Nahodha wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars), Sophia Mwasikili ameondoka Tanzania alfairi ya Januari 30, 2011 kwa ndege ya Turkish Airlines kwenda Uturuki kucheza mpira wa kulipwa.

Mwasikili ataichezea "Lüleburgaz Gücü Kulübü" inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ya Wanawake nchini humo.

Mchezaji huyo kiungo wa kati wa Twiga Stars aliyekuwa akichezea timu ya Sayari Women amejiunga na klabu yake hiyo mpya kwa mkataba wa miaka miwili.

Awali Mwasikili alitakiwa kujiunga mapema na timu hiyo lakini alilazimika kusubiri kwanza mechi ya marudiano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Twiga Stars na Namibia (Brave Gladiators) iliyochezwa Januari 29 mwaka huu.
 


Comments

Evans
01/02/2012 05:11

Kila la kheri Sophia

Reply



Leave a Reply