Kwa uchambuzi wa kina HAKUNA ugomvi wala uhasama kati ya Ndugu Kikwete na Ndugu Slaa; kama binadamu HAKUNA KABISA.
Wapambe wachache wa Mh Kikwete kama Rais ambayo ni taasisi wanajaribu kutengeneza hii taswira ya eti ugomvi na uhasama ili waweze kuhalalisha kuweza kumdhuru Ndugu Slaa vile wanahofia sana umaarufu wake unaozidi kufunika hicho wanachodhani ni umaarufu wa Ndugu Kikwete... Ni siasa uchwara kama alivyoziita Ndugu Rostam Aziz...
Ni siasa ambazo hapo nyuma nchini Kenya zilizaa siasa za kuuliwa kiongozi yeyote aliyeonekana kuwa kipenzi cha wananchi zaidi ya Rais...ni siasa zilizozaa mauwaji ya Tom Mboya, JMKariuki, na Robert Ouko. Dr. Slaa alisimamishwa na Chadema kugombea Urais 2010 na kama wizi wa kura ulizuia ushindi wa Dkt. Slaa kuwa Rais bado hiyo si kisa kati ya Dkt. Slaa na Dkt. Kikwete... Hapana... hilo ni tatizo kati ya CCM na Chadema; kati ya CCM na Watanzania waliochoka ukiritimba wa utawala wa chama kimoja kwa nusu karne.... HICHO NI KISA KATI YA CCM NA WATANZANIA KILICHOIMBUA KASI YA KUDAI KATIBA MPYA NA TUME YA UCHANGUZI ILIYO HURU... SI SWALA BINAFSI KATI YA Dkt. SLAA NA Dkt. KIKWETE LAKUMALIZWA NA ETI KWA KUNYWA CHAI PAMOJA IKULU... Rais Kikwete asijiruhusu kushawishiwa kukubali dhana potofu kuwa eti Dkt. Slaa ni adui yake... Hakuna kitu kama hicho.
Adui wa Dkt. Kikwete ni kupanda kwa bei ya sukari na kuongezeka kwa bei ya umeme; ni kuzidi kudorora kwa uchumi kwa ujumla; na mawazo ya Rais yaelekezwe kwenye adui hao na wala hana haja ya kukutana na Dkt. Slaa eti kuyamaliza.. Kumaliza yepi? Bei ya sukari, mchele, mafuta ya taa na umeme au?
Tuachane na dhana hizi za kijinga za wanasiasa na wanausalama uchwara wanaojikomba kwa Mh Rais ili awapatie ulaji kwa kumwambia eti adui yake mkuu ni Dkt. Slaa vile eti Dkt. Slaa anakinyongo kushindwa kuwa Rais shauri ya wizi wa kura... Huo ni ujinga utokanao na kukataa kukubali ukweli ulio wazi kuwa mwaka 2010 Dkt. Slaa katu hakujipanga kwa mtandao wa miaka kumi wa kuusaka Urais ulioundwa na ndugu na marafiki (ambao hawakuwa wale waliokutana barabarani) na uliogharamiwa na pesa za wizi kama ule wa EPA ...Si hulka ya Dkt. Slaa na hana sababu ya kuyatafisiri matokeo tata ya uchaguzi wa 2010 kama mambo binafsi kati yake na ndugu yake Mtanzania mwenzake Dkt, Kikwete.
Hoja hii ya eti Rais Kikwete amwalike Dkt. Slaa Ikulu wayamalize inatia kinyaa na kudhalilisha dhana nzima ya taasisi ya Urais.
Mwl. Lwaitama


RSS Feed