuwa wagombea wawili Jakaya Kikwete na Dk. Willbrod Slaa wanachuana vikali baadhi ya mikoa na mikoa mingine kufanya vibaya.

Hata hivyo utafiti huu wa kura ya maoni kuhusu wagombea  Urais haukufanyika kwa upande wa Zanzibar japokuwa wananchi wa Zanzibar wanashiriki katika kupiga kura ya kuchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

PS: Deus Steven Msechu alimwakilisha mkurugenzi wa TCIB.

 


Comments

Kenny
15/10/2010 11:14

Ninyi utafiti wenu ni afadhali kuliko wale jamaa wanaoitwa REDET na SYNOVATE

Reply
Heri wanao sema ukweli juu ya hali halisi inayoendelea nchini hususan ktk kipindi hiki kuelekea uchaguzi.Msema kweli ndio mpenzi wa Mungu.
15/10/2010 12:42

Reply
Issa
15/10/2010 13:46

Kwa watanzania Matokeo haya yanaweza kupingwa na kinana and makamba tu kwa sababu wao wana lao jambo kwenye uchaguzi huu.

Reply
Mtanzania
15/10/2010 13:52

Wamechemsha kidogo kuchukua Waliochini ya umri wa kupiga kura

Reply
rama
15/10/2010 15:47

hapo sio kuchemsha kidogo ni either kuchemsha sana au changa la macho ili watu wa-relax kuwa slaa yuko juu!
hapo naona kama wamelenga "digital population" (jamiiforums type), sio wapiga kura!

Reply
mgombea mwenza
15/10/2010 17:27

Utafiti mzuri ni ule unaohusisha wapiga kura na si hata watoto ambao hawana uwezo wa kupiga kura kisharia. Huu ni uchakachuaji na tarehe 31 Oktoba si mbali uongo wa tafiti za aina hii utadhihiri!

Reply
DG
15/10/2010 19:26

hawa maprof wa statistics sijui waliupatia wapi huo u-phd? We have to regulate that professional like engineering, medicine, law & accounts

Reply
msakanyoka
15/10/2010 19:30

jamani dawa yao hao ni 31/10 ni kata mti panda mti

Reply
Ralph
15/10/2010 22:50

Habari ndo hiyo
Karibu rais wetu Dr Slaa ikulu.

Reply
Mzee wa Shoka
15/10/2010 22:54

Kikwete aanze kufunga mizigo aondoke na majini yake. Nguvu ya Mungu ndiyo inayohitajika Tanzania na sio ushirikina.

Reply
SISTER DUH!
15/10/2010 23:45

MI NAONA HUO UTAFITI NI WA HAKI KIASI CHAKE.NA HATA KAMA AMEHUSISHA WATOTO WA PRIMARY NAONA VYEMA PIA.KWANI WATOTO WA PRIMARY WANAREPRESENT WAZAZI WAO MAJUMBANI.KAMA BABA ANAONGELEA KIKWETE KUWA NI MZURI KILA KUKICHA BASI HATA MTOTO WA PRIMARY ATAJUA HIVYO NA HATA KWA DK.SLAA PIA.
NA NAONA BORA YA HAO WALIOWAJUMUISHA HATA WATOTO WA PRIMARY NA SECONDARY NA KUSEMA UKWELI KULIKO HAO WA REDET N SYNOVATE AMBAO WAO TAFITI ZAO UNAJUA NI ZA UONGO KABLA HATA YA KUANZA KUSOMA.LOL!

Reply
SISTER DUH!
15/10/2010 23:50

ISSA WEEE MAKAMBA HANA UJANJA HUO SAA HIZI SI UNAONA ALIVYOTULIA.YAANI KIMYAAA SLAA NI FULL KUMSHHHHHH!TOKA MAMBO YAKE YAWEKWE WAZI AMBAPO ALITAKIWA AWE JELA SASA NA KUENDELEA KUUGULIA VIBOKO VYAKE SITA NA VINGINE SITA ATAKAPOKUWA ANATOKA AKAMWONESHE MKEWE LAKINI NAONA AMETULIA SANAAAAAAAA...YAANI NASUBIRI KWA HAMU AFUNGUE TUU MDOMO DR.SLAA AMTOE NISHAI MAANA BABA NI MROPOKAJI SANA..

