Jeshi la polisi Mkoani Ruvuma linamshikilia Frank Jota (26) mkazi wa kijiji cha Litisha Wilayani Songea kwa tuhuma za kumbaka mama yake mzazi mwenye umri miaka 54 ambaye jina lake limehifadhiwa wakati amelala nyumbani kwake majira ya saa za usiku.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo limetokea Januari Mosi mwaka huu huko katika kijiji cha Litisha kilichopo nje ya mji mdogo wa Peramiho.

Amesema kuwa usiku wa siku hiyo, Jota alikwenda nyumbani kwao ambako alimkuta mama yake mzazi akiwa amelala na baadaye alianza kutafuta namna ya kuingia kwenye nyumba hiyo ambayo mlango wake ulifungwa na komeo kwa ndani.

Jota baada ya kuona hivyo akaamua kuuvunja mlango wa nyumba hiyo kuingia ndani na kwenda moja kwa moja kwenye chumba alicholala mama yake mzazi (jina limehifadhiwa).

Imeelezwa kuwa, baada ya kufika chumbani, Jota alianza kumtisha mama yake kwa kisu alichokuwa ameshika mkononi na baadaye alimkaba shingo na kufanikiwa kumvua ngo ya ndani aliyokuwa amevaa kisha kumbaka.

Wakati Jota akiendelea kubaka, watu waliokuwa jirani na tukio walisikia kelele za mtu akipiga mayowe na walipofika kwenye eneo hilo la tukio waliingia ndani ya nyumba hiyo na kumkuta Jota akitoka kwenye chumba alicholala mama yake. 

Jota alipowaona watu alijalibu kukimbia lakini majirani hao walifanikiwa kumkamata na kumpeleka kituo kidogo cha polisi cha peramiho.

Kamanda Kamuhanda ameeleza kuwa polisi walimhoji mtuhumiwa ambaye alikiri kulitenda kosa hilo na anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara tu upelelezi utakapokamilika.

---
habari imeandikwa na mwandishi wa blogu ya Stephano Mango
 


Comments

12/01/2012 11:15

Ama kweli dunia imekwisha:::

Reply
Evans
12/01/2012 21:29

Ni ugonjwa wa akili,ama yawezekana ni upumbavu uliopita kikomo, ushirikina, bange.
Mungu tusaidie

Reply
Mchome
13/01/2012 03:25

Huyo Kijana inatakiwa akapime akili,maana hiyo siyo akili ya kawaida labda kama ni ya Imani za kishirikina

Reply
hezron jabuya
13/01/2012 12:01

huyo afungwe maisha

Reply
John lochiri
15/01/2012 05:44

Yesu na mitume,,, ama kweli dunia yaisha,,

Reply
Abdallah Mohamed
15/01/2012 05:48

Matendo kama haya inatakiwa mahakama itoe fundisho

Reply
Franklin
15/01/2012 06:54

Ndio vijana wa kileo..sasa hapo mama mzazi anafanywa hivyo hao wengine je??

Reply
juma
15/01/2012 07:17

*ammakwery dunia imeisha minazan uyo kjna mwehu.

Reply
juma
15/01/2012 07:17

*ammakwery dunia imeisha minazan uyo kjna mwehu.

Reply
juma
15/01/2012 07:17

*ammakwery dunia imeisha minazan uyo kjna mwehu.

Reply
JACOB
15/01/2012 10:51

Huyo tayari amelaaniwa adhabu ya ALLAH itamwadhibu na serikali pia impe fundisho iwe funzo kwa wengine wenye mawazo kama hayo.

Reply
JACOB
15/01/2012 10:51

Huyo tayari amelaaniwa adhabu ya ALLAH itamwadhibu na serikali pia impe fundisho iwe funzo kwa wengine wenye mawazo kama hayo.

Reply
VICTOR MARO
16/01/2012 01:37

E! MUNGU WANGU! NAOMBA UMZUIE HUYU IBILISI ASHINDE

Reply
abdul
16/01/2012 11:57

huyu atakuwa katumwa na mganga wa kienyeji..dah

Reply



Leave a Reply