Tumekuwa wazuri sana kwa kupiga kelele kwamba Serikali hivi, Serikali vile, Viongozi hivi, Viongozi vile, tukiendelea kuamini maneno yao ya 'kutuletea maisha bora' wakati ukweli ulio dhahiri ni kuwa, kamwe Serikali haitatuletea chakula mezani bali kwa juhudi za mikono yetu wenyewe.

Mifano hai ya juhudi zenye malengo ni kama mtaalamu Kanja wa masuala ya IT (Information Technology) ambaye alikuwa na ndoto za kununua gari zuri aina ya Audi, lakini punde fedha ya kununulia gari ilipopatikana, akabadili mawazo na kuamua kufanya ufugaji "ranch" na sasa anajiingizia faida ya shilingi za Kenya zaidi ya 400,000 (sawa na zaidi ya shilingi 7,000,000 za Kitanzania; shilingi 1 ya Kenya =  shilingi 18 za Tanzania) kwa shughuli ya ufungaji tu, mbali na mshahara wa ajira yake ya utaalamu wa IT.
Mwendelezo wa mahojiano ya Jeff Koinange na Douglas Kanja yanapatikana youtube (bofya hapa). Jeff pia amewahoji wafugaji wengine ni Njeri Gota (bofya hapa)  na John Gethi (bofya hapa).

Hakuna kazi yenye faida rahisi, lakini ukweli pia ni kuwa, kila mafanikio yanahitaji nia na juhudi.
 


Comments




Leave a Reply