I just don't have evidence but I am sure move za hospitali kukusanya wagonjwa na kuwapeleka India zitakuwa driven by this payment system, I bet our officials may also be involved.
And these people are serious about that business, Apollo wanaanza kuwapa huduma wagonjwa Dubai, so from the airport you start getting services.
And the practice is made in such a way unafanyiwa vipimo vingi kadiri inavyowezekana, including those you don't need, the aim being to maximize the cost.
I am posted at Christian Medical College Hospital in India, this is a hospital which is not business oriented, but it is the best cardiology centre in India, it is one of the best nephrology centre in India also, iko Tamil Nadu km 120 kutoka Chennai.
The cost of services here is 1/3 ya gharama za Apollo and the like, the cost is even cheaper as compared to cost of some services in Nairobi (kuna mgonjwa alikuwa na leukemia Nairobi, gharama ya matibabu Nairobi ilitosha kulipia usafiri, matibabu gharama za kuishi hapa Vellore na akabaki na change), but guess what, no one is referring patient to CMC even in India itself because this hospital does not entertain the system of pay back!!!!!
It is very sad in deed!
YATOKANAYO...
Kwa hivyo, ujumbe huu unaweza ukawa umetufungua macho wengine tuliokuwa tukikuna vichwa kujiluliza kulikoni? Vipi "kutiririka" kwenda India kwa matibabu kwa viongozi wetu kunashamiri na kushika kasi hivi?
Mimi kwa mfano nilijiuliza:
Je! Hii inatokana na wagonjwa hao kukosa imani na tiba toka kwa wataalamu wetu? Kwamba, wanahisi wanapewa tiba isiyo na kiwango?
Au ni imani ya kasumba ya kujitakia au kufuata mkumbo tu kwamba matibabu ya "mzungu" au "mhindi" ama "mchina" yanaponesha vyema na haraka zaidi kuliko yale ya "mbantu" mwenzetu?
Hatuamini wala kuuthamini utaalamu wa wataalamu wetu?
Ikiwa madai yao kwamba wanakwepa huduma hafifu na mbovu, je, hawa viongozi wanaokuwa wepesi kutaka matibabu nje ya nchi, wanakosaje akili ya kuwawezesha wataalamu wetu kwa vifaa na mazingira bora ya kazi kwa kutumia fedha hizo hizo wanazozipeleka "India" ili nasi Watanzania tujivunie Watalaalamu wetu, wananchi wa kipato cha chini nao wasioweza kwenda "India" nao wapate nafuu ya tiba nzuri? Mbona tunadharauliana hivi? Umewahi kujiuliza ni kwa nini Watanzania wengi wanaohama nchi na kuajiriwa nchi nyingine wanasifika kwa uchapa kazi wao lakini wakiwa Tanzania walidharauliwa hata pale waliposhauri yaliyo ya haki? Ama ndiyo "Nabii hakubaliki kwao?"
Fedha wanazolipwa viongozi wetu hawa si zinatokana na kodi za wananchi na rasilimali za mumu humu ndani jamani? Sasa badala ya kuzizungusha humu ndani, ni kwa nini zinapelekwa kunufaisha mataifa ya nje?
Ama yote hayo hayana maana kwa kuwa fedha zenyewe, haziendi "nje" kweli bali zinazunguka na kurudi mifukoni mwao?
Hii nchi hii, ukisikia "pa" ujue ndiyo hivyo tena...!


RSS Feed