Picture
Langa
Ifuatayo ni audio ya kipindi cha Njia Panda kilichorushwa hewani na Dk. Isaac Maro (akishirikiana na Dk. D. Maro) siku ya Jumapili Agosti 14, 2011 kupitia Radio Clouds FM.

Kwenye kipindi alialikwa Langa Kileo ambaye habari yake tuliisoma wiki iliyopita katika vyombo mbalimbali vya habari (unaweza  kubofya hapa kuisoma tena) pamoja na mwanamuziki kwa jina la kisanii "Kala Pina".

Katika kipindi hiki, Langa na Kalapina wanazungumzia juu ya matumizi ya dawa za kulevya, ilivyoanza, mwendelezo wa kuzitumia na hatimaye kufikia hatua ya kutaka kuachana na dawa hizo. Wanagusia magumu waliyoyapitia katika kujidahidi kuziacha dawa, mafanikio na mbinu za kuendelea kushinda.

Langa anatoa dondoo za kilichomwezesha kutimiza miezi 4 hadi sasa bila ya kutumia dawa hizo. Vile vile anaelezea malengo na mikakati yake ya mbeleni katika kuwasaidia vijana wanaotaka kuachana na dawa za kulevya.


 


Comments

14/08/2011 14:16

Mungu amsaidie kijana wa watu. Nimeumia sana na stori yake

Reply
Mc
15/08/2011 23:49

Asante Langa kwa kutueleza kuhusu hili, nimejifunza mengi japo machozi yamenitoka. Mungu ni mwema na atakusaidia,ninakuombea.

Reply
Aggy
16/08/2011 00:55

inauma sana ila mungu aendelee kukupa nguvu utafanikiwa tu!

Reply
Mama Jose
17/08/2011 02:44

Nimefurahishwa sana na huyu kijana, 1. kwa kuomba radhi kwa wananchi, 2. Kusema kwa umma kukiri matatizo aliyokuwa nayo na kusema huku anakoenda siko. Yaani inaonyesha jinsi gani amekomaa kiakili. Pia asiache kumuomba na kumshukuru mwenyezi mungu kila wakati jinsi ya kupambana na haya maovu. Kwani haya ni mapambano katika maisha kwani mwenyezi mungu ana sababu zake naona alitaka wewe uwe good Embassador katika haya matatizo. Kuwakomboa vijana wenzako. Mimi ni mtu mzima nashukuru umenipa bonge la somo. Yaani mwanangu au mdogo wangu usimwache mwenyezi mungu hata mara moja uwe ni mtu wa kuongea na mwenyezu mungu kila wakati. kila la Kheri

Reply
Priscy
17/08/2011 05:02

Mdogo wangu nakupa big up endelea na moyo huo huo wa kubadilika na kuwabadilisha wengine, Unajua hivi karibuni niliona vijana wanatumia mambo haya lakini nikaumia sana moyo wnagu na kuingia hamu ya kuwauliza lakini nilishindwa kutokana na kuona kuwa kunauwezekano wakachukua na wasipende vile nitakavyowambia. Ila namwomba Mungu anisaidie kuniwezesha alau siku moja nimwongoe kijana kama wewe ulivyoweza kujiokoa katika shughuli ile. Yaani unamwona hasa kijana masikini anakuwa mzima kabisa kabisa mara tu anachenji na kuanza kusinzia na kutoka madenda lakini vyote hivyo ni vishawishi visivyo na msingi. Nakuomba ndugu yangu uendelee kutoa somo kwetu na kwa ndugu zetu ambao wameshaanza shughuli hii Mungu awasaidie kuwaokoa. Inasikitisha . Hongera kwa maamuzi mazuri uliyochukuwa kwani wewe ni nguvu ya Taifa.

Reply
RBS
29/08/2011 11:00

PRAISE THE LORD, ALL THE BEST.

Reply
Asali
02/09/2011 22:37

Haleluijaaaah

Reply



Leave a Reply