Reply
ca
16/10/2010 00:53

haaya yetu macho na masikio

Reply
angelo
16/10/2010 00:54

Huu ndio utafiti ambao umelenga vipengele muhimu ambavyo watz walihitaji kuvisikia kama kwa rika, maeneo, idadi ya watu, na percentage aggragate ya wanachama hisika.

Reply
TARIMO charley
16/10/2010 00:56

hii ni moja ya utaratibu mzima wa kampeini , hebu tusubiri tuone hali halisi hapo 31/10/2010

Reply
Mbomboka
16/10/2010 01:38

Hao wasomi Degree ziko miguuni

Reply
MBOMBOKA 2
16/10/2010 02:18

EH HEBU TUELEZE MBOMBOKA ZA KWAKO ZIKO WAPI? USIKUTE ZIPO SEHEMU MYINGINE MBAYA ZAIDI YA MWILI!

Reply
16/10/2010 02:58

Du!! kumbe na watoto wametoa maoni yao kuhusu uchaguzi, haya tusubirie siku hiyo tukapige kura kumchagua kiongozi atakayeleta maendeleo. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE

Reply
Mosha
16/10/2010 03:10

huu ndiyo mwelekeo kamili wa nchi.Kikwete aanze kufunga virago!

Reply
mtu makini
16/10/2010 06:07

WATU AMBAO HUKURUPUKA KUKOSOA BILA HATA KUSOMA NA KUDIGEST UTAWAJUA TU...
WAMESEMA LENGO LA UTAFITI HUU SI KUJARIBU KUTOA TASWIRA YA OCTOBER 31 BALI KUONESHA MAENEO AMBAYO CANDIDATES WANATAKIWA KUJIKITA ZAIDI ....

Reply
Mbomboka
16/10/2010 06:42

Mnapenda sana maneno EEEEEEEE Fanyeni kazi nyie!!! Kabla ya kuilaumu Serikali jifikirie wewe mwenyewe kwanza una mikakati gani ya kujikwamua kimaisha???? Uchaguzi utakuja utapita wewe utaongea utapita.

Reply
Duh
16/10/2010 08:48

Bondy Language za hawa TCIB zipo tofauti kabisa na wale Redeti na Sinvote. Kusanya jirani zako 5 uendekupiga kura siku 14 zijazo.

Reply
sabhai
16/10/2010 09:13

Haya majibu ya TBC ni upuuzi mtupu. Mbona hawakufanya hivyo matokeo ya REDET na SYVOVATE yalipotangazwa? ni wazi kwa sababu kikwete alikuwa anaongoza. TBC ni chombo cha umma lakini kimekuwa kikitumiwa na kikundi cha watu wachache (Kikwete na marafiki zake) kwa faida zao binafsi. Swahiba wa kikwete, Lowassa alipochomolewa uwaziri mkuu kakimbilia TBC. Juzi juzi alipotaka kujisafisha kabla ya uchaguzi kakimbilia TBC. TBC hata haikusumbuka kutafuta upande mwingine wa stori hiyo. wamemfungia milango Mwakyembe mara zote mbili kwa lengo la kuwalinda mshikaji wake Kikwete. Aibu kwenu TBC! tunajua nyie ni makuwadi wa Kikwete na washikaji zake tu. hatuwaamini tena!

Reply
Frank
16/10/2010 13:36

Ndugu sabhai,
Nafikiri hujaisoma taarifa yote au hujaielewa au ulisoma ukiwa umelewa hakika ulikuwa umelewa.

TBC sio waliofanya utafiti huu,TBC wao kama shirika la habari walipata taarifa za utafiti kutoka Tanzania Citizens Information Bureau (TCIB).Tanzania Citizens Information Bureau ni shirika lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na kutoa utafiti wa taarifa mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha wananchi maamuzi kwa uelewa(wavuti.com.

