Picture
Zamani ikijulikana kama kisukari kisichotokana na upungufu wa INSULINI (non-insulin-dependent diabetes mellitus (NIDDM) au kisukari kitokanacho na umri na mfumo wa maisha, hasa ulaji na unywaji  na ukosefu wa mazoezi (adult-onset diabetes).

Aina hii ya kisukari ni rahisi kuondokana navyo, japo inahitaji elimu na umilivu kuhusu  aina gani ya chakula na kinywaji mtu anapaswa kula na kunywa bila kusahau umuhimu wa mazoezi angalau dakika zipatazo 30 kwa siku.

Siku za karibuni kumekuwa na vifo vingi vinavyochangiwa na  maisha ya kiselule (Sedentary lifestyle ) yaani kula na kunywa chochote kile bila ya mazoezi, MKAZO ( STRESS), unyogovu (Depression). Ushauri wa kitabibu unatuambia kuwa kula kiwango kidogo cha chakula sahihi kila baada ya masaa manne ni tiba ya aina hii ya kisukari. Watu wengi hasa waliopo kwenye tabaka la juu yaani wenye fedha wemekuwa wakihangaika kutafuta wachawi wa afya zao bila kujua kuwa ulaji unaopitiliza bila ya kujua madhara yake ndiyo MCHAWI namba MOJA.

Utanachotakiwa kufanya, kama utapenda afya yako iimarike, achana vitu vyakula aina ya wanga, mfano wali mweupe n.k , punguza  matumizi ya  chumvi, ulaji mikate aina nyeupe, unywaji pombe na ulaji wa matunda yenye sukari nyingi.  Japo inaonekana ni adhabu kidogo lakini kama  utazingatia basi ujue kuwa utaangamiza kabisa  aina hii ya kisukari.

Matumizi ya vyakula vilivyotajwa hapo pamoja na kula kiwango kibwa cha chakula na muda mrefu kupita kiasi baada ya mlo hadi  mlo, hufanya sukari kupanda na kushuka ( BLOOD SUGAR FLUCTUATIONS), na zaidi kuongezeka kwa uzito, kitambi na mwishowe kuishia kwenye msukumo mkubwa wa damu  ( HIGH BLOOD PRESSURE) na hata mashambulizi ya moyo ( HEART ATTACK).

N.B: Vyakula vinavyoshauriwa ni kama vile wali wa kahawia ( BROWN RICE), Mkate kahawia ( Brown bread) , njegere, karoti, samaki  na nyama aina zote ni safi. Bila kusau kunywa maji angalau lita mbili kwa siku.

Imeandikwa na:

Malkiory William Matiya
Cell phone: +358458628448
Email: malkiory@gmail.com
Website: www.malkiory.com 

 


Comments

10/01/2012 00:15

It is in point of fact a great and helpful piece of info. I am glad that you shared this useful information with us. Please stay us informed like this. Thanks for sharing.

Reply



Leave a Reply