Aina hii ya kisukari ni rahisi kuondokana navyo, japo inahitaji elimu na umilivu kuhusu aina gani ya chakula na kinywaji mtu anapaswa kula na kunywa bila kusahau umuhimu wa mazoezi angalau dakika zipatazo 30 kwa siku.
Siku za karibuni kumekuwa na vifo vingi vinavyochangiwa na maisha ya kiselule (Sedentary lifestyle ) yaani kula na kunywa chochote kile bila ya mazoezi, MKAZO ( STRESS), unyogovu (Depression). Ushauri wa kitabibu unatuambia kuwa kula kiwango kidogo cha chakula sahihi kila baada ya masaa manne ni tiba ya aina hii ya kisukari. Watu wengi hasa waliopo kwenye tabaka la juu yaani wenye fedha wemekuwa wakihangaika kutafuta wachawi wa afya zao bila kujua kuwa ulaji unaopitiliza bila ya kujua madhara yake ndiyo MCHAWI namba MOJA.
Utanachotakiwa kufanya, kama utapenda afya yako iimarike, achana vitu vyakula aina ya wanga, mfano wali mweupe n.k , punguza matumizi ya chumvi, ulaji mikate aina nyeupe, unywaji pombe na ulaji wa matunda yenye sukari nyingi. Japo inaonekana ni adhabu kidogo lakini kama utazingatia basi ujue kuwa utaangamiza kabisa aina hii ya kisukari.
Matumizi ya vyakula vilivyotajwa hapo pamoja na kula kiwango kibwa cha chakula na muda mrefu kupita kiasi baada ya mlo hadi mlo, hufanya sukari kupanda na kushuka ( BLOOD SUGAR FLUCTUATIONS), na zaidi kuongezeka kwa uzito, kitambi na mwishowe kuishia kwenye msukumo mkubwa wa damu ( HIGH BLOOD PRESSURE) na hata mashambulizi ya moyo ( HEART ATTACK).
N.B: Vyakula vinavyoshauriwa ni kama vile wali wa kahawia ( BROWN RICE), Mkate kahawia ( Brown bread) , njegere, karoti, samaki na nyama aina zote ni safi. Bila kusau kunywa maji angalau lita mbili kwa siku.
Imeandikwa na:
Malkiory William Matiya
Cell phone: +358458628448
Email: malkiory@gmail.com
Website: www.malkiory.com


RSS Feed