@sabhai,Utafiti huu haukufanywa na TBC bali ulifanywa na TCIB.Kwa hiyo hakuna haja ya kuwalaumu wasoma habari TBC,TBC ni kama chombo cha habari kingine like Mwananchi communication,ITV nk.Usikurupuke kutoa maoni bali soma vizuri habari na uielewe,habari yenyewe uko katika lugha ya kiswahili.Nina wasiwasi na elimu yako pia.

Reply
mkakanjia
16/10/2010 15:52

wote wezi watupu,tarehe 31 oct,tutaona uongo wa tafiti zenu,watanzania milioni 43 mkafanye utafiti kwa watu 3000?? haihitaji elimu ya degree kuuona ukichaa huo!

Reply
Ng'wanaMwamapalala
16/10/2010 19:17

Huwezi kulinganisha tafiti za Synovate na Tanzania Citizens Informations Bureau (TCIB) na kusema kuwa tafiti ya TCIB ni bora zaidi. Rejea hata mwandishi wa habari wa gazeti la mwananchi amekudokeza katika kifungu cha pili cha habari kama TCIB hawajulikana zaidi(siyo maarufu).Kabla hujaandika swala lolote jaribu kwanza kufanya uchunguzi. Ni afadhali kujua hujui kuliko kufikili unajua kumbe hujui.Data ziko wazi kwenye mtandao au tu upenzi na ushabiki wa chama ndio unahusika zaidi.Kwa kukusaidia zaidi angalia tofuti ya synovate, www.synovate.com. hili ni shirika kubwa la kimataifa linalokubalika kimataifa na linatumiwa na nchi na makampuni makubwa duniani katika tafiti zao mbalimbali. Mimi sikubaliani na tafiti zote(synovate, RADET na TCIB) lakini hatuwezi kuzizulu(dismiss). kama ni uchaguzi basi synovate wana uzoefu wa maswala kama haya zaidi ya RADET na TCIB na katika kigezo hicho data zao zitakuwa za msingi zaidi ya RADET na TCIB

Reply
PMN
17/10/2010 01:36

Hongera TCIB.

Naona utafiti huu unaleta mtazamo sawa na hali halisi ya kampeni juu ya Chadema. Hao wanaojiita Mtanzania, Mbomboka n.k. hawana tofauti na Kinana na Makamba. Kama hamtaki kubadilika na kuona mfumo wa nchi hii umepotezwa njia kwa maslahi ya wachache - CCM; mabadiliko yatawalazimisha nini kubadilika. Big up TCIB, PHD zenu nazikubali.

Reply
I. NDYEMA
17/10/2010 23:57

Utafiti wa REDET mara nyingi hulenga kuifurahisha CCM, lakini TCIB wameonekana kueleza hali halisi ilivyo. CCM kimebaki chama cha watu waliochoka ki-fikra

Reply
mkweli- halisi
18/10/2010 00:43

utafiti huo haujaonyesha mapungufu kama ya REDET na SYNO ambao umekuwa regulated na Salva wa ikulu,kwan umefanywa kitaaluma tafouti na ule ulio fanywa kwa kulenga kumfurahisha JM na wenzake

Reply
mkweli-halisi
18/10/2010 01:39

hivi we Ng'wanaMwamapalala unauwezo wa kuchambua kweli? uwezo wakufanya tafiti zilizo nzuri na zisizo nzuri, haulinganishwi na muda wa kufanya kazi! uchanga , kutofahamika ama pengine kutokupendelea chama, kusikufanye ukadharau utafitiu wa TCIB, Uwezekano upo mkubwa tu wa TCIB kuwa wakweli kwa kutumia watafiti wenye uweledi ukitofautisha SYNO, inayotumia wakenya wasio na elimu yakiutafiti nakuwabeza watafiti wa tz ambao wana shahada zao na kuweka wakenya wanaojua kiingereza pasipo kuwa waeledi! REDET mapungufu yake ni pale tu taasisi ya elimu inapotumika katika siasa na si uchambuzi wa mambo katika jamii! REDET haina uhalisi wa kitanzania!

Reply
my name
19/10/2010 02:34

hivi wamesajiliwa? wapi?

Reply



Leave a Reply