UMUHIMU WA KUANDIKA WOSIA
  • Unaweka mambo bayana kuondoa utata kwa familia na jamaa zako.
  • Unamchagua msimamizi wa mirathi unayemtaka wewe.
  • Unatoa maelezo ya wapi mwili wako uhifadhiwe, taratibu zitakazotumika kuuzika mwili wako na jinsi gani mali yako igawanywe kama upendavyo wewe na kwa mujibu wa Sheria.
MASHARTI YA WOSIA
  • Mtoa wosia lazima awe na akili timamu.
  • Awe ametimiza miaka kumi na nane (18) na kuendelea.
  • Uonyeshe tarehe,mwezi na mwaka ulioandikwa.
  • Uonyeshe majina ya warithi.
  • Mtoa wosia ahusishe mali zake binafsi na si za mtu mwingine.
  • Wosia ni siri wanufaika hawatakiwi kuujua.
  • Ushuhudiwe na mashaidi wawili,  kwa  mtoa wosia anaye jua kusoma na kuandika na kwa yule asiye jua kusoma ua kuandika mashuhuda wake lazima wawe wanne na wajue kusoma na kuandika.
  • Mtoa wosia lazima aweke saini yake,na kama hajui kusoma na kuandiaka aweke alama ya dole gumba la mkono wa kulia.
  • Mashuhuda lazima waweke saini zao tena kwa wakati mmoja.
SABABU ZINAZOWEZA KUSABABISHA MTOA WOSIA KUTOMRITHISHA MRITHI WAKE
  • Kumtelekeza mtoa wosia pale ambapo anaumwa na kuhitaji msaada.
  • Kufanya uzinzi na mke wa mtoa wosia.
  • Endapo kifo cha mtoa wosia kitakuwa kimesababishwa na mrithi.
1. THAMANI YA MALI: 1 -50,000,000
  • Kutayarisha : 5,000/=
  • Kutunza      : 5,000/=
  • Marekebisho: 5,000/=
2. THAMANI YA MALI: 51,000,000-200,000,000
  • Kutayarisha: 20,000/=
  • Kutunza      : 20,000/=
  •  Marekebisho: 20,000/=
3. THAMANI YA MALI: 201,000,000- 500,000,000
  • Kutayarisha : 30,000/=
  • Kutunza      : 30,000/=
  • Marekebisho: 30,000/=
4. THAMANI YA MALI: 501,000,000- Nakuendelea
  • Kutayarisha : 50,000/=
  • Kutunza      : 50,000/=
  • Marekebisho: 50,000/=
Wasiliana na RITA kupitia anuani zifuatazo:

Afisa Mtendaji Mkuu/Kabidhi Wasii Mkuu
Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA)
Mtaa wa Kipalapala,
Kiwanja Na.516
Upanga
S.L.P 9183
Dar es Salaam.

Simu Namba +255 - 22 – 2153069
Nukushi +255-22-2153075   

----
Ikiwa ulipitwa na masomo ya awali, bofya hapa na hapa kuyarejea.
 


Comments

E!
17/01/2012 07:09

Cha ajabu mie ambaye inabidi nitoe mfano bado hata kuanza kuandika sijaandika.Kwanza mimi nina nini bana? ooh kumbe nina kiwanja ambacho hakijapimwa na nina wadogo zangu nane achilia mbali wakubwa zangu tisa.
Okay natambua kuna umuhimu huu.
Wacha nikaandike najua sio uchuro.Kama ingekuwa uchuro yule mzee wa kijijini kwetu,aliamua kujichongea sanduku la kuweka mwili wake pindi atakapofariki maajabu alidumu zaidi ya miaka ishirini mbele. Huwezijua labda wale wenye imani za ziada mpaka wanaamini mambo ya uchuro huenda wakaamini kuwa ukiandika wosia utaendelea kuishi hata miaka thelathini mbele..

Reply
Ernest
17/01/2012 21:07

Kati ya sababu zilizotolewa za kutomrithisha mrithi ni uzinzi na mke wa mtoa wosia. Je mke akizini nae inakuwaje au inahusu wote?

Reply



Leave a Reply