Ninapoandika habari hii, ninamsikiliza Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza (ITV) akitoa pongezi zake kwa raisi mpya wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

Rais Mteule, Dk. Shein kupitia CCM ameshinda kwa jumla ya kura 179, 809 sawa na 50.1% ya kura zote, il hali Maalim Seif kupitia CUF amepata kura 176, 538 sawa na 49.1% na zilizobaki ni za vyama vingine.
Maalimu Seif ameipongeza tume ya uchaguzi ya Zanzibar, ZEC, kwa zoezi la uchaguzi, lakini pia ametoa maoni juu ya mapungufu aliyoyaona hasa kuhusu shahada za kupiga kura na matumizi ya mabavu kwa mawakala wa vyama na watu mbalimbali wanapohoji na kutaka taarifa sahihi. Amemsihi Rais Mteule alishughulikie suala hilo. Kabla ya kuhitimisha hotuba yake fupi, Malim Seif alisema kuwa katika matokeo haya, "hakuna mshindi wala mshindwa" kwani washindi ni Wazanzibari na imani yake ni kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa italeta mafanikio nchini humo. Amemsihi Rais Mteule kuwaasa watu kuacha kubezana, kwani kufanya hivyo kunaweza kusabababisha mtafaruku. Baada ya kuzungumza, Malim Seif alinyanyuka na kumpa mkono wa pongezi Rais Mteule wa Zanzibar, 2010 - 2015, Dk. Ali Mohamed Shein.

Ilipofika zamu ya Rais Mteule kuzungumza, naye alitoa pongezi kwa Maalim Seif na kupongeza zoezi zima la uchaguzi jinsi lilivyoendeka. Pia ametoa ahadi ya kushirikiana na wote katika ujenzi wa Zanzibar mpya kwa mujibu wa maridhiano mapya ya uundwaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar.

JUMLA YA KURA ZILIZOPIGWA ni 364,924
KURA HALALI ni 358,815
KURA ZILIZOHARIBIKA ni 6109

DK ALI MOHAMMED SHEIN (CCM) amepata 179,809 sawa na 50.1%

MAALIM SEIF SHARIF HAMAD (CUF) amepata 176,338 sawa na 49.1%
SAID SOUD SAID (AFP) amepata 480
KASSIM ALI BAKARI (Jahazi Asilia) amepata 803
HAJI AMBAR KHAMIS (NCCR-Mageuzi) amepata 363
HAJI KHAMIS HAJI
(NRA) amepata 525
JUMA ALI KHATIB amepata 497

-------------

wavuti.com inakupeni HEKO WAZANZIBARI. Nakutakieni Zanzibari mpya yenye Matumaini mapya!
photo credit : Maulid Othman
 


Comments

01/11/2010 12:22

Wow!!!
That was tight!!!

Reply
Kinyogoli
01/11/2010 13:15


Kwa mambo ya kwetu Zenji huyo Mpemba mwenzetu Dr Shein ndiye anakuwa Rais wa kwanza kutoka kisiwa cha Pemba tangu 1964. Na amepata ushindi mnono ukilinganisha na waliomtangulia ambao walikuwa wanaambua 51 - 55%.

Reply



Leave a Reply