Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi (wa tano mstari wa mbele kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Kamati ya Saidia Taifa Stars Ishinde, Ikulu, Dar es Salaam, iliyotwaa ubingwa wa Chalenji 1994, Nairobi Kenya. Katika picha hii wamo pia wanahabari walioripoti fainali hizo.

Kutoka kushoto mstari wa mbele ni; Mpigapicha Richard Mwaikenda (gazeti la Mfanyakazi ambaye kwa sasa ni Mpiga picha Mkuu wa gazeti la JamboLeo na Mmiliki wa BLOGU YA KAMANDA WA MATUKIO), Steven Kuwayawaya, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, aliyekuwa Waziri wa Elimu na Michezo, Profesa Phillemon Sarungi, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Soka Tanzania (TFF), Muhidin Ndolanga, Marehemu Moses Nnauye wa CCM, aliyekuwa Mpigapicha Mkuu wa Daily News na Muhidin Issa Michuzi (sasa ni Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais). 

Mstari wa katikati kutoka kushoto ni; John Hokororo (gazeti la Majira), aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Makame Rashid, James Nhende (aliyekuwa Mhariri wa Michezo gazeti la Mfanyakazi),aliyekuwa mwandishi wa habari za michezo gazeti la Uhuru, Godfrey Lutego (hivi sasa ni Mkuu wa Kitengo cha Matangazo gazeti la Jambo Leo), Japhet Sanga (alikuwa mwandishi wa gazeti la Daily News), aliyekuwa Meneja Usambazaji wa gazeti la Mfanyakazi, Richard Ndasa (sasa ni Mbunge wa Sumve, aliyekuwa Katibu Mkuu wa FAT, Ali Mwanakatwe, Aliyekuwa Mpiga picha wa Mfanyakazi, Deus Mhagale (sasa ni mpiga picha wa gazeti la Mtanzania), aliyekuwa Mhariri wa Michezo wa Daily News na Katibu Mkuu wa Kamati hiyo, Stephen Rweikiza na aliyekuwa Mpig apicha wa gazeti la Mfanyakazi, Joseph Senga (sasa ni Mpigapicha Mkuu wa Tanzania Daima). 

Wengine msitari wa nyuma kutoka kushoto ni; Mwandishi wa habari Msangi na Evarist Mwitumba ambaye ni Mhariri Mkuu wa gazeti la This Day .

picha via blogu ya "Kamanda wa Matukio" Richard Mwaikenda
 


Comments




Leave a Reply