Kwa mujibu wa Taarifa ya Habari ya TBC saa mbili usiku, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha ametoa ufafanuzi kuhusu vurugu zilizotokea mkoani Arusha Januari 5 na kusema kuwa, Serikali itawakutanisha viongozi wa Kisiasa Mkoani Arusha kwa lengo la kutafuta suluhisho la mgogogoro  huo.

Waziri Vuai alisema Serikali inasikitishwa na tukio hilo na kwamba iliacha "hali tete" kuendelea bila kuingilia kati kwa kuwa katika "Nadharia na Taaluma ya Migogoro", kabla ya mgogoro wowote ule haujatatuka, ni lazima uachwe hadi ufike mahali ambapo wahusika wakuu wataamini kuwa lipo tatizo linalohitaji kutatuliwa, kwa kuwa, mgogoro ukianzakutatuliwa mapema, basi ile furaa ya kusikilizana huwa haipo kwani upande mmoja huwa hauoni wala kukubali kuwa lipo tatizo.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Siasa cha Wananchi, CUF, Prof. Ibrahim Lipumba akitoa tamko kuhusu kilichotokea Arusha amesema kuwa, Polisi wangetumia taarifa za kiitelijensia kuzuia vurugu ambazo 'huenda zingetokea kwenye maandamano hayo' na siyo kutumia nguvu kuzuia maandamano yenyewe.

Watuhumiwa 31 wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha, sita kati yao wamesomewa mashtaka yao wakiwa wamelazwa katika hospitali ya Mount Meru. Shitaka  kuu linalowakabili watuhumiwa hao ni "kufanya mkusanyiko bila kibali na kusababisha uvunjifu wa amani". Baada ya kusomewa mashitaka, Hakimu aliruhusu Watuhumiwa kupewa dhamana na Watuhumiwa wote 31 walitimiza masharti ya udhamini na kutoka korokoroni.

Jingine katika taarifa hii ni kutajwa kwa Wamiliki wa Dowans Tanzania Ltd., ambao ni Dowans Holding S.A, Costa Rica  na Portek Systems and Equipment (PTE) Ltd. Barua ya Wakala wa Usajili wa Kampuni (BRELLA) inawataja wakurugenzi kuwa ni Andrew James Tice - Canada, Guy  Picard - Canada, Gopalakrishnan Balachandaran - India,  Stanley Munai - Kenya, Hon Sung Woo - Singapore na Sulaiman Al Adawi - Oman.

1. Bofya kifute cha 'play' usikilize taarifa ya habari ambapo pia Serikali imezungumzia suala la Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala Tawi la Tanzania.

2. Sehemu ya taarifa ya habari ya Dira ya BBC kuhusu hali ilivyo mkoani Arusha, siku moja baada ya rabsha.
 


Comments

Amida
06/01/2011 18:02

Jamani msituchanganye tuambieni watanzania gani wana-share huko Dowans au kurahisisha swali Dowans walikujaje Tanzania, how did we know this people, where they came from, who introduces who, who has the share with the company, how did we get where we are, and where are we going? Lazima kuwe na accountability jamani what type of governance hii isiyo na transparency???

Reply
Mtanzania
06/01/2011 22:52

"inawataja wakurugenzi kuwa ni Andrew James Tice - Canada, Guy Picard - Canada, Gopalakrishnan Balachandaran - India, Stanley Munai - Kenya, Hon Sung Woo - Singapore na Sulaiman Al Adawi - Oman." KWELI WALIJUA WANAKUJA KUFANYA MAAJABU MPAKA WAKAJIPANGA MTU MMOJA KUTOKA NCHI MOJA (WHAT A COINCIDENCE?). HAWA WAKURUGENZI WANABIASHARA NYINGINE WANAYOFANYA PAMOJA JINSI WALIVYO AU WALIFAHAMIANA KWA AJILI YA HII TU? Hahaha, Mtu mmoja nchi moja! Huyu Guy Picard alikuwa mkurugenzi wa Songas (kipindi namfaham alikuwa na miaka 35. Ni kijana sana). Je aliunda kampuni ingine akiwa bado mkurugenzi wa Songas au alikuwa ameshajiuzulu? Atakubali conflict of interest foul?
Na hiyo Dowans tanzania ltd mbona hawajataja wamiliki wake? Mbona hao wamiliki walifichwa hivyo ndo wanatolewa sasa hivi? Kwani hata kama walikuwa wanapika documents kwa jiko la mkaa si singelishakuwa tayari siku nyingi?
Ni vema mliona mtutukane kabisa...DOWANS=DUWANZI (Yaan watanzania ni maduwanzi, haya bwana!)


