Audio iliyopachikwa hapo ni ya kipindi cha pili cha Njia Panda ambacho ni mwendelezo wa "Uponyaji wa Loliondo" kilichorushwa na redio Clouds FM Jumapili ya tarehe 10 Aprili 2011.

Katika kipindi hiki, utayasikia majibu baada ya kupimwa ili kuthibitisha kauli ya dada aliyehojiwa katika kipindi kilichotangulia na kutamka kuwa anaamini amepona baada ya kunywa dawa kwa Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Ambilikile Masapila huko Loliondo kijijini Samunge.

Pia utayasikia majadiliano baina ya wataalamu wa sekta mbalimbali walioalikwa studioni ili kuzungumzia sekta husika zilizoguswa na 'uponyaji' wa dawa ya Mch. Masapile.

Mwendesha kipindi ni Dk. Isaac Maro.

Bofya kifute cha play hapo upate kusikiliza. Audio zipo mbili ili kutoa uchaguzi zaidi ikiwa moja italeta usumbufu wa kutokusikika. Ikiwa huwezi kusikiliza, tafadhali bofya hapa kujipakulia audio hiyo.
 


Comments

Mtanzania
14/04/2011 18:28

Viongozi wetu sielewi wanatupeleka wapi. Tunakwenda wapi? Hili bomu jamani! Narudia kusema kuna siku litalipuka. Science hapa inatakiwa si blablaa! Kweli nami nimeongea na watu wengi wanasema hata mweshimiwa fulani alienda kunywa kikombe kwa nini mimi nisiende. Jamii inapotoshwa kwa kutoelewa. Twasonga mbele au twarudi njuma? Jamani maendeleo hayaji kimiujiza hivi. Tunahitaji kufanya mambo ya kueleweka na kuyasimamia. Wananchi tumewapa viongozi kura kwa imani kuwa watatuongoza katika njia iliyo sahii. Mambo ya imani wakati mwingine yakae pembeni. Kibwetere alifanya nini? Viongozi tujirudi hata kama mlikunywa vikombe. Its time to stop it and be serious.

Reply
Alledros
14/04/2011 22:01

Mtanzania ninaafiki kabisa! Mpe Kaisari... Sasa inaanza kuwa biashara na campaign ya siasa tu.Nimefurahi na kukubali maneno ya Wavuti: heshima kubwa kwa wagonjwa na wandugu! Wapo katika hali ya pekee. Ila polepole na mambo ya “imani”: kiasi sawa, Mungu yupo na ana uwezo, lakini ukisukuma mno ni sawa na waganga wa kienyeji au wachawi!
Tunajua kwamba hata TZ inajaa mitishamba yenye properties ya ajabu:lazima kujua masharti katika matayarisho na utumiaji! Chukua kwa mfano “Aloe.vera”: inaweza kuponya magonjwa mengi makubwa mpaka cancer, magonjwa ya tumbo, kisukari, na mpaka kusaidia sana kwenye ugonjwa wa ukimwi. Sisi tumetumia sana toka zamani na kuona maajabu mpaka kupona kabisa hata vidonda vya tumboni na mengine. Na madawa ni mengi sana: Imani inasaidia kiasi chake!
Hata mimi nimetumia toka zamani na kuona uwezo wa dawa hii na nyingine ya mitishamba na kuwasaidia watu wengi tu na kuona makubwa, kama kupona vidonda mbalimbali kwenye miguu, kichwani na tumboni! Lakini tusichanganye mno na imani

Reply
X-Paster
15/04/2011 04:49

Mimi nashauri serikali iwe makina na maamuzi yake na haswa yanapogusa imani za watu binafsi, hii issue ya babu wa loliondo ni issue kubwa sana, kwa sababu watu wengi wanaonekana kutoa maamuzi amabayo wanakuja kuyajutia baadae...!

Hii kitu nimeizungumzia kwenye toleo lililo pita la wavuti: "Ulaghai wa Dawa ya Mchungaji Ambilikile Mwasapile". Kuna walio nipinga na kuna walio niunga mkono.
Nashukuru sana kuwa yale niliyo yazungumza kule hayatupwa mkono, watu wanapaswa kuchukua hatua sasa.

Reply
makundi
15/04/2011 11:45

thanks for sharing this audio stream.

Reply
15/04/2011 11:59

@ Alledros, shukrani sana kwa kutoa ushuhuda wa dawa na tiba inayotokana na matumizi sahihi ya Aloe Vera. Ni kweli na nimeshuhudia kuwa inatibu sana matatizo ya ngozi, shinikizo la juu la damu, vidonda vya tumbo nk. Nitaandaa dondoo mbalimbali zinazoelezea uwezo wa Aloe Vera kutibu magonjwa mbalimbali.

@makundi, You are welcome, even more thanks to Dk. Maro and CloudsFM, and thank you for listening.

Reply



Leave a Reply