from:

Reply
PMN
06/01/2011 22:54

Binafsi sina imani tena na majina hayo. Yamechakachuliwa!! Kwanini Mtu anayehisiwa kuwa mmiliki wa Dowans humu nchini atoe taarifa kwa vyombo vya Habari kwamba hahusiki na Kampuni hiyo siku chache tu zilizopita kabla Serikali kutoa taarifa hiyo??? Hizo njama na inaonekana Serikali na mfanyabiashara huyo walikaa pamoja kutoa Tamko la serikali, na kabla serikali haijasema akaanza yeye kujitetea halafu ndo serikali ikajifanya kumsafisha. Watanzania tunadanganywa mchana kweupe.

Reply
Fanikio,
06/01/2011 23:30

Tunaposoma Gazeti la Mwana-Halisi, linaoonesha kuwa wamo watanzania wanaohusika na DOWANS lakini katika majina aliyo yataja Waziri, hao watanzania hawamo. Je tumkubali nani kati ya Gazeti na Waziri?

Reply
jk
07/01/2011 00:02

hahahahahahahahahaaaaaaaaaa,
WAJAMANI NAWAOMBENI SASA MUWE WAVUMILIVU KWA MUDA WA MIAKA MITANO IJAYO,HAWA DOWANS NASHAURI WALIPWE HARAKA PESA YAO, IKIBIDI HATA KUWAONGEZEA NA RIBA ASILIMIA 89% YA BILIONI 189.
MIMI NAONA WATANZANIA WANAZO PESA NYINGI SANA,
NAZIDI KUWAOMBA WALE WA MLENGWA WA UPINZANI WATUWIERADHI MAANA TUNAVUNA MATONDA SAFI TULIYOPANDA OCT 31/2010

NAOMBA MTU ASILALAMIKE KWA HAYA YANAYOTOKEA NA MENGINE YA KUFANANA NA HAYA AMBAYO YATATOKEA MUDA SI MREFU.

KAMA YANAWAUMIZA DAWA NI KUIMBA WIMBO WA SIFA NA TENZI CCM JU CCM JU CCM JU, HII ITASAIDIA KUPUNGUZA MAUMIVU

NASHAURI MJITOKEZE KWA WINGI 2015 ILI TUPATE VIONGOZI WENYE UCHUNGU NA RASILIMALI ZA TZ


CHADEMA VIVAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

Reply
mhagama
16/01/2011 04:15

kama ni kuilipa dowans tulipe tu,maana hakuna wa kumfunga paka kengele kwa katiba iliopo.miminamini kitu kimoja ,kama selelii alikuwa hana mvuto kwa wapiga kura wananchi wake huko nzega kwa kuwa mshindi wa pili,mbona aliyekosa kuvutia kabisa mshindi wa tatu hata kwa wana ccm alipitishwa kugombea ubunge na akashinda?hapo tujue kwamba tutapiga kelele lakini tupo nje ya sheria za nchi,muhimu katiba ibadilishwe ili wananchi wawe na maamuzi.

Reply
moshi
16/01/2011 04:20

Haaa hii kali,ukitaka kusajiliwa brela mpaka ujulikane anuani zako zote,mbona hawa wamiliki wa dowans ni watu hawaishi hapa ni wageni wa mataifa mbalimbali,hakuna raia wa hapa bongo,na brela wamewasajili.kubwa zaidi ni pale waziri aliposhindwa kulitaja kwa ufasaha jina la yule mmiliki kutoka india,ilimlazimu acheke.maana alijua kabisa ni sanaa.

Reply
Thomas
27/01/2011 01:16

Washachakachua majina tayari ila sisi tunajua wamiliki ni JK, Rostam na Lowas

Reply
ibrahim
04/02/2011 07:17

hii nchi imeshauzwa naomba mh:rais atugee hayo mafungu yetu na sisi tuweze kula bata

Reply
Ommarizo
05/02/2011 04:31

IMEKAA VIBAYA HII DOWANS BADO HAIJATULIA!!! IMEKAA VIBAYA HII BADO HAIJATULIA!!IMEKAA VIBAYA SANA SERIKALI YETU!! SASA TUFANYAJE WEZENU!!!

Reply



Leave a Reply